Channel ya Sinema Zetu Azam Tv

poa tu

JF-Expert Member
Jun 16, 2016
1,173
1,655
Lengo la hii channel nadhani ilikuwa ni kuitangaza zaidi tasnia ya filamu za Bongo. Kinachofanyika sasa ni upuuzi mtupu utafikiri ni Channel ya bure vile.

Kwa hatua ambayo industry ya film hapa kwetu imefikia na uwingi wa kazi nzuri sokoni, inashangaza mno kuona nyinyi mnarudia movie zile zile tangu mwaka juzi! Halafu sasa ni bora movie zenyewe mnazozirudia rudia kila siku ni bora zingekuwa nzuri basi na zenye ubora wa kuridhisha. Ni vifilamu vya ajabu ajabu tu tena vingi vya zamani mno.

Hakika Bongo movie wanayo sababu ya kuwalaumu kwa sababu kama channel pekee ya filamu za nyumbani ilitakiwa muwe chachu ya kuwafanya watu wapende vya nyumbani kwa kuwaletea filamu tofauti tofauti kila siku ili wakosoe na kushauri na sisi siku moja tufikie japi robo ya Afrika magharibi (Kiswahili kinakua ati). Kusema na ule ukweli, wengi wa sisi Watanzania ni wachache sana wanaoweza kuthubutu kuingia dukani na kununua filamu ya Bongo kwa sasa. Sasa mtu huyu akiingia kwenye channel kama hii yenu akakuta vitu vibovu vibovu kama mnavyoleta sasa ni lini atashawishika kupenda vya nyumbani?

Huenda ugumu wa kuonesha filamu tofauti tofauti na nyingi unakuja kwenye mikataba na wenye filamu zao (gharama) basi mbuni kitu kingine katika kuthamini gharama tunazolipa sio upuuzi huu.
 

Similar Discussions

3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom