Chadema wamshambulia Edward Lowassa

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,148
Na Sharon Sauwa
24th March 2010

1269415959_lowassanew.jpg

Aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ameshambuliwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikiwahoji watu wa jamii ya Kimasai kuamua kutoa cheo cha kimila kwa mtu ambaye amekuwa akikaa kimya wakati wanagombania ardhi...Mashambulizi hayo yalitolewa jana na Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri Kuu ya Chadema, John Mrema, wakati akihutubua mkutano wa operesheni Sangara katika kijiji cha Mbeli wilayani Kiteto, Mkoa wa Manyara.

Mrema alisema Wamasai wilayani Kiteto wamekuwa wakijeruhiwa na kuuawa katika mapigano ya kugombea ardhi kati ya wakulima na wafugaji.

Alisema kuwa ugomvi huo ungeweza kutatuliwa kwa kutenga ardhi kwa ajili ya wakulima na wafugaji, lakini hadi sasa serikali ya CCM haijachukua hatua.

Mrema alisema nchi nyingi ambazo zimekuwa na mapigano sababu kubwa ni ugomvi wa ardhi na kutahadharisha kuwa kama matatizo hayo hayatarekebishwa, nchi itaingia katika matatizo makubwa.

Alitolea mfano kwa Sudan ambayo alisema vita ilisababishwa na mafuta pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) kuingia katiika mapigano kutokana na kugombania madini. "Nyie Wamasai mmetoa cheo kwa Lowassa ni vipi mnampa cheo cha kimila mtu ambaye amekuwa hawatetei, anakaa kimya bungeni?" alihoji Mrema.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, amelitaka Jeshi la Polisi nchini kukaa pembeni wakati wa uchaguzi mkuu na kukiacha chama chake kipambane na CCM kwa uhuru. Alitoa kauli hiyo jana wakati akihutubia mkutano wa operesheni Sangara uliofanyika katika viwanja vya Kata ya Kitelesa, wilayani Kondoa."Tuacheni tupambane na CCM wenyewe, msiingilie," alisema Mbowe.

Alisema wakati wa uchaguzi, polisi wamekuwa wakiwaandama wananchi na vyama vya siasa.

CHANZO: NIPASHE
 
Na Sharon Sauwa
24th March 2010

1269415959_lowassanew.jpg

Aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ameshambuliwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kikiwahoji watu wa jamii ya Kimasai kuamua kutoa cheo cha kimila kwa mtu ambaye amekuwa akikaa kimya wakati wanagombania ardhi...Mashambulizi hayo yalitolewa jana na Mkurugenzi wa Bunge na Halmashauri Kuu ya Chadema, John Mrema, wakati akihutubua mkutano wa operesheni Sangara katika kijiji cha Mbeli wilayani Kiteto, Mkoa wa Manyara.

Mrema alisema Wamasai wilayani Kiteto wamekuwa wakijeruhiwa na kuuawa katika mapigano ya kugombea ardhi kati ya wakulima na wafugaji.

Alisema kuwa ugomvi huo ungeweza kutatuliwa kwa kutenga ardhi kwa ajili ya wakulima na wafugaji, lakini hadi sasa serikali ya CCM haijachukua hatua.

Mrema alisema nchi nyingi ambazo zimekuwa na mapigano sababu kubwa ni ugomvi wa ardhi na kutahadharisha kuwa kama matatizo hayo hayatarekebishwa, nchi itaingia katika matatizo makubwa.

Alitolea mfano kwa Sudan ambayo alisema vita ilisababishwa na mafuta pamoja na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) kuingia katiika mapigano kutokana na kugombania madini. “Nyie Wamasai mmetoa cheo kwa Lowassa ni vipi mnampa cheo cha kimila mtu ambaye amekuwa hawatetei, anakaa kimya bungeni?” alihoji Mrema.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, amelitaka Jeshi la Polisi nchini kukaa pembeni wakati wa uchaguzi mkuu na kukiacha chama chake kipambane na CCM kwa uhuru. Alitoa kauli hiyo jana wakati akihutubia mkutano wa operesheni Sangara uliofanyika katika viwanja vya Kata ya Kitelesa, wilayani Kondoa.“Tuacheni tupambane na CCM wenyewe, msiingilie,” alisema Mbowe.

Alisema wakati wa uchaguzi, polisi wamekuwa wakiwaandama wananchi na vyama vya siasa.

CHANZO: NIPASHE
Hiki chama matatizo ona majina yote ya viongozi wao ni akina 'MEKU'
 
hakuna aliposhambuliwa , ila wameeleza ukweli kuwa Lowassa hashughulikii matatizo ya waliompeleka kule Bungeni, yeye kutwa kwenye vikao na kina RA na mafisadi wa kariba hiyo.
 
Back
Top Bottom