CHADEMA waoneshe dhamira ya kweli kupinga 'udikteta', watangaze kujitenga na Serikali Uingereza na Marekani

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Feb 17, 2016
17,506
15,997
Ndugu zangu,

kabla ya kujadili turejee uamuzi wa Serikali ta Tanzania kuzuia Bunge kuoneshwa ''live''. Hapa ndipo ''kiki'' zilianza,ukuta ukazaliwa na harakati ''mfu'' ikiwemo kuandika barua lukuki kwa umoja wa ulaya na Marekani.

Kama kweli Chadema ni chama cha ''kidemokrasia'' kiutangazie umma wa Tanzania kupinga udikteta wa Marekani na Uingereza dhidi ya bunge na wabunge.

Nianze na Marekani, mwezi uliopita tumemshuhudia Trump akiwabagua wabunge wenye asili ya kiafrika na kilatino huku ukizingatia kuwa yeye hakushinda uraisi kwa kura nyingi bali kwa kupora ushindi kupitia 'NEC' yao inayoundwa na genge linalojiita ''electoral college''.

Uingereza, hawa amiri jeshi mkuu ni malkia/mfalme ambaye hapigiwi kura na wabunge wote huapa kiapo cha kutii maamuzi yake bila kuwa na fursa ya kupinga mahakamani kwani yeye ndiye ''katiba''. Zaidi ameidhinisha amri ambayo itawakosesha wabunge wa uingereza haki ya kujadili mustakabali wa taifa lao kuhusu kujitoa umoja wa ulaya. Chadema kumbukeni mliandika barua kuwaomba hawa wazungu wawasaidi ili Bunge liwe ''live'' sasa angalia wao wanafanya nini?

Kibaya zaidi, Chama cha Conservative ambao chama tawala ni chama rafiki yenu mara kadhaa mmetamba kushirikiana nao.Kiongozi wa Conservative ambaye ni Waziri mkuu wa UK kaandika barua kumshawishi malkia ambaye yupo juu ya katiba na bunge ''kuwapiga pin'' wabunge.

Mkiendelea kuandika barua kuomba msaada wa ''kidemokrasia'' kutoka uingereza na Amerika mnapata laana.Huwezi kuomba thawabu toka kwa shetani labda uwe ''kashetani''.

Nimalize tu kwa kusema 'makamanda'' msio na madhara amkeni kumekuchaa.
 
Uongozi wa Marekani na Uingereza waweza kutoa maoni au hisia zao lakini hawawezi kukiuka katiba zao wakabaki madarakani.Ndio maana Trump yapo alitaka kujenga ukuta lakini wabunge wa senate walipomukataria kuidhinisha fedha za kufanya hivyo ilibidi arudi nyuma.Hata huyo Boris Johnson wa Uingereza hawezi kuforce Brexit bila kuungwa mkono na wabunge wa 10 Down street.Na sisi Tanzania tujifunze uzuri wa demokrasia badala kuwa overwhelmed na utawala wa autocratic system
 
Uongozi wa Marekani na Uingereza waweza kutoa maoni au hisia zao lakini hawawezi kukiuka katiba zao wakabaki madarakani.Ndio maana Trump yapo alitaka kujenga ukuta lakini wabunge wa senate walipomukataria kuidhinisha fedha za kufanya hivyo ilibidi arudi nyuma.Hata huyo Boris Johnson wa Uingereza hawezi kuforce Brexit bila kuungwa mkono na wabunge wa 10 Down street.Na sisi Tanzania tujifunze uzuri wa demokrasia badala kuwa overwhelmed na utawala wa autocratic system

..Na Boris anapingwa hata na wabunge wa chama chake cha Conservative.

..Na wabunge hao hawaitwi wasaliti na kuwindwa na kushambuliwa kama wanyama wa porini.

..Zaidi, Spika wa Bunge la Uingereza ametoa msimamo tofauti na wa Waziri Mkuu Boris.
 
Mkuu naona Daniel Chongo kaula amekuwa kimya, Ritz
Mkuu JokaKuu heshima kwako! Unajua mtu ukikutana na hoja dhaifu kama ya mtoa mada kisha ukapata za chinichini kuwa mtoa mada ni mtu ana hold post ya juu ndani ya mamlaka unapata taabu sana!
Swali unalojiuliza, jee huyo mteuzi anajuwa analolifanya au ana abuse power aliyonayo kwa kuweka hata michepuko bila kujali uwezo?
Jee haya si ndio matokeo kwa nini nchi ime stuck na haisongi mbele?
Maana kwa fikra kama hizo hata ukimpa kijiji hawezi kukiongoza sembuse wizara!
 
Ndugu zangu,

kabla ya kujadili turejee uamuzi wa Serikali ta Tanzania kuzuia Bunge kuoneshwa ''live''. Hapa ndipo ''kiki'' zilianza,ukuta ukazaliwa na harakati ''mfu'' ikiwemo kuandika barua lukuki kwa umoja wa ulaya na Marekani.

Kama kweli Chadema ni chama cha ''kidemokrasia'' kiutangazie umma wa Tanzania kupinga udikteta wa Marekani na Uingereza dhidi ya bunge na wabunge.

Nianze na Marekani, mwezi uliopita tumemshuhudia Trump akiwabagua wabunge wenye asili ya kiafrika na kilatino huku ukizingatia kuwa yeye hakushinda uraisi kwa kura nyingi bali kwa kupora ushindi kupitia 'NEC' yao inayoundwa na genge linalojiita ''electoral college''.

Uingereza, hawa amiri jeshi mkuu ni malkia/mfalme ambaye hapigiwi kura na wabunge wote huapa kiapo cha kutii maamuzi yake bila kuwa na fursa ya kupinga mahakamani kwani yeye ndiye ''katiba''. Zaidi ameidhinisha amri ambayo itawakosesha wabunge wa uingereza haki ya kujadili mustakabali wa taifa lao kuhusu kujitoa umoja wa ulaya. Chadema kumbukeni mliandika barua kuwaomba hawa wazungu wawasaidi ili Bunge liwe ''live'' sasa angalia wao wanafanya nini?

Kibaya zaidi, Chama cha Conservative ambao chama tawala ni chama rafiki yenu mara kadhaa mmetamba kushirikiana nao.Kiongozi wa Conservative ambaye ni Waziri mkuu wa UK kaandika barua kumshawishi malkia ambaye yupo juu ya katiba na bunge ''kuwapiga pin'' wabunge.

Mkiendelea kuandika barua kuomba msaada wa ''kidemokrasia'' kutoka uingereza na Amerika mnapata laana.Huwezi kuomba thawabu toka kwa shetani labda uwe ''kashetani''.

Nimalize tu kwa kusema 'makamanda'' msio na madhara amkeni kumekuchaa.
Nyundo makini haiwezi jibiwa kifasaha,ukweli huu tegemea kusindikizwa na matusi,ndio uwezo wao wa kufikiri ulipogotea
 
Kwamb huyu mleta mada hana hata uwezo wa kutofautishi nini maana ya "ceremonial leader" hahaha sijui alisoma wapi huyu
 
Back
Top Bottom