idoyo
JF-Expert Member
- Jan 13, 2013
- 3,051
- 1,423
Akizungumza kwenye kipindi chake cha mwisho, Dira ya Dunia, mtangazaji mahiri wa radio na televisheni, Charles Hillary, ametangaza kustaafu rasmi kazi hiyo. Amefanya kazi na BBC-Swahili tangu mwaka 2006 mpaka Aprili, 2015 akitokea DW-Swahili alipoanza mwaka 2003 baada ya kuondoka Radio One alipofanya kuanzia mwaka 1994. Kabla ya hapo aliwahi pia kufanya kazi na RTD. Amesema ametimiza umri (wa zaidi ya miaka 55) wa kustaafu kwa mujibu wa sheria.
Last edited by a moderator: