Sildenafil Citrate
JF-Expert Member
- Jan 29, 2021
- 573
- 2,553
Klabu ya Chelsea imemfuta kazi kocha wake Mkuu Thomas Tuchel kutokana na uwepo wa mwendelezo mbaya wa matokeo unaoikabili timu hiyo.
Kufurushwa huku kumetokea masaa machache baada ya kupokea kipigo cha goli moja kwenye michuano ya UEFA kutoka kwa Dinamo Zagreb.
Tuchel alijiunga na timu hii mwaka 2021 ambapo alifanikiwa kushinda taji la ligi ya mabingwa Ulaya (UEFA) mwaka huohuo.
Kocha huyu ameondoka akiwa amecheza michezo 6 kwenye ligi Kuu ya Uingereza (EPL) msimu huu huku akishinda mechi 3, droo 1 na kupoteza michezo 2.
Ameiacha timu hiyo ikiwa inashikilia nafasi ya 6 kwenye msimamo wa ligi kuu ya EPL.