Chaguo la Mungu mwaka 2010 huyu hapa

Wewe una akili sana.

Mimi naona suala sio kushinda pekee, hata kama atashindwa lakini naona ataleta changamoto kubwa kwa JK katika uchaguzi kuliko kiongozi mwingine yeyote katika upunzani, na hata asilimia watakazopata wapinzani katika urais na ubunge zitaongezeka sababu ya changamoto yake. Hatapotea ila upinzani utaimarika. Lipumba, Mbowe wamegombea urais mara kadhaa ,hivyo hawapo bungeni, je tumewapoteza? I dont think so
 
kuna watu wengine wanaanza uzandiki kusema JK aongezewe miaka 5....nimeshangaa sana kwa lipiii alilofanya??aende zake hy 2010...
 
Mimi naona suala sio kushinda pekee, hata kama atashindwa lakini naona ataleta changamoto kubwa kwa JK katika uchaguzi kuliko kiongozi mwingine yeyote katika upunzani, na hata asilimia watakazopata wapinzani katika urais na ubunge zitaongezeka sababu ya changamoto yake. Hatapotea ila upinzani utaimarika. Lipumba, Mbowe wamegombea urais mara kadhaa ,hivyo hawapo bungeni, je tumewapoteza? I dont think so

Hivi mchango alioutoa Dr Slaa na changamoto aliyoileta kwenye bunge letu unalinganisha na changamoto waliyoileta Lipumba na Mbowe kwa kugombea kwao Urais. Tumia hekima yako nzuri uliyonayo upambanue hili.

Changamoto ya kweli ingeletwa na wapinzani kusimamisha mgombea mmoja.

Mitazamo ya mimi na wewe kwamba kwa mchango alioutoa kama mbunge basi Dr Slaa ataweza kuleta changamoto kwenye Urais ni hatari. Urais na Ubunge ni mambo tofauti kabisa. Ili kuleta changamoto japo kidogo tu atahitaji support ya kifedha ya hali ya juu, na bado atashindwa na fedha hiyo itakayotumika kwenye kugombea Urais ingeweza kutumika kufanikisha kampeni za wagombea ubunge hata 10 na kati yao hata wa 5 wanaweza shinda.

Piga mahesabu vizuri, Dr Slaa akigombea urais kwisha kazi, tutamsahau. Atanyanyasika vibaya. We kumbuka jinsi Mbowe alivyokuwa akikubalika kama mtazamo wako ulivyo sasa kwa Slaa mwaka 2005, na aliambulia nini, amepoteza umaarufu kiasi gani?

Upinzani wawe wajanja, waanzie kujiimarisha serikali za mitaa na bungeni, hapo ndiyo wataweza kupambana vizuri kwenye kinyanganyiro cha Urais. Tanzania haijafikia mahala pa mtu kuwa na wabunge wawili kwenye chama chako halafu ukachaguliwa Urais.

Kwanza propaganda za kinyang'anyiro cha urais utaziweza? Muulize Salim Ahmed Salim atakwambia.
 
..........
7. Aliyethibitika wazi kuwa anajali utu wa Watanzania si muigizaji huku anaenda
safari akiacha watanzania wakilipukiwa na mabomu, wakifukiwa na milima,
wakisombwa na mafuriko, wakifa njaa- [/SIZE][/FONT]Anayejali utu si msanii


....wakifyekwa na mapanga kwa kigezo cha kulipa kisasi (Msoma), wakisombwa na mafuriko (Kilosa), wakipigwa na bunduki kama waasi wa Darfur (Ukerewe), .......

Inauma sana!!!!!!
 
Hivi mchango alioutoa Dr Slaa na changamoto aliyoileta kwenye bunge letu unalinganisha na changamoto waliyoileta Lipumba na Mbowe kwa kugombea kwao Urais. Tumia hekima yako nzuri uliyonayo upambanue hili.

Changamoto ya kweli ingeletwa na wapinzani kusimamisha mgombea mmoja.

.

Nakubaliana na wewe 100% kuwa wapinzani wanabidi wasimamishe mgombea mmoja ili kuleta changamoto zaidi, actually moja kati ya vitu ambavyo hawa jamaa wamekuwa wanadissapoint mpaka sometimes naona kama nao ni "waroho" kama viongozi wa chama tawala na hawana mapenzi ya kweli na malengo ya kukomboa nchi hii,basi ni suala hilo la wao kushindwa kusimamishwa mgombea mmoja,manake linapokuja hilo suala wanaweka mbele maslahi binafsi au maslahi ya chama na kuweka pembeni kwanza maslahi ya nchi na waTZ.

Ninja,swali langu linabaki moja,unamaanisha wapinzani wamsimamishe mgombea dhaifu saiv kwa sababu tu wakimweka aliye strong tutampoteza sababu ushindi kwa JK ni uhakika?
 
nani, slaa, thubutu........................ ni JK kwa kwenda mbele................. rekodi yake ya utendaji inajieleza..................... napendekeza mgombea mwenza awe sophia simba ili amshauri kwa karib zaidi kuhusu uharaka wa kuchukua hatua inapolazimu kufanya maamuzi magumu................................

Kama Sophia Simba ni shangazi yako subiri kumpokea huko kwenu baada ya uchaguzi maana atarudi bush kuliko kuliangamiza taifa letu kiusalama.
 
Hii inamake sense tuachane na wale wachache waliotudanganya mwanzo sasa tutumie vigezo sio hisia tena
 
Hivi ile report iliyosema JK anaongoza kwa 75%
Mbowe 10%
Lipumba 9 %
wameitoa wapi???:)
 

2. Aliyethibitika wazi si kwa hisia kuleta maendeleo ya nchi yetu kwa ujumla wake
si kuiba huku na kupeleke kwa wapiga kura- Maendeleo ya kweli
3. Aliyethibitika kuwa hakuiba pesa za Watanzania ili kununua uongozi- Si mtoa
rushwa wala hakutumia pesa za wizi



Nadhani mkuu huyo mtu hayupo kabisa duniani, labda bado hajazaliwa.
 
Sijui wewe ni muumini wa Kakobe au vipi. Nashangaa sana unaposhindwa kuelewa kwamba maandiko yanatuagiza tuheshimu walioko kwenye mamlaka kwa kuwa mamlaka zote hutoka kwa Mungu. Sasa wewe unapingana na Mungu unaposema mamlaka yaliyopo siyo chaguo lake? Je wataka kumchagulia Mungu mamlaka unayopendezwa nayo wewe na si yeye? Basi kama umeshaona mamlaka iliyopo haitoki kwa Mungu tueleze wazi ni nani anayetakiwa na Mungu kuwepo uchaguzi ujao kwa maana pengine ameshakushushia Roho wake akuongoze. Tafadhali tujuze usilete porojo hapa ndani ya JF
 
Huu si wakati wa M/mungu kutuchagulia kama alichotuchagulia mwaka 2005(sikiri)!ni wakati wa Watanzania kwa ujumla kuamka na kuukataa uongozi mbovu wowote.Tumuombe M/mungu atuongoze katika hilo.naomba Dunia nzima iitikie AMEEN
 
2. Aliyethibitika wazi si kwa hisia kuleta maendeleo ya nchi yetu kwa ujumla wake
si kuiba huku na kupeleke kwa wapiga kura- Maendeleo ya kweli
3. Aliyethibitika kuwa hakuiba pesa za Watanzania ili kununua uongozi- Si mtoa
rushwa wala hakutumia pesa za wizi



Nadhani mkuu huyo mtu hayupo kabisa duniani, labda bado hajazaliwa.

Amekwisha kuzaliwa ila si mzuri wa sura hata tumpende na si mashuhuri hata tumkubali. Jiwe lililokataliwa na waashi limekua jiwe kuu la pembeni. Bahati mbaya ni tuna macho lakini tu vipofu, tuna akili lakini tu usingizini.....nini kitakachotuokoa na hii laana...ashukuriwe Mungu wa mbinguni maana njia zake si zetu na hekima yake ni upumbavu kwa wanadamu. Siku si nyingi huyu umtamanie ataiongoza hii nchi. Jipe moyo muda si mrefu nchi hii itapata jibu la matatizo yake pengine huyu aandikae ndiyo kati ya hao lakini hata aki declare tatizo ni hilo je ni mzuri hata umtamani? Ni mashuhuri hata uamini anaweza... well time is a gud friend one day this day dream will turn to be a reality; I am too young to dispair.
 
Sijui wewe ni muumini wa Kakobe au vipi. Nashangaa sana unaposhindwa kuelewa kwamba maandiko yanatuagiza tuheshimu walioko kwenye mamlaka kwa kuwa mamlaka zote hutoka kwa Mungu. Sasa wewe unapingana na Mungu unaposema mamlaka yaliyopo siyo chaguo lake? Je wataka kumchagulia Mungu mamlaka unayopendezwa nayo wewe na si yeye? Basi kama umeshaona mamlaka iliyopo haitoki kwa Mungu tueleze wazi ni nani anayetakiwa na Mungu kuwepo uchaguzi ujao kwa maana pengine ameshakushushia Roho wake akuongoze. Tafadhali tujuze usilete porojo hapa ndani ya JF

Chaguo la Mungu huchaguliwa na wengi, wa 2005 alichaguliwa na wachache waliotudanganya. Chaguo la Mungu hatokani na hadaa- sasa tunafahamu vigezo 1-7, kwa chaguo la Mungu 2010.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom