Kulwa Jilala
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 3,510
- 7,755
Tokea Freeman Mbowe alambe asali viongozi wa Chadema wanakosoa serikali ya Rais Samia kwa umakini mkubwa ili wasimkwaze akamnyima asali mwenyekiti wao. Hata ripoti ya CAG ya mwaka 2023 wanalazimika kumkosoa na kumtajataja Magufuli ambaye hayupo madarakani na duniani kwa miaka 2 iliyopita.
Enzi ya Hayati Rais Magufuli TISS( usalama wa taifa) walisimamiwa vizuri na walifanya kazi yao kwelikweli kuzuia hujuma zote kwa taifa hadi nchi ikaingia uchumi wa kati miaka 5 mapema zaidi tofauti na ilivyokuwa imetabiriwa na mabeberu kwamba Tanzania itachukua miaka 10 kuingia uchumi wa kati!.
Tanzania iligeuka si salama kwa wahujumu uchumi wote ikiwemo Tundu Lissu aliyekuwa anatuma meseji kwa Acacia wampe nyaraka ili aone jinsi ya kuwasaidia ili Tanzania ishitakiwe MIGA, Akina Erick Kabendera hawataisahau TISS ya awamu ya tano kwani ilijua kuwafuatilia na kuwatia adabu mawakala wa mabeberu hapa nchini, hata ilipoingia corona Freeman Mbowe alijipapatua kwa kulazimisha iwepo lockdown Tanzania lakini alikiona cha moto kutoka kwa usalama wa taifa kwani walimwanika hadharani namna anavyosaliti taifa.
Enzi ya Hayati Rais Magufuli TISS( usalama wa taifa) walisimamiwa vizuri na walifanya kazi yao kwelikweli kuzuia hujuma zote kwa taifa hadi nchi ikaingia uchumi wa kati miaka 5 mapema zaidi tofauti na ilivyokuwa imetabiriwa na mabeberu kwamba Tanzania itachukua miaka 10 kuingia uchumi wa kati!.
Tanzania iligeuka si salama kwa wahujumu uchumi wote ikiwemo Tundu Lissu aliyekuwa anatuma meseji kwa Acacia wampe nyaraka ili aone jinsi ya kuwasaidia ili Tanzania ishitakiwe MIGA, Akina Erick Kabendera hawataisahau TISS ya awamu ya tano kwani ilijua kuwafuatilia na kuwatia adabu mawakala wa mabeberu hapa nchini, hata ilipoingia corona Freeman Mbowe alijipapatua kwa kulazimisha iwepo lockdown Tanzania lakini alikiona cha moto kutoka kwa usalama wa taifa kwani walimwanika hadharani namna anavyosaliti taifa.