Chama cha ACT-Wazalendo chapitisha katiba ya chama

Chama cha ACT-Wazalendo chapitisha katiba ya chama

Mwl. Kaijage

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2015
Posts
216
Reaction score
214
KWA KUWA tumeamua kupambana dhidi ya rushwa, ufisadi, uzembe na uvivu;

NA KWA KUWA tumeamua kuhakikisha kuwa maliasili ya Nchi yetu Tanzania ni mali ya wananchi wote na kwamba lazima itumike kutokomeza umasikini nchini kwetu na kuleta
maendeleo sawia na endelevu ya kiuchumi, kijamii,kiutamaduni na kisiasa;

NA KWA KUWA tumeamua kujenga Chama cha siasa chenye lengo la kuchochea ujenzi wa Taifa la Kujitegemea, lisilo na unyonyaji wala ubaguzi wa rangi, dini, kabila, jinsia, maumbile, hali ya kipato na kwa kuzingatia misingi ya haki kwa watu wake wote;

NA KWA KUWA tumeamua kushiriki katika ujenzi wa Umoja wa Afrika ili kuwaenzi waasisi wa
ukombozi wa Mwafrika na kujenga bara lenye sauti yenye nguvu na ushawishi katika jamii ya mataifa ulimwenguni;

NA KWA KUWA tumeamua kupigania demokrasia,umoja, utu, uadilifu, uwajibikaji, uzalendo kwa Taifa;

NA KWA KUWA kwa nia moja tumeamua kujenga Chama chenye kufuata misingi ya Ujamaa wa
Kidemokrasia (Democratic Socialism), na misingi asili iliyoasisi Taifa letu (Unyerere) ikiwemo Azimio la Arusha; na

NA KWA wajibu tulio nao wa kujenga, kukuza na kuendeleza demokrasia na utamaduni wa mfumo wa vyama vingi nchini Tanzania;

HIVYO BASI; Sisi Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Taifa wa Chama cha Wazalendo (ACT) uliofanyika Dar es salaam leo tarehe 28 Machi 2015,

Tumepitisha KATIBA MPYA ya Chama chetu itakayojulikana kama KATIBA YA ACT YA MWAKA 2015.
 
Unakera sana. hivi chama hakina msemaji mkaja ni kitu kinchoeleweka? kama mmepitisha katiba turitaraji mtuwekee hapa lakini unacholeta hapa ni dibaji wala siyo katiba.
 
Bora hata ungetoa summary ya mambo ya msingi katika katiba hiyo mliopitisha yatakayosaidia kuthibitisha hayo uyasemayo na yenye kuonyesha ubora(kama upo) ukilinganisha na vyama vingine.
 
Nimesikia habari ya kuanzishwa chama kipya cha siasa. Nimeelezwa kuwa kiuchumi na kijamii kina mrengo wa ujamaa kikifuta azimio la Arusha, Nikaambiwa ni chama makini sana , hata hivyo ningalipenda kukipima kwa katba yake, lengo ni kujiunga na ikiwa nitaridhika nayo. Nimefuatilia sana kwenye mitandao sijaona soft copy . Nilitarajia ingalikuwapo kwa kuwa chama hiki kinajinasibu kwa ku-promote uwazi na demokrasia ya kweli. Je katika mikutano katiba ziligawiwa? Naombeni mwenye katiba husika aitupie humu mara moja
 
Kuna ile ya ACT TANZANIA
hii ya chama kipya hawajatunga
 
Kuna ile ya ACT TANZANIA
hii ya chama kipya hawajatunga
acha utani bwana mi naitaka hiyo ya ACT-wAZALENDO kwa gharama yoyote nataka tusaidiane kuichambua leo mei mosi ,jumatatu nikachukue kadi usifanye masikhara
 
katiba anao mwigulu act hawajapewa cop

haijalishi kama anayo Nape ama Mwigulu ama Samsoni mi naihitaji leo nina muda wa kuianalyse nipeni ushirikiano punguzeni masikhara nina zana zote za kiuchambuzi hapa, Chama ni katiba bwana!
 
Sasa kama hata katiba hujaisoma nu kipi kunakufanya uhamie huko...
 
muone kiongozi mkuu wa viongozi wote atakupatia,
 
Je katika mikutano katiba ziligawiwa? Naombeni mwenye katiba husika aitupie humu mara moja
Kwenye mikutano yao walikuwa busy kugawa kitabu cha Chacha Wangwe badala ya katiba.
 
Nimesikia habari ya kuanzishwa chama kipya cha siasa. Nimeelezwa kuwa kiuchumi na kijamii kina mrengo wa ujamaa kikifuta azimio la Arusha, Nikaambiwa ni chama makini sana , hata hivyo ningalipenda kukipima kwa katba yake, lengo ni kujiunga na ikiwa nitaridhika nayo. Nimefuatilia sana kwenye mitandao sijaona soft copy . Nilitarajia ingalikuwapo kwa kuwa chama hiki kinajinasibu kwa ku-promote uwazi na demokrasia ya kweli. Je katika mikutano katiba ziligawiwa? Naombeni mwenye katiba husika aitupie humu mara moja

Katiba Pamoja na Ilani ya uchaguzi viligawiwa,hiki Chama ni cha uwazi kama msingi wa chama, muone MWALIMU KAIJAGE atakusaidia zaidi.
 
Nimesikia habari ya kuanzishwa chama kipya cha siasa. Nimeelezwa kuwa kiuchumi na kijamii kina mrengo wa ujamaa kikifuta azimio la Arusha, Nikaambiwa ni chama makini sana , hata hivyo ningalipenda kukipima kwa katba yake, lengo ni kujiunga na ikiwa nitaridhika nayo. Nimefuatilia sana kwenye mitandao sijaona soft copy . Nilitarajia ingalikuwapo kwa kuwa chama hiki kinajinasibu kwa ku-promote uwazi na demokrasia ya kweli. Je katika mikutano katiba ziligawiwa? Naombeni mwenye katiba husika aitupie humu mara moja

Usiwe na hofu na gharama,gharama ni ndogo tu,ni kujitoa msukule wa Zitto kila kitu utapata kiulaiini.
 
katiba ni ile ile ya ccm kwa hiyo wewe muombe nape au kinana au lowasa au mwigulu utaipata haraka sana
 
acha utani bwana mi naitaka hiyo ya ACT-wAZALENDO kwa gharama yoyote nataka tusaidiane kuichambua leo mei mosi ,jumatatu nikachukue kadi usifanye masikhara

Jamaa Hajafanya Masiala Ukweli Ni Kwamba Act Tanzania Ndicho Chama Chenye Usajili, Ambacho Katiba Yake Ndio Unaweza Kuipata, Yenye Unazungumzia Mwanachama Kutochaguliwa Kuwa Kiongozi Mpaka Uanachama Wake Ufikishe Myez 6, Alafu Inamtambua Kiongozi Mkuu Wa Chama Ni Mwenyekt, Hii Ya Wahuni Walijibatiza Uzalendo Haina Katiba, Maana Haijasajiliwa.
 
Back
Top Bottom