pangalashaba
JF-Expert Member
- Jan 10, 2011
- 1,325
- 1,615
Me nashangaa sana huu utamaduni wa watanzania kutokupenda kukosolewa au kuambiwa ukweli pale inapobidi. Naiona hii hali hata humu ndani JF Kila mtu akipost mada ya kuikosoa CHADEMA basi atatukanwa na kuitwa mtoto wa mafisadi.
People inabidi mjifunze kudigest different ideas. Inabidi tujenge utamaduni wa kukubali kutokubaliana. JUST BECAUSE NAIKOSOA CHADEMA IT DOESNT MEAN MIMI NI CCM, I CAN BE INDEPENDENT.
Katika chaguzi nyingi duniani wanaoamua mshindi ni watu kama mimi because sina chama so i can vote to chama chochote ambacho kina sera nzuri. Tofauti na watu ambao wenyewe ni wapenzi wa vyama, hata vyama vyao vikifanya madudu wanavipigia kura tu.
MAPENZI HULETA UPOFU, I dont support CCM 4 any mean kwani najua 80% ya matatizo yanayolikabili taifa letu yamesababishwa nao, na kama wangekuwa na gut wangeweza kuyamaliza yote.
The same time siwez tu kuisuport CHADEMA sababu tu ni chama cha upinzani kikuu wakati kuna madudu kibao nawaona wakifanya.
CHADEMA INABIDI WABADILIKE, UMAARUFU WAO UMEKUJA GHAFLA MNO AND THATS BAD, inabidi wafanye reform kubwa sana katika utawala na kurecruit watu.
ASIKWAMBIE MTU VINGINE, UKWELI NI KUWA NGUVU YA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA INAANZIA KWENYE MATAWI YA NYUMBA KUMI KUMI. HUKO NDIO KWA KUINVEST NA KUMWAGA MAPESA, NA SIO MAANDAMANO NA MIKUTANO ISIYO NA TIJA.
CHADEMA wafukuzeni CCM kimya kimya bila makelele kwa kukijenga chama katika nyumba kumi kumi.
Msinitukane wazee ni maoni tu.
Tuliambiwa tusiwachague wanaonekana wakati wa uchaguzi tuu. Tukasema sawa tukawapa CCM japo tunajua "hatukuwapa" bali walijipa kura zetu wenyewe...
Nimekaa kidogo kila nikisafiri kila mkoa sasa ni CHADEMA CHADEMA CHADEMA.... Yaani kama unapenda CCM waweza ugua ule ugonjwa wa ukichakaa kama malaria sugu.
Sasa nimeshangaaa CCM wamekiri kuwa CHADEMA si chama cha msimu na wanaomba jamii iwaonee huruma wao kwa kupiga mbiu CHADEMA ni cha kidini(waislamu na wakristo) na ukabila(makabila kama 120 hivi). Maana wakati tunaenda kupiga kura waliochagua CHADEMA kwa wingi nimesikia ni wasukuma kule Shinyanga na Mwanza. CHADEMA chama cha kikabila cha wasukuma. Baadae nikaambiwa na Mbeya nikagundua kumbe hiki ni cha kikabila wasafwa, wanyakyusa na wengine.
Nikaendelea na safari yangu kama kawaida nchi nzima. Kufika kibaha nikaambiwa Mgombea wa CHADEMA alishinda akachakachuliwa kwa kuwa mgombea wa CCM Silvestry Koka pale mjini ni mkristo halafu Habibu wa CHADEMA ni muislamu. Wakadai kuwa "eti" pale kibaha kuna waislamu wengi kwa hiyo walimchagua Habibu kwa kuwa ni muislamu. Nikagundua kumbe CCM wanaposema CHADEMA cha kidini kumbe kweli maana huyu mgombea muislamu alipata kwa sababu hiyo.
Cossortium de facto le pressee'..... Hoja haiwezi kuwa hoja mpaka ujiridhishe kwanza
Nawasilisha.
watu wengi tu walishasema kuhusu chadema kujibadilisha kisera, kimtazamo na ki-organisation, naona ujumbe unazidi kuwaingia , tusubiri wamalize hii ngwe, tuone kinachofuata.
siku moja niliuliza, hivi ikitokea, jk akajifanya kichaa, awafunge akina mapacha watatu, je cdm itakuwa na hoja gani ya mvuto?
kujiimarisha kwa kutumia udhaifu wa mwenzio sio deal.
wakubwa eee, sikilizeni ushauri.
HONGERA SANA BOSS
The Boss, siasa ina manjonjo yake. Unakumbuka hivi majuzi huko USA yaliyomkuta OBAMA??? Pamoja na kuwa wote wanajua kuwa OBAMA ni Mzaliwa wa USA lakini REPUBLICAN walikuja na hoja ya kuwa inabidi OBAMA atoe Cheti cha kuzaliwa ili waweze kuhakikisha. Republican hawakuwa wajinga kuja na madai hayo, na wala si kuwa hawakuwa na hoja nyingine za kuongelea juu ya uchumi na au day to day activities. Hiyo ndio SIASA BOSS
Hivi ukiwa vitani, akitokea mwenye panga utamwacha sbb wewe unamtafuta mwenye bunduki??....niwakumbushe kidogo, wakati ule wa uchaguzi mkuu Makamba alikuja na story ya unyumba wa Dk.Slaaa na upadri wake alipopigwa lile dongo la kumpa mimba mwanafunzi akawa mpole akafunga mdomo hatukumsikia tena, akaibuka Six na kupinga hoja ya elimu bure eti haiwezekani akaambiwa yeye si msafi na ni fisadi kama wenzake akakumbushwa ile ofisi ya spika ya millioni 500 kule jimboni kwake akawa mpole akanyamaza. Akaibuka Kinana, akapewa dozi yake kuhusu ufisadi wa zile meli zake na akaambiwa makombora mengine bado akatulia akaanza kuongea sera personal attack akaacha, akaibuka Shimbo, akapewa dozi yake ya tenda za kifisadi alizopewa na JK nae hatukumsikia tena. Kilichoponza Riz1 ni yeye na gazeti lake kumsakama kuisakama CDM kapewa dozi yake katulia...huyu Nape kajiingiza mwenyewe safari hii Dk katulia Marando na Mpendazoe wakampa dozi yake...Nape kashakuwa mpole baada ya hapo maandamano na kuwaeleza wananchi ukweli yako pale pale.
