Hapo dar panahitaji nguvu kubwa mno,kwa sababu watu wa hapo bado wako gizani sana,
Kamanda cheza nao hao mpaka wabadirike.
Katika miji ambayo kama uchaguzi unakuwa free and fair basi jiji la Dar CCM haitashinda hata kiti cha udiwani kimoja achilia mbali ubunge. Uchaguzi wa 1995, CCM walipoona kuwa wanashindwa kwa kishindo walichofanya ni kuvuruga uchaguzi wa Dar ambao ulirudiwa baada ya wiki kadhaa.
Tatizo kubwa la Dar ni kuwa wengi ni watafutaji na wapo busy hasa na mambo yao ya kimaisha kutokana na ugumu wa kuishi jijini. Watu wengi kama watajitokeza kupiga kura basi CCM haitakuwa na lake. Kinachofanya Dar kuonekana ni legelege kwenye upinzani ni mbinu za CCM ambazo husema kuwa Dar is a strategic city hivyo kuwa chini ya upinzani ni kuimaliza CCM, hivyo hutumia kila mbinu za ulaghai wa kura ili wajitangaze wameshinda. Na kwa watu wa Dar suala la kulinda kura linaingia palepale kwenye maisha magumu ya jiji. Kama CDM inahitaji hasa kuchukua nchi Haina kazi kubwa sana ya kufanya Dar zaidi ya kuahamasisha watu kupiga kura na kulinda kura zao, kuhusu suala la nani watampigia hilo ni dhahiri kuwa yeyote isipokuwa CCM.