Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha Kijamii (CCK), David Daud Mwajojele, amewasili katika Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Njedengwa, Jijini Dodoma, akiwa ameambatana na mgombea wake mwenza, kwa ajili ya kuchukua fomu za kuteuliwa kugombea nafasi ya Rais na Makamu wa Rais katika Uchaguzi Mkuu 2025.
Baada ya kukabidhiwa fomu hizo na Mwenyekiti wa INEC, Jaji (Rufani) Jacobs Mwambegele, Mwajojele amesema iwapo atachaguliwa kuwa Rais, serikali yake itaandaa mazingira bora kwa watumishi wa umma, ikiwemo kuwajengea nyumba ili waishi maisha yenye hadhi baada ya kustaafu.
Soma Pia: Mgombea Urais wa Chama cha Kijamii (CCK) awasili kuchukua fomu INEC
Amesisitiza kuwa, hilo litasababisha wafanyakazi kutoogopa kustaafu kwa hofu ya kuishi maisha magumu.
Baada ya kukabidhiwa fomu hizo na Mwenyekiti wa INEC, Jaji (Rufani) Jacobs Mwambegele, Mwajojele amesema iwapo atachaguliwa kuwa Rais, serikali yake itaandaa mazingira bora kwa watumishi wa umma, ikiwemo kuwajengea nyumba ili waishi maisha yenye hadhi baada ya kustaafu.
Soma Pia: Mgombea Urais wa Chama cha Kijamii (CCK) awasili kuchukua fomu INEC
Amesisitiza kuwa, hilo litasababisha wafanyakazi kutoogopa kustaafu kwa hofu ya kuishi maisha magumu.