jamani,hvi ili hoja kutolewa na kusikika bila matusi ilikwisha shindikana??na hasa watu wanapodiscuss uchadema na uccm humu ndani,kwa bahati mbaya wengi wa watu wanaopost humu ndani ni either viongozi au wana ndoto za kuongoza kwenye ngazi tofauti kwa madai ya kua vijana na kuleta fikra mpya katika kukabiliana na changamoto za dunia ya leo.kila m2 anajua upinzani nchi hii haukuanza jana wala juzi,vijana walikuwepo tangu zamani hata mwl nyerere pia kuna wakati alikua kijana pamoja na viongozi wote wa upinzani,hvi mbna me sijawahi kuckia wakitukanana eti kwa sababu tu ya itikadi zao za vyama??hoja ikija mezani sisi tunaojiita vijana wasomi 2naonesha ni kwa jinsi gani hatuna nguvu ya hoja,hvi kama tunashindwa kujadili hoja ndogo hizi kweli tutaweza kujadili mustakabali wa taifa hili??nyerere alikua na uchungu wa kweli na taifa hili na alikua akikemea mambo mengi lakini ckuwahi kumckia aki2kana ma2si ya nguoni.vijana tunautaka uongozi bila kujua maana yake,2mekua watu wa kubebeshwa mizigo ya hoja ili turopoke bila kujua uzito na madhara yake,2mefundishwa kuchukiana bila sababu,sasa tunabebeshwa hoja ya violance eti ndio itakayoleta mabadiliko bila kujua hasa ni mabadiliko yapi hasa 2nahitaji...vijana 2naharaka na maisha tunataka kuendesha magari punde baada ya kupata shahada zetu,tunanataka mambo makubwa ya kuiga,sio mbaya kutamani mafanikio lakini leo kijana anamaliza degree yake anafanya mambo mawili 2,kutembea kuomba kazi na kuangalia movie,eti nasubiri mchongo..fine..tukikaa two yrs bila kazi mzigo wa lawama 2naitupia serikali kwa nguvu zikifuatiwa na hoja za kisiasa..hvi jamani kina eric shigongo,ruben ndege,kusaga,martin kadinda na wengine wengi hawatoshi kua mifano ya vijana waliomake it from zero??hvi mabadiliko ya nchi yatakuja kwa wote cc kua wanasiasa??hvi ni kweli tukilalamika na kubadilisha vyama ndo viongozi watabadilisha hali ya nyumbani kwa mama zetu??hvi kweli tunaamini kuna m2 atakuja kukupa wewe ajira na mshahara wa kukidhi mahitaji zetu??hvi ni kweli tumegeuzwa mtaji wa siasa za kuwavusha baadhi ya watu kuwafikisha wanapotaka huku 2kisubiri wageuke kutuvuta na cc??kweli wasomi sisi tumeshindwa kutambua kua sasa ni wakati wa kutimiza ndoto??je ni kweli ndoto zetu zitatimia kwa kukubali kutumiwa huku tukifa na kuwaacha walio2somesha na kututegemea??vijana ha2na spirit ya kihustler,2mekua wavivu,tumesahau kua elimu tunayopata dunia ya leo co kwa ajili ya ajira tena,we are not creative,mawazo yetu yamegandishwa na siasa uchwara za nchi hii wakati hao viongozi wanaopingana ni marafiki wakubwa,wamesoma wote,pombe wanakunywa wote,sis tunahubiri kuuana,we are so damn stupid..hatuwazi kua hawa wanao2chochea wamekwisha timiza sehemu kubwa ya ndoto zao,je wewe umetimiza hata moja??mwanao jee??nikiwaangalia vijana huwa natamani waujue ukweli lakini ni kama wamefunikwa na kitambaa cheusi..Tusipoteze muda kuwashabikia watu ambao hatuna hata uhakika ku mwaka 2015 watakua bado kwenye vyama vyao au watakua wamehama,hawa viongozi wanaopingana majukwaani hawana uhasama ambao wanataka sisi tuwe nao ni washkaji wakubwa hata wanawake zao ni mashoga..sasa sisi tunachukiana kwanini??tumecheza kombolela pamoja,kibaba mama pamoja,makida pamoja..leo hii vyama vitufanye tutukanane matusi,vyama vyenyewe hatujui mengi kuvihusu..2nayoyakua ni yale waliyo amua 2yajue,ha2jui makubaliano yao kwa sababu hata wakati vinaanzishwa hawakutuita sasa leo wanatuweka mbele 2pigane wao wakiwa wamelala na wake zao..na sisi tumekua majuha 2nakubali tena kwa hasira zote,hizi degree ze2 ni za kazi gani sasa??amka kijana timiza ndoto zako siasa utaikuta tu,utashabikia siasa haitokupa chochote,utakufa masikini kwa kuwategemea wanasiasa wabadilishe maisha yako,utakimbiwa na mkeo kwa kushindwa kum2nza,life iz too short wake up and go get your money hapo hata wanasiasa watakuheshimu!