Nanyaro Ephata
JF-Expert Member
- Jan 22, 2011
- 1,237
- 1,828
Ndugu zetu Arusha leo Feb 8 tunaenda kuhitimisha kampeni za udiwani wa kata ya Sombetini zilizoanza Jan 16.Hitimisho la kampeni hizi ambazo sisi CHADEMA tutahitimisha katika viwanja vya Ngusero,tunahitimisha kampeni wakati wanachama wetu 9 wakiwa wamejeruhiwa kwa mapanga na green guard.
Jumamosi ya leo inatukumbusha Tarehe 15.06.2013 viwanja vya Soweto wakati wa hitimisho la Kampeni za kata nne,pale watawala walipouwa raia wasiokuwa na hatia kwa bomu.Lilikuwa tukio ovu kabisa katika historia ya mageuzi ya nchi yetu,ulikuwa ukiukwaji mkubwa sana dhidi ya utu na haki ya kuishi ya binadamu.Hata hivyo hatutokata tama wala kurudi nyuma dhidi ya wakandamizaji, wanyonyaji, wakiukaji wa haki za binadamu.Hata hivyo umma wa Arusha ukadhihirisha kuwa haukubaliani na mauaji haya na hivyo tukashinda kata zote nne.
Tunahitimisha kampeni zetu tukiwa wajasiri sana,tukiwa na uhakika wa ushindi wa 95%,ushindi ambao utakuwa kwa heshima ya wale waliouwawa katika harakati za mabadiliko ya Taifa letu.
Tunawashukuru sana Sombetini kwa kutuunga mkono,tutalinda kura zetu kwa gharama yoyote
A man who won't die for something is not fit to live.
Jumamosi ya leo inatukumbusha Tarehe 15.06.2013 viwanja vya Soweto wakati wa hitimisho la Kampeni za kata nne,pale watawala walipouwa raia wasiokuwa na hatia kwa bomu.Lilikuwa tukio ovu kabisa katika historia ya mageuzi ya nchi yetu,ulikuwa ukiukwaji mkubwa sana dhidi ya utu na haki ya kuishi ya binadamu.Hata hivyo hatutokata tama wala kurudi nyuma dhidi ya wakandamizaji, wanyonyaji, wakiukaji wa haki za binadamu.Hata hivyo umma wa Arusha ukadhihirisha kuwa haukubaliani na mauaji haya na hivyo tukashinda kata zote nne.
Tunahitimisha kampeni zetu tukiwa wajasiri sana,tukiwa na uhakika wa ushindi wa 95%,ushindi ambao utakuwa kwa heshima ya wale waliouwawa katika harakati za mabadiliko ya Taifa letu.
Tunawashukuru sana Sombetini kwa kutuunga mkono,tutalinda kura zetu kwa gharama yoyote
A man who won't die for something is not fit to live.