Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 137,499
- 272,183
Asante sana kamanda , hata TEMEKE cdm inasonga mbele kwa kasi mno , keko machungwa , keko mwanga , kurasini , keko juu ccm kwisha kazi .
Kufikia 2014 October kila palipo na balozi wa ccm kuna balozi wa chadema
Asante sana kamanda , hata TEMEKE cdm inasonga mbele kwa kasi mno , keko machungwa , keko mwanga , kurasini , keko juu ccm kwisha kazi .
Lissu awalaumu viongozi wa Chadema Dar
Dar es Salaam. Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, amewaponda viongozi wa Chadema mkoani Dar es Salaam kuwa wameshindwa kufanya kazi za siasa za kukijenga chama hicho.
Lissu amesema viongozi hao wamekuwa wakitumia muda mwingi kukiponda chama tawala, badala ya kutumia nguvu kubwa kukipigania chama chao.
Aliyasema hayo jana alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara, uliofanyika katika Jimbo la Segerea, mkutano ambao ulihudhuriwa na idadi ndogo ya wanachama.
Kwa mujibu wa Lissu, idadi ya wanachama aliowakuta katika Jimbo la Segerea ni ndogo kuliko ya kijiji kimoja cha Jimbo la Singida Mashariki.
Alisema idadi ndogo ya wanachama katika mkutano huo, ni ishara kwamba viongozi wa Chadema mkoani Dar es Salaam, wameshindwa kufanya kazi za siasa.
Alisema viashiria kwamba viongozi wa Chadema, mkoani humo hawafanyi kazi za siasa, vinadhihirishwa na hali katika majimbo ya uchaguzi.
Dar es Salaam ndiyo moyo wa Tanzania, ni jiji linalotakiwa kutegemewa sana kisiasa, lakini cha kushangaza inapata wabunge wawili wa upinzani, inakuwa nyuma na mikoa ya Shinyanga na Kigoma, hii ni aibu, alisema Lissu.
Wilaya ya Ilala ina madiwani wawili tu wa upinzani, viongozi wa Chadema wapo na wameridhika wanaona hilo ni jambo la kawaida, tutaboresha vipi maisha ya wananchi kwa kuwa na madiwani wawili, alisisitiza Lissu.
Alisema mageuzi yoyote makubwa ambayo yamewahi kutokea katika nchi mbalimbali, yalianzia katika miji mikubwa kama Dar es Salaam.
Mageuzi hayaji kwa kulalamika kwamba CCM wametuibia kura, wakati wanaiba kura nyinyi mlikuwa wapi, hiyo inaonyesha kwamba hamfanyi kazi ipasavyo, alisema Lissu.
Alisema malalamiko ya kuibiwa kura hayana msingi katika kipindi hiki kwa sababu kama CCM wanatuhumiwa kuiba kura kwa nini walishindwa kufanya hivyo katika majimbo ya Ubungo, Kawe na Singida Mashariki.
Lissu alisema viongozi wa Chadema wanapaswa kubadilika na kufanya kazi za siasa kama kweli wanataka mabadiliko mwaka 2015 na kwamba vinginevyo, wataendelea kulalamika.
Lissu awalaumu viongozi wa Chadema Dar - Habari - mwananchi.co.tz
Huu ndiyo ukweli.Kufikia 2014 October kila palipo na balozi wa ccm kuna balozi wa chadema
Sehemu ambapo kiwango cha elimu ni kikubwa kama Bukoba inabidi ccm itokomezwe kabisa!
CDM Kagera tunawategemea mpate ushindi mkubwa kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa.
Hongereni kwa kazi nzuri. Hizi bila shaka ni rasharasha, tunasubiri mvua zenyewe mwakani. Our prayers are with you!
Lema anakiua chama nyie mko hapa mnafarijiana.
Poleni misukule.
Huu ndiyo ukweli.
CHADEMA kipo kwenye ulingo wa kisiasa kuanzia 1992 ambapo ni miaka kama 21 kwa sasa ambapo hakina hata mabalozi to match CCM halafu unaongelea miezi ndiyo wataweza kufanya kazi hiyo. You must be joking.
Sitting allowance kwa viongozi wenu wa kitaifa zinataka kuwatoa macho. Uchaguzi wa ndani ya CHADEMA, viongozi wanaogopa kuufanya. Mtaweza kupambana na mazingira na mtandao wa CCM nchini?.
Fikra zako ni placebo ya kisiasa.
Huu ndiyo ukweli.
CHADEMA kipo kwenye ulingo wa kisiasa kuanzia 1992 ambapo ni miaka kama 21 kwa sasa ambapo hakina hata mabalozi to match CCM halafu unaongelea miezi ndiyo wataweza kufanya kazi hiyo. You must be joking.
Sitting allowance kwa viongozi wenu wa kitaifa zinataka kuwatoa macho. Uchaguzi wa ndani ya CHADEMA, viongozi wanaogopa kuufanya. Mtaweza kupambana na mazingira na mtandao wa CCM nchini?.
Fikra zako ni placebo ya kisiasa.