Mkuu
Eiyer sidhani kama kujua ni chanzo cha uovu, kwasababu uovu haujaanza na mwanadamu, kwa maana nyingine uovu ninaweza nikasema ni dhambi, Kutokana na shughuli za shetani katika bustani ya Edeni inaonekana dhambi ilikuwepo ulimwenguni kabla Adamu na Hawa hawajatenda dhambi...
Tukirudi katika Biblia haielezi dhambi ilivyoanza katika asili yake, inaelezewa jinsi ilivyoingia kwa wanadamu, Mungu alipowapa wanadamu ulimwengu ulioumbwa aliweka mpaka, kwasababu uhuru kamili usingelingana na hali ya mwanadamu ya kuwa mfano wa Mungu
Mwanzo 2:15-17
15 Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.
16 Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula,
17 walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.
Lakini mwanadamu alivuka mpaka Mungu aliomuwekea hivyo aliangukia katika dhambi, Alitaka kutawala maisha yake mbali na Mungu na kuwa mwamuzi wa mwisho kuhusu mambo yaliyo mema na Mabaya Mwanzo 3:1-6
Kiburi kilikuwa kiini cha dhambi ya mwanadamu, Warumi 1:21-23
21 kwa sababu, walipomjua Mungu hawakumtukuza kama ndiye Mungu wala kumshukuru; bali walipotea katika uzushi wao, na mioyo yao yenye ujinga ikatiwa giza.
22 Wakijinena kuwa wenye hekima walipumbazika;
23 wakaubadili utukufu wa Mungu asiye na uharibifu kwa mfano wa sura ya binadamu aliye na uharibifu, na ya ndege, na ya wanyama, na ya vitambaavyo.
1 Yohana 2:16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.
Isaya 10:15 Je! Shoka lijisifu juu yake alitumiaye? Je! Msumeno ujitukuze juu yake auvutaye? Ingekuwa kana kwamba bakora ingewatikisa waiinuao, au fimbo ingemwinua yeye ambaye si mti.
Obadia 1:3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Mwenye makao yako juu sana; Asemaye moyoni, Ni nani atakayenishusha mimi?
Dhambi ya mwanadamu ilianza moyoni mwake mwenyewe, tendo la kutotii lilikuwa matokeo yake
Mithali 4:23 Linda moyo wako kuliko yote uyalindayo; Maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
Yeremia 17:9 Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?
Marko 7:21-23
21 Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,
22 wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.
23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi.
Kwa hiyo kwa muktadha huo tunaweza tukasema chanzo cha uovu tunaweza tukasema ni kiburi, ni chombo ambacho shetani alikitumia na kufaulu alipomjaribu mwanadamu ili amwasi mwumbaji wake Mwanzo 3:1-6
Mithali 16:18 Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko.
Danieli 5:20 Lakini moyo wake ulipoinuliwa, na roho yake ilipokuwa ngumu akatenda kwa kiburi, aliuzuliwa katika kiti chake cha enzi, nao wakamwondolea utukufu wake.
Kiini cha kiburi ni ubinafsi, furaha ya mwenye kiburi siyo kuwa na kitu fulani tu, bali kupata zaidi kuliko watu wengine, kuwa bora zaidi kuliko watu wengine, Kiburi pia ni dhambi aichukiayo Mungu
Mithali 8:13 Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; Kiburi na majivuno, na njia mbovu, Na kinywa cha ukaidi pia nakichukia.
Mithali 16:5 Kila mwenye moyo wa kiburi ni chukizo kwa Bwana; Hakika, hatakosa adhabu.
kwa hiyo ukijaribu kuangalia kwa undani zaidi chanzo cha uovu hakitokani na mwanadamu, lakini mwanadamu ameukuta uovu tayari upo, kwa hiyo kujua sidhani kama ni chanzo cha uovu, chanzo cha uovu kwa maana nyingine kinatokana na shetani, hata kule Edeni shetani ndio muhusika pia...