BUBERWA D.
JF-Expert Member
- Apr 22, 2011
- 2,293
- 1,170
nadhani unashindwa kutofautisha siasa za majukwaani na siasa za kimipango. vilevile tujue kuwa mtoto wa kiongozi naye ni binadamu kama wengine na nimtanzania na mwenye haki kama wengine. jambo kubwa la kujadili ni je? nafasi hizo wanazipata kwa ushindani uliohuru kama wengine? kama kuna walakini katika upatikanaji wa nafasi hizo hiyo ndo hoja ya msingi. najua kuna taratibu za kuwapata viongozi ndani ya vyama vyao. nadhani anayesambaza huo ujumbe anatakiwa kutueleza walivyo "by-pass" taratibu ili watoto wao wapate nafasi hizo na hata wengine wametishwa kujiondoa ili watoto wao wapate.Ndungu wana Jr. nashangazwa sana na sera ya Chadema na mwendelezo wake hadi sasa wamepoteza mwelekeo. Awali ya yote huwa nawambia Chama hiki kipo after maslahi ya wachache, baada ya kugunduwa Ndg; Godbless Lema ameshindwa kwenye kesi aliyokata rufaa sasa mawazo yao yote yamehamia Arusha. Jiulize ni kwa nini ARUSHA na si kwingineko? sababu kubwa Arusha watalii wanaingia wengi hivyo kipato kipo, pamoja na wavuta ............... wa machimbo wapo kwa wingi. Mbona Tanga baada ya kutishwa na kijana wa Makamba wamekuwa kimya au hawakusikia alicho sema?
Nauliza tu hivi vyama vingine havina mpango wa Uchaguzi ndani ya vyama vyao? kwani kila kukicha CCM imekuwa hivi !!!!!!!!!, au ndo kusema waliopo hakuna wakuwatoa?
Cha ajabu sana Chadema wamefuata nyayo ya CCM kwa kutumia mtandao wa sms kutumia watu ujumbe hata wasiowahusu.(( Nanukuu ujumbe niliotumiwa hivi punde; HATARI! Angalia, watoto wa vigogo waliopita UVCCM ngazi ya taifa DICKSON MEMBE, FRED LOWASA, RIDHIWANI KIKWETE, ASHURA HUSSEIN MWINYI, BENY SAMWEL SITA, DEBORA MWANDOSYA, IREN PINDA, FELSTER NDUGAI, CHRISTOFER NDEJEMBI, SHARIFER BILALY, HAWA KIGODA, JUDITH MUKAMA NA JALOME MSEKWA. Nchi hii imekwisha. Inatia hasira, wacha watoto wa maskini tupambane kupitia mlango mwingine ''CHADEMA'' ili kutete maskini wenzetu, wazazi na watoto zetu! Vita Hii Inaanza Sasa! Upatapo meseji hii , tuma kwa WAZALENDO wenzako 5 )) Mwisho wa kunukuu.
Je CHADEMA kuna ngugu wa viongozi wangapi hadi sasa au ndo huwa sielewi tena ngazi kubwa kabisa? Mfano Dr. Slaa Mkewe mtelekezwa ni Mb wa kuteuliwa, ambapo mteuaji mkubwa ni Dr. Slaa mwenyewe, Wakili maarufu wa kuongea sana na Mwanasheria Mkuu mtarajiwa Dada yake naye ni Mb wa kuteuliwa. Wapo wengi sana lakini vyanini wakati wote wanashibisha matumbo yao kwa kutumia udhaifu huu wa kuto kufikilia mbali, na kutegemea mawazo dhaifu kama haya.
Chadema kimekuwa kinavuta watu kwa nguvu kuingia kwenye Chama, bila kujua madhara yake makubwa ya baadae, Mfano Kiongo anasimama anasema VUA GAMBA VAA GWANDA. Fikilia huyu unayemvuta aliko sasa unamponda je akija huku utamwosha na Omo ili atakate ama atakuja kuendeleza ufisadi?
Nawasilisha TUUNGANE KUJENGA NCHI SIYO KUBOMOA
jambo la msingi sio ..."mbona na wale wanafanya hivyo"? hilo haliwezi kuhalalisha uovu wowote.
swala la kukutumia sms ni swala la kawaida na tabia ya vyama vya siasa kushawishi wasiokuwa wao wajiunge.
swala la sms wala halijaasisiwa na ccm. hata ccm imeiga. nakumbuka hata daruso-udsm tulitumia sms kabla ya ccm.
swala la vua gamba vaa gwanda ni jambo jema tu kwa chama kujitafutia wana chama. kumbuka chama ni taasisi yenye miongozo yake na ndiyo yenye miongozo ya mienendo ya wanachama wake. kwa hiyo hata huyo mwenye gamba akiingia akakuta mfumo mzuri wa maadili na miiko atakuwa mzuri tu. hakuna aliye zaliwa ni gwanda au gamba ila mifumo yetu ndiyo imekuwa ikituumba au kutuumbua. kingunge wa miaka ya sitini na sabini enzi za mfumo wa maadili na miiko wa mwalimu ni tofauti na kingunge wa leo wa mfumo ulio oza ili hali chama ni kilekile. tafakari.