CHADEMA yatangaza maandamano Kigoma

Ndugu,

Hebu soma agenda za mkutano huo kabla ya kulaumu na kuelekeza....

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza kufanya maandamano makubwa ya amani mkoani hapa mwezi ujao kupinga hali ngumu ya maisha kutokana na mfumuko wa bei na malipo ya fidia ya Sh. bilioni 94 kwa kampuni ya kufua umeme ya Dowans Tanzania Limited.


Ndugu,

Naona hukusoma vizuri post yangu. Mimi sikulaumu Chadema wala sikuzungumzia maandamano yoyote maalumu. Ndio maana nilizungumzia kuwepo au kutokuwepo kwa maandamano. Nilichosema ni kwamba kufanya maandamano sio tatizo bali tatizo ni kufanya maandamano ya vurugu na uchochezi. Kama nia ni kufanya maandamano ya amani kuonesha hisia ya ugumu wa maisha hakuna tatizo. Hata hivyo, agenda za maandamano kusomeka hivyo peke yake sio ushahidi kwamba yatakuwa ya amani na kisheria. Ndio maana nikawatahadharisha viongozi wangu wa Chadema kwa nia njema tu kwamba wawe makini katika kauli zao. Kwa mfano, kama katika maandamano yao ya amani na mada zao wataipa serikali siku 90 au mia kuondoa kero fulani la sivyo watatumia hatua nyingine za kimabavu hiyo itakuwa kinyume cha katiba.
 
Ndugu,

Naona hukusoma vizuri post yangu. Mimi sikulaumu Chadema wala sikuzungumzia maandamano yoyote maalumu. Ndio maana nilizungumzia kuwepo au kutokuwepo kwa maandamano. Nilichosema ni kwamba kufanya maandamano sio tatizo bali tatizo ni kufanya maandamano ya vurugu na uchochezi. Kama nia ni kufanya maandamano ya amani kuonesha hisia ya ugumu wa maisha hakuna tatizo. Hata hivyo, agenda za maandamano kusomeka hivyo peke yake sio ushahidi kwamba yatakuwa ya amani na kisheria. Ndio maana nikawatahadharisha viongozi wangu wa Chadema kwa nia njema tu kwamba wawe makini katika kauli zao. Kwa mfano, kama katika maandamano yao ya amani na mada zao wataipa serikali siku 90 au mia kuondoa kero fulani la sivyo watatumia hatua nyingine za kimabavu hiyo itakuwa kinyume cha katiba.
Mbona UVCCM Kilimanjaro wamewapa UVCCM taifa siku saba kuomba radhi na kujiuzuru vinginevyo watajuta ina maana wao hawavunji katiba.
 
Mbona UVCCM Kilimanjaro wamewapa UVCCM taifa siku saba kuomba radhi na kujiuzuru vinginevyo watajuta ina maana wao hawavunji katiba.

Ndugu,

UVCCM sio serikali. Kama Chadema wangesema wanampa mwenyekiti wa CCM siku saba kutekeleza kitu fulani la sivyo ajihuzuru pasingekuwa na tatizo. Tatizo litakija kama mtu atatumia nguvu au vitisho kuiondoa serikali iliwekwa madarakani kwa mujibu wa katiba na sheria. Unapozungumzia kumuondoa Raisi madarakani kwa njia yoyote isiyokuwa ya kisheria ni uhaini na uvunjaji wa katiba. Raisi anaweza kuondolewa madarakani kwa mujibu wa sheria zetu kwa njia tatu tu. Uchaguzi Mkuu, Kura ya kutokuwa na imani inayopigwa na wabunge kwa utaratibu maalumu au kwa sababu za kiafya kwa utaratibu ulioainishwa kisheria.
 
