CHama cha Makahaba chasajiliwa rasmi Malawi

CHama cha Makahaba chasajiliwa rasmi Malawi

i pad3

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2012
Posts
1,518
Reaction score
378
Chama cha makahaba chasajiliwa rasmi By Mwandishi Wetu Imewekwa Sunday, November 11 2012 at 11:26 Malawi
ZAIDI ya makahaba 2000 nchini Malawi
wameungana kwa ajili ya kupinga manyanyaso
wanayoyapata na kuboresha mazingira ya afya,
baada ya kuzindua rasmi chama cha kuwatetea juzi. Kundi hilo linaundwa na vyama visivyo vya
kiserikali vya ndani na nje ya nchi hiyo, ikiwa ni la
kwanza kutambuliwa rasmi na kupewa usajili
katika nchi hiyo ya kusini mwa Afrika ambapo
biashara ya ukahaba inaharamishwa. “Muda wa kujadili kwa pamoja matatizo
yanayowakabili ndio huu. Mnajua namna Polisi na
Mahakama vinavyowabana na kwamba mnahitaji
kupata huduma nzuri za kulinda afya zenu na afya
ya uzazi bila kipingamizi,” alisema mwanasheria wa
haki za binadamu, Chrispin Sibande alipokuwa akizungumza na kundi la wateja wake wapatao 50
ambao ni makahaba.
Source and full article: Mwananchi.co.tz
 
Good, ni vyema kuwatambua hawa viumbe ili kuweza kukusanya Kodi na kuwaweka katika mazingira salama. Kuliko kuwaacha wanazagaa hovyo huku wakijihatarishia Usalama wao na wakihatarisha usalama wa "wateja" wao wanaowafuata mafichoni....
 
Back
Top Bottom