Chama cha Walimu( CWT) ni jipu

Ruyama

JF-Expert Member
Sep 6, 2019
367
561
Hakika walimu tunaonewa,kunyonywa na kukandamizwa na hiki chama tokea kilipo anzishwa hadi leo.

Binafsi ninakatwa makato makubwa elfu 30 kila mwezi na hichi chama lakini kila baada ya miezi 3 ninapata gawio la elfu 5 tuu,cha ajabu May Mosi ya mwaka huu hatujapewa matisheti wamesema eti zilipelea

Mwalimu akistaafu CWT inampa mabati 15 sasa jiulize amechangia shillings ngapi aje apewe mabati 15, iko hivi walimu waliostaafu 2019 hadi leo hii hawajapewa hayo mabati 15 mwalimu huyo mstaafu amefatilia wee lakini anapigwa kiswahili njoo siku fulani hadi leo 2021 tunaelekea katikati ya mwaka hajapewa.

CWT imejenga majengo makubwa nchini kote Tanzania wameyapangisha lakini mwalimu hanufaiki hata shilling 100, viongozi wa CWT wanakaa nyumba za bure, usafiri bure,mawasiliano(vocha bure),vikao wanajilipa mapesa mengi.

Nchi hii inawalimu wengi lakini hatujawahi nufaika na hichi chama.Kuna chama kipya kilianzishwa kinaitwa CHAKAMWATA hiki chama kilikuwa mkombozi CWT kuhofia kupoteza wanachama kikapigwa marufuku kikaondolewa.

Tumeshapaza kelele nyingi mnoo juu ya hiki chama maana sio mkombozi kwa mwalimu,sijui ninani aje atuondolee haya machungu,hayati Magufuli alishindwa na alikuwa mwalimu .

Ndugu zangu nibora mjue adha tunayoipata walimu kupitia hiki chama kandamizi na cha kinyonyaji.
 
Njia iliyobaki kwa walimu ni kugomea uwepo/namna hicho chama kinavyoendeshwa,hakuna mwanasiasa atakaye_feel maumivu ya mwalimu,wa kuiondoa cwt ni walimu wenyewe,maandamano/mgomo ndio njia iliyobaki kukomesha adha ya hiko chama.
Shida ya kada ya ualimu,ni uoga na kukosa umoja,walimu wanauwezo wa kudai haki toka kwa wakuu wao wa shule tu,hao ndio size yao,sio sehemu zingine.
 
Hiko chama kinachangia fedha wakati wa kampeni kwahiyo hata upige kelele vipi hakuna kitakachotokea. Magufuli aliwaambia wapunguze makato hawajatekeleza hadi amefariki. Kuna walimu walijitoa CWT wakaingia CHAKAMWATA. Baada ya miezi 6 wakarudishwa kwa lazima.
 
CWT ni tawi la CCM! Hivyo usitegemee maajabu. Hiyo 2% ya makato kila mwezi, ni wizi tu. Kuna sababu gani ya kuwakata wanachama kwa mtindo wa asilimia?
Na wakati wanatofautiana mishahara! Yaani mwalimu huyu anakatwa elfu 30, mwingine elfu 10! Mwingine elfu 15!! Kama siyo wizi ni nini hiki!! Haishangazi kuona viongozi wa hiki chama wakitumia fedha za walimu kwenda kuangalia mpira wa Taifa Stars kule Cape Verde! Ni kwa sababu wanalindwa na kulelewa na Serikali ya CCM!

Lakini pia hicho chama kinatakiwa kiwatetee wanachama wote kwa usawa! Sasa kwa nini wanachama wote wasikatwe makato yanayo fanana? Yaani flat rate? Naamini aliyepitisha aina hii ya sheria ya kuwakata walimu ada ya hicho chama kwa mfumo wa asilimia, basi alikuwa ni Mchawi au ni mwendawazimu!

Chama kina wanachama lukuki nchi nzima, kina vitega uchumi vya majengo ya kupangisha kila Mkoa! Kina jengo la Mwalimu House Dar es salaam! Kuna Benki ya Walimu! Lakini vyote hivi havitoshi!

Na chakushangaza zaidi, hiyo benki ina matawi Dar es salaam tu kama sikosei! Na wakati wana majengo karibia kila Mkoa nchini! Riba iko juu! Kiasi cha kuwafanya walimu kukimbilia benki za kibiashara kama CRDB, NMB, nk.
 
Njia iliyobaki kwa walimu ni kugomea uwepo/namna hicho chama kinavyoendeshwa,hakuna mwanasiasa atakaye_feel maumivu ya mwalimu,wa kuiondoa cwt ni walimu wenyewe,maandamano/mgomo ndio njia iliyobaki kukomesha adha ya hiko chama.
Shida ya kada ya ualimu,ni uoga na kukosa umoja,walimu wanauwezo wa kudai haki toka kwa wakuu wao wa shule tu,hao ndio size yao,sio sehemu zingine.
Hakika
 
CWT ni tawi la CCM! Hivyo usitegemee maajabu. Hiyo 2% ya makato kila mwezi, ni wizi tu. Kuna sababu gani ya kuwakata wanachama kwa mtindo wa asilimia?
Na wakati wanatofautiana mishahara! Yaani mwalimu huyu anakatwa elfu 30, mwingine elfu 10! Mwingine elfu 15!! Kama siyo wizi ni nini hiki!! Haishangazi kuona viongozi wa hiki chama wakitumia fedha za walimu kwenda kuangalia mpira wa Taifa Stars kule Cape Verde! Ni kwa sababu wanalindwa na kulelewa na Serikali ya CCM!

Lakini pia hicho chama kinatakiwa kiwatetee wanachama wote kwa usawa! Sasa kwa nini wanachama wote wasikatwe makato yanayo fanana? Yaani flat rate? Naamini aliyepitisha aina hii ya sheria ya kuwakata walimu ada ya hicho chama kwa mfumo wa asilimia, basi alikuwa ni Mchawi au ni mwendawazimu!

Chama kina wanachama lukuki nchi nzima, kina vitega uchumi vya majengo ya kupangisha kila Mkoa! Kina jengo la Mwalimu House Dar es salaam! Kuna Benki ya Walimu! Lakini vyote hivi havitoshi!

Na chakushangaza zaidi, hiyo benki ina matawi Dar es salaam tu kama sikosei! Na wakati wana majengo karibia kila Mkoa nchini! Riba iko juu! Kiasi cha kuwafanya walimu kukimbilia benki za kibiashara kama CRDB, NMB, nk.
Yaani hiki chama hiki
 
Back
Top Bottom