CHADEMA yazidi kukimbiwa na Madiwani wake

CHADEMA yazidi kukimbiwa na Madiwani wake

wandamba

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2014
Posts
510
Reaction score
839
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na madiwani na waliowahi kuwa madiwani wa CHADEMA walioamua kuhamia CCM wakati wa sherehe za kukamisheni maafisa wapya wa kijeshi katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha leo Septemba 23, 2017
IMG-20170923-WA0239.jpg
IMG-20170923-WA0241.jpg
 
Wote hao walikuwa wanajaribu wakajikuta wamesukumiziwa kwenye uongozi.
 
Hakuna kipya hapo, zote ni zilipendwa tu. Hizo ni kick za marudio, wote hao wanaodaiwa kuwa ni madiwani wa CHADEMA walishatangazaga kujiuzuru udiwani wao siku nyingi sana na kuhama CHADEMA na wengine walifukuzwaga, na hilo tukio la kusema wamehamia CCM huenda leo ni marudio yake, maana walishafanya hivyo hivyo mara mbili katika nyakati tofauti tofauti.
 
Hawa ni wapya au ni wale waliohama zamani ??? Hivi si walewale ambao walishapokelewa na polepole???
 
Bado sijaelewa tukio la kuhamia CCM kwenye sherehe za heshima za kijeshi za kuvishana nishani.
Hao madiwani walikuwa wanajeshi?
Au hao wanajeshi ni wanaCCM?
 
Siku zote waerevu huwa ni wachache kuliko wapumbavu,peponi wanakaa watu wema wachache kuliko jehanamu so acha wajinga wanafki na wapumbavu wengi washike njia yao,tubaki waerevu na wenye akili zetu tuendelee kuwaelimisha hao wasiojielewa!!!!
 
Bado sijaelewa tukio la kuhamia CCM kwenye sherehe za heshima za kijeshi za kuvishana nishani.
Hao madiwani walikuwa wanajeshi?
Au hao wanajeshi ni wanaCCM?

Mkuu wacha tu, kila siku tunasema ccm ni chama cha kijeshi watu wanabisha. Leo rais kawanyamazisha wanajeshi huku akipokea wanajeshi maraia huku Taifa likishuhudia.
 
Kimsingi halikuwa eneo sahihi kwa nchi inayoheshimu mfumo wa vyama vingi kunadi madiwani wanaohama vyama kwenye shughuli za jeshi(Jeshi ni Mali ya wananchi na vyama vya siasa ni Mali ya wanachama).Kutumia jukwaa na shughuli za jeshi kukusanya na kuvisimanga vyama vingine kunaacha maumivu kwa kila mwenye kuheshimu haki na kila jambo kwa wakati na mahali pake.Najiuliza kuna shida gani kuruhusu mikutano na hadhara za kisiasa?
 
Arusha inarudi ili tuwaachie wenye chama chao pale Kilimanjaro manake cc Mwanza tulishasahau kama kuna Chagadema!!
 
Hao waliishajitoa siku nyingi mbona au mkuu ulikuwa bado mdogo wakati huo!
 
Back
Top Bottom