CHADEMA, tumeingia katika mtego wa kujadili agenda zinazoibuliwa na CCM na tunaacha kuongelea matatizo ya wananchi

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,372
Ni bahati mbaya sana viongozi na wafuasi wa CHADEMA na upinzani kwa ujumla tunaonekana kunasa katika mtego huu wa CCM wenye lengo la kutuvuruga, kutogombanisha na zaidi kutufanya tutumie muda mwingi kujadili agenda na propaganda zinazobuliwa na CCM badala ya sisi kama upinzani kuibua madhaifu ya serikali hii ya CCM.

Tunachopaswa kutambua ni kuwa,hawa mabwana kwa sasa wameshagundua udhaifu wetu wa kujadili zaidi agenda ya hamahama wanayoiibua kila kukicha badala ya kutumia muda wetu kuibua na kujadili mambo mengi ambayo awamu hii imeshindwa kuyatekeleza pamoja na makosa waliyoyafanya.

Ndungu zangu,hata Lowassa kukubaliwa kwenda Ikulu kipind hiki inawezekana ni sehemu ya mkakati huu au muendelezo wa huu mkakati wa wao ku-set agenda na sisi tukabaki tunatumia muda mwingi kujadili agenda hizo badala ya kuwaeleza wananchi ni jinsi gani utawala huu unavyofeli katika mambo kadha wa kadha.

Je,leo hii Sumaye alielalamika kunyang'anywa mashamba yake akiitwa Ikulu kujadili kuhusu mashamba hayo unadhani atakataa?

Je,akiitwa Ikulu na kupewa habari za matumaini na kisha nae akasifia huu utawala,tutaanza tena kujadili mazunguzo ya Sumaye na Mkulu?Ita
kuwa ni akili tukaanza tena kuparuana kisa Sumaye kasifia huu utawala?

Viongozi wa CHADEMA na mashabiki wa upinzani ni bora tukapuuza hizi habari za hamahama au sijui nani kaenda Ikulu na badala yake tujikite kueleza mapungufu ya hii serikali na zaidi tupaze sauti kutetea wananchi.

Tutambue hii hamahama na watu kwenda Ikulu havitaisha leo wala kesho bali ni mambo yatakayokuwa yanafanywa kimkakati ili kututoa kwenye reli maana kama ni wa kuhama bado wako wengi na mkakati huu unaweza kuendelea mpaka 2020.

Ingekuwa ni busara na jambo la kimkakati kama leo mbunge au diwani wa CHADEMA anatangaza kujiuzulu na kuhamia CCM,kesho Tundu Lissu anakuja na barua au waraka kutoka Uturuki akielezea mkakati au mpango wa CHADEMA kwenda mahakani kufungua kesi kupinga makato ya asilimia 15 kwa ajili ya Bodi ya Mikopo.

Wakati wao wanatangaza kumpokea kiongozo kutoka upinzani,waziri kivuli wa utumishi anapanga kukutana na waandishi wa habari kueleza ni jinsi gani serikali hii imeshindwa kuboresha masilahi ya watumishi wa umma pamoja na kushindwa kulipa malimbikizo yao.

Wakati Mkulu anaibua kashifa mpya ya ufisadi,kiongozi wa kambi rasimi ya upinzani na mwenyekiti wa chama anaita waandishi na kueleza mlolongo wa kashifa na tuhuma kibao ambazo mpaka sasa hakuna mtuhumiwa hata mmoja alieshitakiwa mahakamani.

Si hivyo tu,wakati wao wanaendelea kujisifu kuongeza mapato,waziri kivuli wa elimu anaita waandishi wa habari na kuwaeleza idadi ya wanafunzi waliokosa mikipo au kupewa mikopo kiduchu pamoja na vigezo vipya vinavyowabana wanafunzi wengi kupata mikopo.

Badala ya kukaa na kujadili hamahama,CHADEMA kama chama huu ni wakati wa kutoa awareness kwa umma juu ya mapungufu yaliyoko katika mswaada unaotarajiwa kuwasilishwa Bungeni kuhusu kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii.