Nimevumilia sana kutokusema but nimeshindwa sasa
inabidi niseme tu kilicho moyoni kwangu.
Kwa ufupi nashangazwa na busara za CHADEMA na Dk Slaa.
Mimi ni katika wale ambao nimesha give up na CCM.
Chochote watakachokifanya kikiwa kibaya sishangai na kikiwa kizuri
kwangu hakivutii.
Sasa nilitegemea CHADEMA wawe tofauti saana lakini
wanayoyafanya mimi naona kama hawapo serious kabisa.
1. La kwanza ni hili la kujaribu na kujibizana na watu wa CCM,
kwanza kwa nini chadema wana react na mambo ya CCM?
Mfano mkutano mkuu wa ccm na suala la kujivua gamba?
Kwa nini kwa mfano chadema walishindwa nini kudharau na
kutokuongea lolote, badala yake wakawa wanazungumzia
namna ya kupunguza gharama za maisha zinazopanda, na namna
ya kuwafaidisha watanzania na zoezi la mjadala wa katiba mpya?
2. Kwa nini wasizungumze ni vipi katiba mpya itawasaidia watanzania
kupambana na rushwa, ufisadi na matatizo mengine?
3. Imeandikwa kwenye media kuwa, watuhumiwa wa ufisadi
watawatumia viongozi wa vyama vya upinzani kumtukana Kikwete
na familia yake, na siku haipiti Dk Slaa anaanzisha madai ya Ridhiwani?
Imean hata kama yuko right,what about the wrong time?
kwa nini now wakati inatangazwa maadui wa Kikwete watakitumia chama cha upinzani?
4. Tazama hili la Nape na CHADEMA, nani anaefaidika kama sio
watuhumiwa wa ufisadi, maana sasa hawazungumzwi wao.
attention imehama kutoka kwao. Kwa msaada wa Dk Slaaa.
5. Hivi hata kama Nape alitaka kujiunga HADEMA au CCJ, kumuumbua huko
kunaleta faida au hasara kwa CHADEMA?
6. watu wengine walio CCM nao wangependa kuondoka, wanaonaje?
Hivi CHADEMA hawawezi kuzungumza kuhusu mustakabali wa tanzania bila
kuzungumzia CCM kwa jazba?
Mimi nakuwa dissapointed na CHADEMA.
Kwa sababu hata wakati wa uchaguzi, Mbowe na wenzie wa CHADEMA
walinishangaza walipomlalamikia Kikwete kufanya kampeni baada ya muda rasmi
kupita, badala ya CHADEMA kupinga hiyo sheria ya kipuuzi ya kuweka limit ya masaa ya kampeni.
CCM wanakivuta CHADEMA kwenye malumbano, hii inasababisha CHADEMA i-withdraw attention kwenye mambo muhimu.
CHADEMA walivyoanza suala la katiba yakaja mabomu ya gongo la mboto, walivyokuja na dowans isilipwe akajitokeza babu wa Samunge, sasa wanahubiri ugumu wa maisha huku kuna kuvuana magamba CCM.
Naona mwanzishaji wa hii thread alishakata tamaa kabisa hata kama ukifanya lolote jema. Mimi binafsi nafikiri hiyo strategy wanayotumia CHADEMA ku-REBUT uongo unaoenezwa na CCM ni nzuri. Hata Jaluo wa Marekani (Obama) alitumia the same strategy ku-shut down uongo uliokuwa unaelekezwa kwake na Republican na Talk Radio hosts wa ki-conservative wakati wa uchaguzi mkuu US. Matokeo yake conservatives waliumbuka.
Huwezi kunyamaza wakati uongo unaundwa kuwa ukweli. JK alitajwa kuwa ni fisadi, hajawahi hata siku moja kukanusha hilo wala kwenda mahakamani kwa kuchafuliwa jina. That means anakubaliana na hao waliomtuhumu kwa ni fisadi. Na hakuna Ubishi katika hilo, JK is FISADI.
Ni vema CHADEMA wakaendelea ku-rebut uongo wa CCM kwa uthibitisho.
Kudo CHADEMA.
kweli kabisa chadema inabidi ishughulike na mambo ya wananchi kuendelea kujibizana na ccm ni kupoteza attention ya mambo ya msingi nakuunga mkono mkuu the boss
And how the f**k you gonna go about it?who is the duty bearer? Is it cdm or the govt of ccm?
The right holders are the tz communities the role of cdm is not to provide the services/rights to tz communities but to hold the duty bearers accountable to tz communities' rights.
Ma agent wa CCM ndani ya JF wala hawajifichi.