Ndugu,

UVCCM sio serikali. Kama Chadema wangesema wanampa mwenyekiti wa CCM siku saba kutekeleza kitu fulani la sivyo ajihuzuru pasingekuwa na tatizo. Tatizo litakija kama mtu atatumia nguvu au vitisho kuiondoa serikali iliwekwa madarakani kwa mujibu wa katiba na sheria. Unapozungumzia kumuondoa Raisi madarakani kwa njia yoyote isiyokuwa ya kisheria ni uhaini na uvunjaji wa katiba. Raisi anaweza kuondolewa madarakani kwa mujibu wa sheria zetu kwa njia tatu tu. Uchaguzi Mkuu, Kura ya kutokuwa na imani inayopigwa na wabunge kwa utaratibu maalumu au kwa sababu za kiafya kwa utaratibu ulioainishwa kisheria.

Watu wote wangekuwa na mawazo kama yako, basi hadi hii leo nchi zote za Africa zingekuwa zinatawaliwa na wakoloni. Kumbuka wanamapinduzi wote including Mandela waliitwa wahaini kwani walikuwa wanapinga "serikali zilizo halali"

Anyway sifahamu umri wako, lakini labda mfano ulio karibu kama watu wote wangekuwa na mawazo kama yako basi hadi hii leo Hosni Mubaraka (Egypt), Ben Ali (Tunisia) wangekuwa madarakani.
 
Ndugu,

tatizo ni kufanya maandamano ya vurugu na uchochezi. Kama nia ni kufanya maandamano ya amani kuonesha hisia ya ugumu wa maisha hakuna tatizo. Hata hivyo, agenda za maandamano kusomeka hivyo peke yake sio ushahidi kwamba yatakuwa ya amani na kisheria.

Kwa hiyo yakisomeka vipi ndio yatakuwa ya amani na Kisheria?....Naona sasa kwa kweli mmelewa wewe unajua hata sheria inavyolazimishwa kuyakataza maandamano..? Ni lini CDM au chama chochote cha Siasa nchini kishawahi kufanya maandamano ya vurugu na uchochezi? usiongee vitu kama upo mbinguni au kaburini...elezea vitu kwa uhalisia wake..na pia usi-base kwenye tahadhari za ki Abunuwasi...
 
Watu wote wangekuwa na mawazo kama yako, basi hadi hii leo nchi zote za Africa zingekuwa zinatawaliwa na wakoloni. Kumbuka wanamapinduzi wote including Mandela waliitwa wahaini kwani walikuwa wanapinga "serikali zilizo halali"

Anyway sifahamu umri wako, lakini labda mfano ulio karibu kama watu wote wangekuwa na mawazo kama yako basi hadi hii leo Hosni Mubaraka (Egypt), Ben Ali (Tunisia) wangekuwa madarakani.

Mifano unayoitoa ni ya nchi zisizokuwa na mfumo wa demokrasia na utawala wa sheria. Ukoloni ulikuwa ni mfumo wa ukandamizaji, ubaguzi na unyonyaji. Utawala ulikuwa ni wa wageni unaowekwa pia katika mfumo usio wa kidemokrasia. Misiri na Tunisia haina mfumo wa kidemokrasia wa kubadili uongozi kama Tanzania. Ni nchi zilizokuwa na mfumo unaofanana fanana na ufalme au umalikia.

Tanzania tunao mfumo wa kubadili watawala kila baada ya miaka mitano. Uchaguzi Mkuu umepita miezi michache tu iliyopita. Kero za Dowans na maisha magumu wananch waliambiwa sana katika kampeni za siasa. Baada ya kusikiliza kwa makini nyimbo kutoka vyama vyote vya siasa ndio wameamua hivyo. Sasa kama tumeshindwa kuzitumia vizuri nyimbo za Dowans na maisha magumu kuing'oa serikali iliyopo kwa njia ya kura, tunataka kuzitumia kuwang'oa kwa njia ya nguvu. Sasa kama hao asilimia 30 ya wapiga kura waliipigia Chadema katika Uchaguzi Mkuu uliopita watakuwa na uwezo wa kuitisha maandamano na kuishinikiza serikali iliyochaguliwa na asilimia 70 iachie madaraka demokrasia ya uchaguzi itakuwa na maana yoyote?

Hivi kama asilimia kumi ya watanzania walioshindwa katika Uchaguzi Mkuu wakiamua kuandamana kuishinikiza serikali itoke madarakani kutakalika kweli? Je nani atakaekuwa analinda asilimia 70 ya watanzania wanaoiunga mkono serikali? Vigezo gani vitatumika kujua kama hawa watu wanaoandama kushinikiza serikali iondoke madarakani wanawakilisha mtizamo wa majoroty ya watanzania? Hivi leo tukipiga kura za watanzania wote tuna uhakika gani kama tutapata hata asilimia kumi ya watanzania wanaounga mkono maandamano yoyote yanayokusudia kutumia njia ya mabavu kuiondoa serikali madarakani? Mimi naona namna pekee ya kujua kama serikali iliyopo inatakiwa au la ni kupitia kura za wananchi.

Kama kuna lolote la dhalura linajitokeza kabla ya miaka mitano sheria imeweka njia nyingine ya demokrasia wakilishi ambayo kupitia kwake Raisi au Waziri Mkuu anaweza kuondolewa madarakani. Wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi wamepewa nguvu hizo kwa utaratibu maalumu kama kiongozi wa nchi anakosa maadili ya kuongoza nchi au kumuondoa Wziri Mkuu na hatimaye Cabinet yake kama hana uwezo wa kuongoza nchi.

Umeniuliza umri, mimi nakimbilia miaka 34.
 
Kwa hiyo yakisomeka vipi ndio yatakuwa ya amani na Kisheria?....Naona sasa kwa kweli mmelewa wewe unajua hata sheria inavyolazimishwa kuyakataza maandamano..? Ni lini CDM au chama chochote cha Siasa nchini kishawahi kufanya maandamano ya vurugu na uchochezi? usiongee vitu kama upo mbinguni au kaburini...elezea vitu kwa uhalisia wake..na pia usi-base kwenye tahadhari za ki Abunuwasi...

Ndugu yangu ungesoma post yangu yote. Mimi sijasema kama Maandamano kusudiwa yapo au hayapo. Nilichotahadharisha ni kwamba maandamano hayo yawe ya amani na ya kuzingatia sheria. Kama maandamano yatafanyika na kuvunja sheria nitasema. Hapo sioni tatizo liko wapi mpaka hapo?
 
CHADEMA HII HII AU KILE Chama Chetu Malumbano......?

Mimi naweza kuwa tofauti sana na unavyoweza kuwa unanidhania. Mimi kwa uhakika naheshimu vyama vyote vya siasa japo sina chama. Najua kwa mfumo huu wa demokrasia chama chochote cha siasa kinaweza siku yoyote kuchukua dola. Kwa hiyo, kiongozi wa chama chochote cha siasa, kwa mtizamo wangu (I could be terribly wrong) ni kiongozi wangu. Ndio maana nilisema "viongozi wangu wa Chadema".
 
Natumaini sheikh mkuu anatambua juu ya maisha magumu tuliyonayo..kama maisha yataendelea kuwa magumu amani lazima itapotea tu.mbona agenda ipo wazi hapo inaonyesha uvunjifu wa amani hapo?
 
Mimi naweza kuwa tofauti sana na unavyoweza kuwa unanidhania. Mimi kwa uhakika naheshimu vyama vyote vya siasa japo sina chama. Najua kwa mfumo huu wa demokrasia chama chochote cha siasa kinaweza siku yoyote kuchukua dola. Kwa hiyo, kiongozi wa chama chochote cha siasa, kwa mtizamo wangu (I could be terribly wrong) ni kiongozi wangu. Ndio maana nilisema "viongozi wangu wa Chadema".
Kama mmoja ana mlengo wa kushoto mwingine wa kulia wewe utakuwa upande gani usituletee mazungumzo ya kwenye gahawa, nafikiri ulivyoandika kwenye red uko sahihi kabisa.
 
Kama mmoja ana mlengo wa kushoto mwingine wa kulia wewe utakuwa upande gani usituletee mazungumzo ya kwenye gahawa, nafikiri ulivyoandika kwenye red uko sahihi kabisa.

Pia nimepokea hayo kama mawazo na maoni yako japo sijapendezwa na kuyahukumu maneno yangu kama ya kwenye kahawa. Waungwana hujadiliana kwa hoja badala ya personality. Tukianza kushindana kwa kupeana majina hatuwezi kufika popote. Kukosoa na kukosoana ndio sehemu ya mjadala ndio maana nikaandika uliyoyakoleza kwa wino mwekundu.

Niamanivyo mimi kiongozi ni yule anayechaguliwa na wengi hata awe mlengo wa kushoto au kulia. Kesho watanzania wakiamua kumchagua Mh. Mbatia au Mh. Mbowe kuwa Raisi nitamheshimu kwa kiwango kile kile kama ninavyomheshimu Mh. Kkwete hadi amalize muda wake. Kwani kwa kumheshimu na kumtii yeye nitakuwa ninawaheshimu na kuwatii waliomchagua. Hii ni imani yangu na msimamo wangu. Japo kama kuwa una makosa nitaendelea kuwa nao
 
Pia nimepokea hayo kama mawazo na maoni yako japo sijapendezwa na kuyahukumu maneno yangu kama ya kwenye kahawa. Waungwana hujadiliana kwa hoja badala ya personality. Tukianza kushindana kwa kupeana majina hatuwezi kufika popote. Kukosoa na kukosoana ndio sehemu ya mjadala ndio maana nikaandika uliyoyakoleza kwa wino mwekundu.

Niamanivyo mimi kiongozi ni yule anayechaguliwa na wengi hata awe mlengo wa kushoto au kulia. Kesho watanzania wakiamua kumchagua Mh. Mbatia au Mh. Mbowe kuwa Raisi nitamheshimu kwa kiwango kile kile kama ninavyomheshimu Mh. Kkwete hadi amalize muda wake. Kwani kwa kumheshimu na kumtii yeye nitakuwa ninawaheshimu na kuwatii waliomchagua. Hii ni imani yangu na msimamo wangu. Japo kama kuwa una makosa nitaendelea kuwa nao
Endelea na imani yako ya kufyonza kama dodoki yeyote kwako twende tu bila hata kujiuliza, hauko tofauti na wanawake wa kabila fulani ambao hawana tabia ya kukataa almradi mwanamme katangulia FIFO.
 
Endelea na imani yako ya kufyonza kama dodoki yeyote kwako twende tu bila hata kujiuliza, hauko tofauti na wanawake wa kabila fulani ambao hawana tabia ya kukataa almradi mwanamme katangulia FIFO.

Nashukuru kaka. Katika forum kubwa kama hii yenye watu wa upeo tofauti sio lazima kila mtu aweze kukuelewa unachosema na pengine mtu anaweza kukuelewa lakini akaamua kupotosha ulichosema kwa maslahi ya kupata sifa kwa watu kwamba anajua sana kusema. Posts zangu zote ziko hewani wanajamii forum watasoma na kuamua nani yuko sawa na nani analazimisha kuwa sawa. Kwa mjadala huu na kwa faida yetu na ya wasomaji wengi naomba tuishie hapa nimekubali mshindi wewe kaka. Vinginevyo tutaanza kubishana kwa kupeana majina yasiyopendeza ili mradi kila mtu afurahi kwa kutonesha hisia za mwenzake. Ningemshauri mhariri (kama yupo) aanzishe forum maalumu ya watu vipaji vya matusi ili sisi tusio na ubavu katika fani hiyo tujitowe.
 
Kama kuna lolote la dhalura linajitokeza kabla ya miaka mitano sheria imeweka njia nyingine ya demokrasia wakilishi ambayo kupitia kwake Raisi au Waziri Mkuu anaweza kuondolewa madarakani. Wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi wamepewa nguvu hizo kwa utaratibu maalumu kama kiongozi wa nchi anakosa maadili ya kuongoza nchi au kumuondoa Wziri Mkuu na hatimaye Cabinet yake kama hana uwezo wa kuongoza nchi.

Umeniuliza umri, mimi nakimbilia miaka 34.[/QUOTE]

To George Jinasa kwa umri ulionao nilitegemea uwe na busara kidogo japo bado una-qualify kuwa UVCCM. Pia umenifurahisha maana unaongonea kama Membe siku ile alipoongea ITV

Mimi huwa napenda kuandika kwa mifano. Tanzania na Ivory Coast ninaweza kusema zina mfumo unaofana kama ulivyoeleza hapo juu. Kubadilisha viongozi kila baada ya miaka ya mitano through a ballot box, ambao wewe umeiita "demokrasia".

The catch 22 hapa ni je kweli demokrasia hiyo inatendeka? Tofauti ya Tanzania na Ivory Coast ni kwamba.

Tume ya uchaguzi ya Ivory Coast ilikuwa na brave enough ya kumtangaza mshindi aliyeshinda uchaguzi, lakini incumbet president Gbabo amekataa kutoka madarakani.

Tume ya uchaguzi ya Tanzania haikuwa na gut ya kumtangaza mshindi, hence ikamtangaza ALIYESHINDWA kuwa ndiye MSHINDI. Sasa hiyo demokrasia ya kubadilisha viongozi iko wapi wakati NEC ndiyo iliyotuchagulia kiongozi.

Kwa umri wako huwezi kufahamu lakini kabla ya mapinduzi ya ZNZ, kila ulipfanyika uchaguzi ASP ilikuwa ikishindwa kwenye ballot box, kwasababu ya sheria mbovu za uchaguzi zilizokuwepo.

Sasa kama hayati Abed Amani Karume angekuwa na AKILI kama zako basi hadi hii leo ZNZ ingekuwa chini ya utawala wa sultan.

Hayo yote uliyoeleza yanawezekana tu pale ambapo kuna free and fairly election and more important TUME YA UCHAGUZI IKO HURU vitu ambavyo Tanzania hatuna. Mwisho usivae miwani ya mbao au kujitia upofu kwamba Mubara na Ben Ali walikuwa hawafanyi huo unaoita uchaguzi kama Tanzania?!
 
Kama kuna lolote la dhalura linajitokeza kabla ya miaka mitano sheria imeweka njia nyingine ya demokrasia wakilishi ambayo kupitia kwake Raisi au Waziri Mkuu anaweza kuondolewa madarakani. Wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi wamepewa nguvu hizo kwa utaratibu maalumu kama kiongozi wa nchi anakosa maadili ya kuongoza nchi au kumuondoa Wziri Mkuu na hatimaye Cabinet yake kama hana uwezo wa kuongoza nchi.

Umeniuliza umri, mimi nakimbilia miaka 34.

To George Jinasa kwa umri ulionao nilitegemea uwe na busara kidogo japo bado una-qualify kuwa UVCCM. Pia umenifurahisha maana unaongonea kama Membe siku ile alipoongea ITV




Mimi huwa napenda kuandika kwa mifano. Tanzania na Ivory Coast ninaweza kusema zina mfumo unaofana kama ulivyoeleza hapo juu. Kubadilisha viongozi kila baada ya miaka ya mitano through a ballot box, ambao wewe umeiita "demokrasia".

The catch 22 hapa ni je kweli demokrasia hiyo inatendeka? Tofauti ya Tanzania na Ivory Coast ni kwamba.

Tume ya uchaguzi ya Ivory Coast ilikuwa na brave enough ya kumtangaza mshindi aliyeshinda uchaguzi, lakini incumbet president Gbabo amekataa kutoka madarakani.

Tume ya uchaguzi ya Tanzania haikuwa na gut ya kumtangaza mshindi, hence ikamtangaza ALIYESHINDWA kuwa ndiye MSHINDI. Sasa hiyo demokrasia ya kubadilisha viongozi iko wapi wakati NEC ndiyo iliyotuchagulia kiongozi.

Kwa umri wako huwezi kufahamu lakini kabla ya mapinduzi ya ZNZ, kila ulipfanyika uchaguzi ASP ilikuwa ikishindwa kwenye ballot box, kwasababu ya sheria mbovu za uchaguzi zilizokuwepo.

Sasa kama hayati Abed Amani Karume angekuwa na AKILI kama zako basi hadi hii leo ZNZ ingekuwa chini ya utawala wa sultan.

