George Jinasa
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 399
- 52
Ndugu,
Hebu soma agenda za mkutano huo kabla ya kulaumu na kuelekeza....
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza kufanya maandamano makubwa ya amani mkoani hapa mwezi ujao kupinga hali ngumu ya maisha kutokana na mfumuko wa bei na malipo ya fidia ya Sh. bilioni 94 kwa kampuni ya kufua umeme ya Dowans Tanzania Limited.
Ndugu,
Naona hukusoma vizuri post yangu. Mimi sikulaumu Chadema wala sikuzungumzia maandamano yoyote maalumu. Ndio maana nilizungumzia kuwepo au kutokuwepo kwa maandamano. Nilichosema ni kwamba kufanya maandamano sio tatizo bali tatizo ni kufanya maandamano ya vurugu na uchochezi. Kama nia ni kufanya maandamano ya amani kuonesha hisia ya ugumu wa maisha hakuna tatizo. Hata hivyo, agenda za maandamano kusomeka hivyo peke yake sio ushahidi kwamba yatakuwa ya amani na kisheria. Ndio maana nikawatahadharisha viongozi wangu wa Chadema kwa nia njema tu kwamba wawe makini katika kauli zao. Kwa mfano, kama katika maandamano yao ya amani na mada zao wataipa serikali siku 90 au mia kuondoa kero fulani la sivyo watatumia hatua nyingine za kimabavu hiyo itakuwa kinyume cha katiba.