Changamoto za NIDA saa za lala salama

Changamoto za NIDA saa za lala salama

eddy

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2007
Posts
17,080
Reaction score
12,300
Wakati mkuu wa kaya kasema hakuna muda wa nyongeza kwa atakayechelewa bado changamoto ni nyingi hapa nitazungumzia chache:

1. Watu bado ni wengi walioko kwenye foleni na waliohudumiwa hawajapata namba na hazijulikani zitatoka lini.

2. Huduma ya nida inatolewa wilayani hivyo wananchi wanaacha shughuli za shamba kwenda kupanga foleni siku nzima na hakuna la maana wanaloambulia kwani unakuta wilaya nzima mashine ni moja au mbili tofauti na tume ya uchaguzi walikuwa na mashine kila kata tena zaidi ya moja

3. Mtandao wa NIDA uko slow sana sijui hizo server zao wamezinunua china? Sitegemei server kama chubb au LG zinaweza kuwa hivi?

4. Wakati huu wa masika barabara nyingi ni changamoto na maeneo mengine madaraja yamesombwa na maji hivyo wananchi wameamua kusema potelea mbali

5. Wananchi wanaona kazi ya namba za NIDA ni kusajili simu wanaposajili huzitupa

6. Baadhi ya familia wameamua kuwa na line moja tu ya familia badala ya zamani itakuta familia ina simu tano yaani baba, mama, watoto, dada wa kazi, mlinzi, shambaboy na kila simu ilikuwa na line mbili, sasa inabaki simu moja yenye line moja au mbili hivyo tutegemee mapato ya simu kushuka.

7. Wapo waliosajili line kwa kutumia namba za majirani au ndugu waliopata namba za NIDA hivyo zoezi kupoteza maana.

8. Wananchi wanaona hayo ni manyanyaso tu, kwani wakati wa kuandikisha wapiga kura zoezi lilifanyika kwenye kata na mitaa na mashine zilikuwepo za kutosha na zoezi hili lilichukua mwezi mmoja na kila mtu alipata kitambulisho chake pale pale.

Sasa kwanini utaratibu ule ule kwa kutumia mashine zile zile za tume ya uchaguzi au kutumia wafanyakazi wale wale wa tume ya uchaguzi kwanini haukutumika kurahisisha zoezi?
 
Sio kweli mkuu huku kwetu karibu 90 %wamepata number waliobaki ni wenye matatixo na viambata tuache mazoea ndiyo yanaponza wengi

Sent using i phone x
Namisururu vipi imeisha? Server kutokufanyakazi nazo vipi? Raia wakigeni kutokupata namba na hakuna namna ya kuangalia kwenye mtandao wenu je?

Unaweza sema watu wamepata kumbe wamesema poteleambali itakavyokuwa na iwe
 
Mapato hayawezi kushuka. Ni watu wachache sana wasioweza kuishi na mawasiliano kwa dunia yetu ya leo.
 
Mapato hayawezi kushuka. Ni watu wachache sana wasioweza kuishi na mawasiliano kwa dunia yetu ya leo.
Tayari makampuni yameanza kulalamika kuwa usajili uko 50% tu, ngoja tuone hiyo 202020
 
Zoezi hili litaleta usumbufu kwa watu wote watakaofungiwa na waliokwisha kujiandikisha.

Mawasiliano yatakua ya tabu pande zote hivyo inaweza kuleta mtafaruku kwa wananchi.

Naimani bado muda utaongezwa zaidi na hakuna line zitakazofungiwa, maana mfungiaji nae anaweza kosa mawasiliano ya maana na watu wake muhim watakaokuwa bado hawajajiandikisha hivyo ataongeza muda.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huku lindi zoezi limesimama kutokana na uandikishaji wa wapiga kura

Hivyo ukienda ofisi za nida huikuti mtu,

HD Sasa sina namba, na niliniandikisha kitambo sanaaaa,

Kwa hali ilivyo, wafunge tuh, nishachoka,

Kwanza hii process Inataka kutumika kweny kampeni, mataga watatumia kujisifia kuwa 90% ya watanzania hawakuwa na vitambulisho lkn Sasa karibu 99.99%, wana vitambulisho

Hili zoezi ni kinyaa tuh, watakavyoamua potelea mbali,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom