Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, kimesema hakina nia ya kususia uchaguzi mkuu 2025, bali kinataka mabadiliko ya mifumo wa uchaguzi ndio uchaguzi ufanyike kwa misingi ya haki kwa washiriki wote.
Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Ali Ibrahim Juma, ameyasema hayo jana Visiwani Zanzibar wakati wa mafunzo ya siku mbili kwa kamati maalum kwa masuala ya uendeshaji wa chama.
Amesema CHADEMA haina maana ya kususia uchaguzi mkuu lakini kufanya mabadiliko ya mifumo ili kuwe na usawa na haki kwa uchaguzi huru.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
“Tunaamini kupitia mabadiliko tutawapa fursa wananchi kushiriki uchaguzi vizuri na matokeo yatangazwe kwa ukweli,”amesema.
Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo viongozi wa CHADEMA wa zamani na wapya ambao wamejaza nafasi kwa walioamua kuhama chama, na kwamba lengo ni kuwa na mipango na mikakati ya kukiinua chama.
Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Ali Ibrahim Juma, ameyasema hayo jana Visiwani Zanzibar wakati wa mafunzo ya siku mbili kwa kamati maalum kwa masuala ya uendeshaji wa chama.
Amesema CHADEMA haina maana ya kususia uchaguzi mkuu lakini kufanya mabadiliko ya mifumo ili kuwe na usawa na haki kwa uchaguzi huru.
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
“Tunaamini kupitia mabadiliko tutawapa fursa wananchi kushiriki uchaguzi vizuri na matokeo yatangazwe kwa ukweli,”amesema.
Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo viongozi wa CHADEMA wa zamani na wapya ambao wamejaza nafasi kwa walioamua kuhama chama, na kwamba lengo ni kuwa na mipango na mikakati ya kukiinua chama.