Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CDM kimekidhoofisha Chama Cha Mapinduzi-CCM wilayani Magu kwa kupukutisha wanachama wake 55 ambao wamejitoa katika chama hicho na kujiunga na CDM.Tukio hilo lilitokea katika operesheni M4C iliyoongozwa na diwani wa kata ya Magu Zena Zacharia aliyehutubia mikutano mbalimbali katika kata tofauti za jimbo la Magu.Wanachama hao waliohamia CDM ni kutoka kata za Mwamanga,Nyigogo,Nkunguru,Mwamabanza na Magu mjini.Katika operesheni hiyo pia vyama vya NCCR,CUF na UDP vilikimbiwa na wanachama 12 waliojiunga na CDM.
Wachunguzi wa mambo ya siasa jimboni Magu wanasema CDM ndicho chama kinachokubalika zaidi jimboni Magu kuliko chama chochote kwa hivi sasa.
Source:Mwananchi Alhamisi uk.14
Wachunguzi wa mambo ya siasa jimboni Magu wanasema CDM ndicho chama kinachokubalika zaidi jimboni Magu kuliko chama chochote kwa hivi sasa.
Source:Mwananchi Alhamisi uk.14