Wakati wao wanaendelea kuchukua madiwani wetu,sisi kama wapinzani ni wakati wa kuhoji hatima ya mazunguzo ya makinikia,kutaka mikataba ya ununuzi wa bombedier na ujenzi wa reli ya kisada iwekwe wazi/iwasilishwe Bungeni..

Wakati wanajinadi kuwa hii ni serikali ya wanyonge, ni wakati wa upinzani kuisuta hadharani serikali hii kwa kushindwa kutimiza ahadi ya kutoa milioni 50 kwa kila kijiji.

Jamani hii ndio kazi ya upinzani na si kujadili Lowassa kaenda Ikulu au sijui nani kahamia CCM kutoka upinzani.

CHADEMA imefika hapa ilipo kwa kupigania matatizo ya wananchi agenda ambayo sasa tumewekwa mtegoni ili tuitelekeze na tubaki kujadili hamahama,fulani kaenda Ikulu au mheshimiwa leo kaibua ufisadi fulani bandarini, n.k

Ndungu zangu, tunapotea na sasa ni bora turudi kwenye mstari kwa kuongelea zaidi agenda zinazogusa maisha ya wananchi wengi moja kwa moja kama kilimo,ajira,n.k. na kuionyesha jamii ni kwa kiasi gani hii serikali imekuwa mzigo kwa wananchi.

Pia tumeweka mkazo zaidi katika kuongelea maswala ya demokarasia, utawala bora, utekaji,n.k huku tukisahau matatizo mengine kama shida ya maji,umeme,n.k mambo ambayo yanagusa wananchi moja kwa moja

Tushituke huu ni mtego kwetu.
 
Acha kutufanya watoto
Lowasa kaenda ikulu bila idhini ya chama
Usilembe hata kama hauna macho hata kile walichoongea na JPM ni wazi katuvua nguo wapinzani
 
Wewe ulipo tupo na lowasa wenu acheni kukiharibu chama chetu.
Kama mnaipenda ccm sana na kuisifia sifia hamieni huko.
Chadema kimeharibiwa mno na hawa watu wa CCM
 
Kumbe ukitulia unaongea point za maana, kila siku tunasema humu hizo kelele mlizoaminishwa eti hakuna Uhuru wa vyombo vya habari wakati wamiliki wa vyombo hivyo akina Mengi, Manji, Mbowe etc wote ni matajiri mwananchi wa kawaida inamsaidia nini?,eti demokrasia inaminywa wakati watu vijiweni wana discuss chochote wakiwa free kumbe ni Mbowe na Lema wamepigwa Pin kuzurula mikoa mingine wakae majimboni mwao na kuwakalilisha demokrasia hakuna, hiyo demokrasia inamsaidia nini mwananchi aliye bize na kujipatia kipato?,.Leo nakupongeza sana ingawa wenzako watakubeza.Ni wakati wa kujikita kwenye matatizo ya wananchi ya moja kwa moja.
 
Ni bahati mbaya sana viongozi na wafuasi wa CHADEMA na upinzani kwa ujumla tunaonekana kunasa katika mtego huu wa CCM wenye lengo la kutuvuruga,kutogombanisha na zaidi kutufanya tutumie muda mwingi kujadili agenda na propaganda zinazobuliwa na CCM badala ya sisi kama upinzani kuibua madhaifu ya serikali hii ya CCM.

Tunachopaswa kutambua ni kuwa,hawa mabwana kwa sasa wameshagundua udhaifu wetu wa kujadili zaidi agenda ya hamahama wanayoiibua kila kukicha badala ya kutumia muda wetu kuibua na kujadili mambo mengi ambayo awamu hii imeshindwa kuyatekeleza pamoja na makosa waliyoyafanya.

Ndungu zangu,hata Lowassa kukubaliwa kwenda Ikulu kipind hiki inawezekana ni sehemu ya mkakati huu au muendelezo wa huu mkakati wa wao ku-set agenda na sisi tukabaki tunatumia muda mwingi kujadili agenda hizo badala ya kuwaeleza wananchi ni jinsi gani utawala huu unavyofeli katika mambo kadha wa kadha.

