Kudakwashe
Member
- Nov 23, 2014
- 53
- 25
Duru za uchunguzi zinaeleza kwamba Chenge amehojiwa na Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa ( Takukuru ) na kuthibitisha alilipwa kiasi hicho cha fedha kutoka kwenye fedha za ESCROW kiasi cha Tsh 300 bilion.
Chenge alipoulizwa kiasi hicho kilikua cha nini alipata wakati mgumu kujibu , lakini mwisho alijibu ni ada ya ushauri.
'' Imethibitika pasishaka kwamba Chenge amepewa kiasi cha Sh 1.6bilion.Ameithibitishia Takukuru alipohojiwa , " zilisema duru za habari za kuaminika kutoka ofisi ya Bunge.
Chanzo kiliongeza : "Awali alipoulizwa ni za nini hakuweza kutoa jibu la haraka sana , lakini mwisho akasema ni za ushauri ".
Uchunguzi zaidi umebaini kuwapo kwa wanufaika wengine wa fedha hizo lakini ( majina yao yamehifadhiwa baada ya kukosekana kujitetea kama maadili ya taaluma yanavyoeleza ).Hata hivyo , juhudi za kuwatafuta zinaendelea na wataanikwa.
Lakini tayari pia Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anna Tibaijuka amekiri kupokea kiasi cha Sh 1 bilioni kutoka kwa mtuhumiwa wa wizi wa ESCROW.
MAJIBU YA CHENGE.
Alipoulizwa Chenge kuhusiana na tuhuma hizo alijibu kama ifuatavyo :
MWANDISHI : Mheshimiwa shikamoo pole kwa majukumu yote , samahani mimi mwandishi habari gazeti la MWANAHABARI kuna taarifa ambazo zikielekeza kuhusika kwako na kashfa ya Escrow , unazungumziaje.
CHENGE : Na mimi nimeona na kusikia kwenye mitandao ya kijamii yakiwemo Magazeti kunihusisha na suala hilo lakini mimi siwezi kusema chochote.
MWANDISHI : Kwanini usitoe ufafanuzi zaidi ili ukweli ujulikane kama unahusika au uhusiki kuliko kukataa kuzungumza ?
CHENGE : Mimi sitaki kabisa kuzungumzia suala hilo.
MWANDISHI : Au unakataa kuzungumza suala hili kwa sababu unaongea na mimi kwenye simu ungependa tuonane ana kwa ana. ?
CHENGE : Hapana hata ukija tukionana sitakua tayari kuzungumza chochote.
MWANDISHI : Mheshimiwa lakini kwa ujumla unalionaje suala la Escrow.
CHENGE : Sijui lolote.
MWANDISHI :Kweli hujui suala la Escrow Account ?
CHENGE : Kukata simu bila kujibu swali wala kuagana.
Chanzo: Mwanahabari :
Chenge alipoulizwa kiasi hicho kilikua cha nini alipata wakati mgumu kujibu , lakini mwisho alijibu ni ada ya ushauri.
'' Imethibitika pasishaka kwamba Chenge amepewa kiasi cha Sh 1.6bilion.Ameithibitishia Takukuru alipohojiwa , " zilisema duru za habari za kuaminika kutoka ofisi ya Bunge.
Chanzo kiliongeza : "Awali alipoulizwa ni za nini hakuweza kutoa jibu la haraka sana , lakini mwisho akasema ni za ushauri ".
Uchunguzi zaidi umebaini kuwapo kwa wanufaika wengine wa fedha hizo lakini ( majina yao yamehifadhiwa baada ya kukosekana kujitetea kama maadili ya taaluma yanavyoeleza ).Hata hivyo , juhudi za kuwatafuta zinaendelea na wataanikwa.
Lakini tayari pia Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Anna Tibaijuka amekiri kupokea kiasi cha Sh 1 bilioni kutoka kwa mtuhumiwa wa wizi wa ESCROW.
MAJIBU YA CHENGE.
Alipoulizwa Chenge kuhusiana na tuhuma hizo alijibu kama ifuatavyo :
MWANDISHI : Mheshimiwa shikamoo pole kwa majukumu yote , samahani mimi mwandishi habari gazeti la MWANAHABARI kuna taarifa ambazo zikielekeza kuhusika kwako na kashfa ya Escrow , unazungumziaje.
CHENGE : Na mimi nimeona na kusikia kwenye mitandao ya kijamii yakiwemo Magazeti kunihusisha na suala hilo lakini mimi siwezi kusema chochote.
MWANDISHI : Kwanini usitoe ufafanuzi zaidi ili ukweli ujulikane kama unahusika au uhusiki kuliko kukataa kuzungumza ?
CHENGE : Mimi sitaki kabisa kuzungumzia suala hilo.
MWANDISHI : Au unakataa kuzungumza suala hili kwa sababu unaongea na mimi kwenye simu ungependa tuonane ana kwa ana. ?
CHENGE : Hapana hata ukija tukionana sitakua tayari kuzungumza chochote.
MWANDISHI : Mheshimiwa lakini kwa ujumla unalionaje suala la Escrow.
CHENGE : Sijui lolote.
MWANDISHI :Kweli hujui suala la Escrow Account ?
CHENGE : Kukata simu bila kujibu swali wala kuagana.
Chanzo: Mwanahabari :