Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,436
- 5,234
Kaimu Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara, Amani Golugwa, akiambatana na mawakili wa chama hicho, wamewasilisha maombi Mahakama Kuu Kanda ya Manyara Agosti 20, 2025, wakipinga maelekezo ya barua ya Msajili wa Vyama vya Siasa kuhusu kutoutambua uongozi wa chama hicho.
Barua ya Msajili imeelezwa kutotambua uteuzi wa Katibu Mkuu, Manaibu Katibu Bara na Zanzibar pamoja na wajumbe wa Kamati Kuu waliopitishwa na Baraza Kuu la CHADEMA Januari 22, 2025, kwa hoja kwamba uteuzi huo haukuwa na akidi ya kikatiba, kufuatia malalamiko yaliyowasilishwa na Lembrus Mchome, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Mwanga.
Akizungumza na wanahabari nje ya Mahakama, Golugwa amesema msingi wa shauri hilo ni kupinga maelekezo ya Msajili na kuiomba Mahakama itoe zuio la kutotekelezwa kwa barua hiyo.
Mahakama imetoa maelekezo kuwa uamuzi wa awali kuhusu maombi hayo utatolewa Agosti 28, 2025 saa 8 mchana.
Ikumbukwe kuwa vuguvugu la shauri hili linahusishwa na kesi iliyofunguliwa na Mchome mnamo Aprili 2025, akipinga mchakato wa uchaguzi wa Kamati Kuu ya CHADEMA akidai haukufuata akidi ya kikatiba.
Barua ya Msajili imeelezwa kutotambua uteuzi wa Katibu Mkuu, Manaibu Katibu Bara na Zanzibar pamoja na wajumbe wa Kamati Kuu waliopitishwa na Baraza Kuu la CHADEMA Januari 22, 2025, kwa hoja kwamba uteuzi huo haukuwa na akidi ya kikatiba, kufuatia malalamiko yaliyowasilishwa na Lembrus Mchome, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Mwanga.
Akizungumza na wanahabari nje ya Mahakama, Golugwa amesema msingi wa shauri hilo ni kupinga maelekezo ya Msajili na kuiomba Mahakama itoe zuio la kutotekelezwa kwa barua hiyo.
Mahakama imetoa maelekezo kuwa uamuzi wa awali kuhusu maombi hayo utatolewa Agosti 28, 2025 saa 8 mchana.
Ikumbukwe kuwa vuguvugu la shauri hili linahusishwa na kesi iliyofunguliwa na Mchome mnamo Aprili 2025, akipinga mchakato wa uchaguzi wa Kamati Kuu ya CHADEMA akidai haukufuata akidi ya kikatiba.