Hayo yote uliyoeleza yanawezekana tu pale ambapo kuna free and fairly election and more important TUME YA UCHAGUZI IKO HURU vitu ambavyo Tanzania hatuna. Mwisho usivae miwani ya mbao au kujitia upofu kwamba Mubara na Ben Ali walikuwa hawafanyi huo unaoita uchaguzi kama Tanzania?![/QUOTE]

Nashukuru kwamba tumerudi katika mstari na pia sioni tatizo kama nitakuwa nimeonga kama Mh. Membe ili mradi tu alichokiongea nakubaliana naye.

Kwamba kuna matatizo katika Sheria ya Uchaguzi, mimi nakubaliana nawe kwa sehemu fulani. Naongezea kusema kwamba matatizo katika sheria ya uchaguzi yamekuwepo toka tulipoingia mfumo wa vyama vingi na baadhi yameshapunguzwa kutokana na marekebisho mbalimbali. Licha ya mapungufu yote, sikubaliani nawe kwamba aliyetangazwa mshindi katika Uraisi hakuwa mshindi. Hata kama tukitumia mantiki ya kawaida tu haiwezekani huyu aliyeshindwa kwa asilimia zaidi ya 60 katika uchaguzi wa wabunge na zaidi ya asilimia 70 kwenye cchaguzi wa serikali za mitaa akalalamikia matokea ya uraisi tu huku ya ubunge na serikali za mitaa yakawa sawa.

Nikirudi katika matatizo ya sheria za uchaguzi, utakubaliana nami kwamba toka kipindi cha kampeni hata baada ya matokeo ya uchaguzi kumekuwa na mijadala inayoendelea ya kutaka kubadilisha sheria zetu za uchaguzi na katiba kwa ujumla ili tuondoe dosari zilizopo. Utakumbuka kwamba kwa kipindi kirefu katika maisha ya nchi tumekuwa na mfumo wa chama kimoja. Katiba na sheria yetu iliathirika vya kutosha na mfumo huo kiasi kwamba hata tulipoingia mfumo wa vyama vingi mwaka 1992 hatukuweza kuondoa athari hizo. Yamefanyika marekebisho mbali mbali ya sheria na katiba lakini tatizo liko pale pale. Sasa baada ya shinikizo kubwa la wanasiasa na wanaharakati wa haki za binaadamu, serikali imeafiki iwepo katiba mpya itakayousuka mfumo wetu wa sheria na katiba upya ili uendane na wakati tulio nao. Nilitegemea kwamba tungetumia nafasi hiyo ili kutoa dosari katika mfumo wetu wa sheria na katiba. Kama serikali wangekuwa hawakubali uwepo wa dosari katika mfumo wetu na hawako tayari kufanya mabadiliko labda tungesema hamna alternative.

Mfano wa Zanzibar nisingependa kuuzungumzia sana kutokana na hali ya utulivu iliyopo Zanzibar sasa. Vurugu zote ambazo zimekuwepo Zanzibar kwa muda mrefu chimbuko lake ni histroria ya Zanzibar pamoja na mapinduzi. Utakumbuka kwamba muda mfupi kabla na baada ya ulioitwa uhuru wa Zanzibar mwaka 1963 (kama sikosei) vyama vya siasa Zanzibar viliundwa katika msingi wa asili. Wazanzibar wenye asili ya kiarabu kwa sehemu kubwa walikuwa na chama kimoja tu. Kwa upande mwingine Wazanzibar wenye asili isiyo hiyo walikuwa na vyama tofauti vikiegemea katika maslahi mengine ya kijamii. Haukupita muda mrefu baadhi ya Wazanzibar bila kujali asili yao waliona uhuru waliopewa na Waingereza ulikuwa wa bandia wenye lengo la kuwafanya Waingereza kuendelea kutawala kupitia kwa makundi walioyataka.
 
Jamani kulikuwa na Ratiba ya kufanya maandamano machi 13, 2011 mjini kigoma naambiwa Dk na viongozi wote walifika lakini sijapata update hapa kwenye Forum, Je maandamano yalifanyika au yaliakhirishwa mpaka lakini na kwa nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom