Mshume Kiyate
JF-Expert Member
- Feb 27, 2011
- 6,766
- 894
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetoa tamko kikitaka serikali kuitisha uchaguzi wa Meya wa Manispaa ya Arusha ndani ya siku 21, vinginevyo nguvu ya umma itatumika. Tamko hilo lilitolewa na Katibu Mkuu wa Chadema Dk Willibrod Slaa, mjini Kigoma akihutubia mkutano wa hadhara Uwanja wa Mwanga Center.
Dk Slaa alisema uchaguzi wa kumpata Meya wa Manispaa ya Arusha, ulifanyika mwaka ulikuwa mbovu na uliokiuka taratibu za sheria kwa kaimu mkurugenzi kuvurunda kwa maslahi ya CCM hivyo kusababisha wananchi kuandamana na watu watatu kuuawa kwa risasi na polisi.
"Tunatoa siku 21 kwa serikali kuhakikisha inaitisha uchaguzi wa Meya Manispaa ya Arusha, Tunasema Rais na Waziri Mkuu watumie busura zao ndani ya siku 21 kulipatia ufumbuzi suala hili, vinginevyo nguvu ya Umma itafanya kazi yake" alisisitiza Dk Slaa.
Mwananchi Machi 23, 2011
Dk Slaa alisema uchaguzi wa kumpata Meya wa Manispaa ya Arusha, ulifanyika mwaka ulikuwa mbovu na uliokiuka taratibu za sheria kwa kaimu mkurugenzi kuvurunda kwa maslahi ya CCM hivyo kusababisha wananchi kuandamana na watu watatu kuuawa kwa risasi na polisi.
"Tunatoa siku 21 kwa serikali kuhakikisha inaitisha uchaguzi wa Meya Manispaa ya Arusha, Tunasema Rais na Waziri Mkuu watumie busura zao ndani ya siku 21 kulipatia ufumbuzi suala hili, vinginevyo nguvu ya Umma itafanya kazi yake" alisisitiza Dk Slaa.
Mwananchi Machi 23, 2011