CHADEMA yalaani vikali CCM kutumia magari ya serikali

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimelaani tabia ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutumia magari ya serikali kwa shughuli za chama hasa katika sherehe mbalimbali za chama hicho.
Akihutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kata ya Kihesa mkoani hapa, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, alisema CCM ilitumia magari ya serikali wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 35 ya kuzaliwa kwa chama hicho, jambo ambalo ni kinyume cha sheria.
Alisema wabunge na viongozi wa CHADEMA hawatakubali kushuhudia mali za serikali zikitumiwa na CCM katika shughuli za kisiasa na kwamba atafuatilia kwa makini kiasi cha fedha zilizotumika kuyahudumia magari hayo.
“Nitaongoza mapambano na kuyapiga mawe magari ya serikali, halmashauri au ya mahakama yatakayoonekana yakifanya kazi za CCM halafu watuambie yalienda kufanya nini. Mimi nitaongoza mapambano hayo kwa sababu yale magari ni ya serikali, CCM inunue magari yao,’’ alisema Msigwa.
Awali mbunge huyo alilalamikiwa na wananchi wa Sentema juu ya baadhi ya viongozi wa kata hiyo kuwachangisha wananchi michango mbalimbali bila kupata matumizi ya fedha walizozichanga, hali ambayo inawakatisha tamaa kuendelea kuchangia.
Katika mkutano huo, mbunge huyo aliwapokea wanachama wapya 78 na kuzindua tawi jipya katika Kata ya Kihesa.

Source:Tanzania Daima
 
Mh taratibu, tusipige mawe tutumie njia nyingine mbadala, tupange magogo barabarani ili yasitembee, najua inauma sana kuona magari ya Serikali yakitumika kinyume na matarajio ya watz, badala ya kuwahudumia wananchi ambao ndio walipa kodi yanatumika kwa shughuli za chama
 
hizi silaha za jadi ni za muhimu kutumia, ni wazo zuri, tuliboreshe, naamini litailazimisha serikali kubana matumizi.
 
siungi mkono hoja ya kuyapiga mawe mimi nashauri tuunde kikosi kazi cha kuwanyanganya madereva funguo.
 
Ina maana kaishiwa hoja/mbinu ingine ya kutumia kudhibiti hilo hadi hilo la kupiga mawe? That wont be proper!
 
ccm kimeshapoteza mvuto kwa wananchi wa kawaida -- wana kazi kubwa mno kurudisha uaminifu sababu kuu zikiwa ni uongo, wizi (wa kura na mali za umma) kutisha tisha wananchi kwa kutumia vyombo vya dola, rushwa iliyokomaa ndani ya mfumo wa sekta ya umma, kulindana - haya yote ni kansa liyofika level hata mionzi haifanyi kazi ku-heal donda

CDM waanze kujiandaa kuunda dola maana wananchi wenye mamlaka na nchi hii tayari wameshakata kauli 2015 lazima changes zitokee katika historia ya nchi hii.
 
Back
Top Bottom