CHADEMA/UKAWA mmejipangaje na 2020?

CHADEMA/UKAWA mmejipangaje na 2020?

wengine tuliuliza kipaumbele na main objective ya kuanzishwa UKAWA ni upi??mbona sioni lengo la kuanzishwa kwake,mmebaki kudandia vitu vya msimu yaani kwa kifupi mnaendeshwa na upepo,linalokuja hilohilo ndilo mnalokimbizana nalo,malengo na kipaumbele cha chama kikuu cha upinzani ni kipi??kuna watu wanasingizia eti marufuku ya mikutano imefanya wao wasituhabarishe juu ya malengo ya chama ,ni upuuzi.semeni tu kama mnaridhika na hali ya kulalamika baada ya uchaguzi kila election tuwaelewe.
 
Watajipangia wapi na wakati Mikutano ya kuweza kujipanga imepigwa marufuku!

Huwezi ukafanyia Siasa Chumbani ni lazima utoke uende kwa wananchi uwaeleze a,b,c etc..

Tumekaa kutoa Lawama kwa Upande mmoja pasipo kuangalia upande mwingine..

Nguvu ya umma haina kizuizi.

Kama huamini nenda kamuuliza Hosni Mubarak.
 
obila mkono hii nchi hatutaheshimiana
 
Nyani Ngabu bwana.

Yaani bado unahangaika na watu wasio na ajenda?

ACT Wazalendo baada ya kumaliza mkutano wao wa Kidemokrasia mwezi mmoja uliopita walitoka na Ajenda ya kudai katiba ya wananchi.

Baada ya Chadema kuskia hiyo ajenda haraka haraka nao wakaita waandishi wa habari na kuja na ajenda ya katiba mpya na kuagiza kila wilaya wafanye vikao vya kuhusu katiba.

Lkn mpka sasa hivi hakuna kikao wala mkutano yaani hawana wanachosimamia na wataendelea kurukaruka hivyo hivyo mpka 2020 na CCM wanarudi madarakani kwa kishindo.
 
Sijaelewa! yaani unataka uelezwe formulae za CDM kwa mwaka 2020 humu jf???
 
Nawaona Chadema wakipotea kwenye ramani kama ndoto vile. Inauma sana tena sana, nawachukia ccm na mambo yao. Lakini Chadema wamegeuka kuwa watu wa hovyo hovyo na kutetea mambo ya hovyohovyo sana, hata tukiwaambia wanabaki na ujuaji pamoja na utetezi wa hovyo hovyo kwenye ukweli. Hata siku hizi wanapoitwa manyumbu acha tu waitwe, kosa lililofanyika mwaka 2015 ndiyo sumu waliyojaribu kwa kuilamba.
 
Haya, kama kulikuwa na shaka au sintofahamu juu ya suala la katiba mpya, hali hiyo imeondolewa na kauli ya si mwingine bali mtukufu wetu mwenyewe, rais wetu mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Mwenyewe kwa mdomo wake wakati alipoongea na waandishi wa habari kwenye mkutano wake na wao alisema kwamba wakati wa kampeni hakuahidi chochote kuhusu katiba mpya na hivyo kwake si suala lenye kipaumbele.

Sasa nyie chama kikuu cha upinzani mmejipangaje ? Bado mtashiriki kwenye huo uchaguzi na kuendelea kuwa wasindikizaji wa CCM ikulu?

Wiki chache zilizopita niliwashauri msusie chaguzi zote zijazo hadi hapo kitapoeleweka kuhusiana na katiba mpya pamoja na tume huru ya uchaguzi.

Vipi sasa baada ya kusikia moja kwa moja kutoka kwa mkulu, bado mstashiriki huo uchaguzi [wa 2020]?

Unaanza kukera sasa
 
Back
Top Bottom