Je,leo hii Sumaye alielalamika kunyang'anywa mashamba yake akiitwa Ikulu kujadili kuhusu mashamba hayo unadhani atakataa?

Je,akiitwa Ikulu na kupewa habari za matumaini na kisha nae akasifia huu utawala,tutaanza tena kujadili mazunguzo ya Sumaye na Mkulu?Ita
kuwa ni akili tukaanza tena kuparuana kisa Sumaye kasifia huu utawala?

Viongozi wa CHADEMA na mashabiki wa upinzani ni bora tukapuuza hizi habari za hamahama au sijui nani kaenda Ikulu na badala yake tujikite kueleza mapungufu ya hii serikali na zaidi tupaze sauti kutetea wananchi.

Tutambue hii hamahama na watu kwenda Ikulu havitaisha leo wala kesho bali ni mambo yatakayokuwa yanafanywa kimkakati ili kututoa kwenye reli maana kama ni wa kuhama bado wako wengi na mkakati huu unaweza kuendelea mpaka 2020.

Ingekuwa ni busara na jambo la kimkakati kama leo mbunge au diwani wa CHADEMA anatangaza kujiuzulu na kuhamia CCM,kesho Tundu Lissu anakuja na barua au waraka kutoka Uturuki akielezea mkakati au mpango wa CHADEMA kwenda mahakani kufungua kesi kupinga makato ya asilimia 15 kwa ajili ya Bodi ya Mikopo.

Wakati wao wanatangaza kumpokea kiongozo kutoka upinzani,waziri kivuli wa utumishi anapanga kukutana na waandishi wa habari kueleza ni jinsi gani serikali hii imeshindwa kuboresha masilahi ya watumishi wa umma pamoja na kushindwa kulipa malimbikizo yao.

Wakati Mkulu anaibua kashifa mpya ya ufisadi,kiongozi wa kambi rasimi ya upinzani na mwenyekiti wa chama anaita waandishi na kueleza mlolongo wa kashifa na tuhuma kibao ambazo mpaka sasa hakuna mtuhumiwa hata mmoja alieshitakiwa mahakamani.

Si hivyo tu,wakati wao wanaendelea kujisifu kuongeza mapato,waziri kivuli wa elimu anaita waandishi wa habari na kuwaeleza idadi ya wanafunzi waliokosa mikipo au kupewa mikopo kiduchu pamoja na vigezo vipya vinavyowabana wanafunzi wengi kupata mikopo.

Badala ya kukaa na kujadili hamahama,CHADEMA kama chama huu ni wakati wa kutoa awareness kwa umma juu ya mapungufu yaliyoko katika mswaada unaotarajiwa kuwasilishwa Bungeni kuhusu kuunganisha mifuko ya hifadhi ya jamii.

Wakati wao wanaendelea kuchukua madiwani wetu,sisi kama wapinzani ni wakati wa kuhoji hatima ya mazunguzo ya makinikia,kutaka mikataba ya ununuzi wa bombedier na ujenzi wa reli ya kisada iwekwe wazi/iwasilishwe Bungeni..

Wakati wanajinadi kuwa hii ni serikali ya wanyonge, ni wakati wa upinzani kuisuta hadharani serikali hii kwa kushindwa kutimiza ahadi ya kutoa milioni 50 kwa kila kijiji.

Jamani hii ndio kazi ya upinzani na si kujadili Lowassa kaenda Ikulu au sijui nani kahamia CCM kutoka upinzani.

CHADEMA imefika hapa ilipo kwa kupigania matatizo ya wananchi agenda ambayo sasa tumewekwa mtegoni ili tuitelekeze na tubaki kujadili hamahama,fulani kaenda Ikulu au mheshimiwa leo kaibua ufisadi fulani bandarini, n.k

Ndungu tunaacha tunapotea na sasa turudi kwenye kuongelea agenda zinazogusa maisha ya wananchi wengi moja kwa moja kama kilimo,ajira,n.k.

Pia tumeweka mkazo zaidi katika kuongelea maswala ya demokarasia, utawala bora, utekaji,n.k huku tukisahau matatizo mengine kama shida ya maji,umeme,n.k.

Tushituke huu ni mtego kwetu.

Hizo changamoto za wananchi chadema wanaweza kuzitatua kwa kufanya kitu gani?

Na unajua wao hawana serikali na ilani inayofuatwa sio yao ni ya ccm
 
Mkuu heshima kwako

1. Tayari unajadiri ajenda ya CCM nakushauri uwe unajadiri agenda za CDM. Ndiyo maana sisi wengine tunazijibu kwa hoja kiaina na matusi.

2. Ni vigumu kwenye jamvi hili kujadiri ajenda zenye tija il mradi CCM wanazikodolea na kuzivamia kwa upuuzi wa ajabu wakati mwingine hata bila malengo.

3. Wao wana forum zao ambazo nina uhakika huwezi jinafasi kama humu. Pia wanatumia ofisi za serikali kwa kila rasilimali kuning'inia humu JF.

4. JF mods wanamchango mkubwa sana kupromoti ajenda za CCM

Yapo mengi ya kufanya kuepukana na janga hili.

i. Kususia kuchangia ajenda zao kuna faida ya kuwafanya wajione irrelevant, hasara zake kwanza wengi wetu hatuna kifua cha kususia. Pili kuzijibu kwa hoja kunawapa faida ya kupata mirejesho muhimu kuhusu CDM (Iwapo wana akili hiyo). Tatu kuna kundi la dola lenye kila rasilmali linalotumiwa na CCM kujenga hoja humu, hawa ni maadui namba moja kwa sababu ajenda yao siyo siasa zenye tija kwa afya ya demokrasia ni watumishi kwa maana ni watumwa. Wanasema ukimjua adui yako umefaidika na mkakati wa kupambana naye.

ii. Ikulu yetu imegeuzwa ofisi kuu ya CCM. Cha muhimu ni kusoma na kuziacha propaganda za ikulu kwa sababu haziwahusu wapinzani wala nchi zinamhusu Magu tu.

iii. Nina uhakika umewatambua wachangiaji wenye mawazo mazuri kama yako. Kwa enzi hizi za teknologia na kwa kutumia hii hii JF ajenda za upinzani zinaweza kujadiriwa. Ni kwa kucombine hoja za hapo juu. Pia, kutumia inbox kama siyo subforum humu humu yenye uwezo wa vetting kama Great Thinkers forum; tatizo ni kama JF wataridhia.

Usisahau kuwa pamoja na wasomaji wengi wa humu JF, si sampuli halisi ya fikra za wananchi kwenye masuala ya siasa za Tanzania. KWA HIYO faidika na kusoma, usihangaike kudakwa na chambo.
 
Umeongea point sana mkuu!
Watawala wameshatusoma sana sisi watanzania wote bila kujali vyama vyetu kuwa wengi ni bendera fuata upepo.
Kila linaloanzishwa kimkakati wote tunazamia huko 100/100.
Sasa hivi chadema tunapaswa kuwa tunatakiwa kumuandaa mgombea wa 2020,hivyo Ngoyai aende ikulu asiende kwetu isiwe hoja maana kwake umri ushaenda na hana nafasi tena iwe CCM ama UKAWA.
Chadema wasimamie kukosoa kasoro za kiuchumi ambazo zinawakabili watu wengi
Tuwe na hoja kinzani za namna tofauti ambayo serikali yetu ingeongozwa kama tungechukua nchi
Wam
 
Mie nadhani hata huu uamuzi wa Chadema kususia uchaguzi utakuwa ni ushauri wa Lowassa huu huku yeye akiendelea kufanya mambo ndani ya chama kwa siri.
Ishu ni kwa nini mwana CHADEMA ndo atumike kuivuruga CHADEMA?? Why Lowassa atumike kutuvuruga. na yeye yupo comfortable tu akiona CDM inawaka moto kwa sababu ya maslahi yake.
 
Ukawa wajikite kuwaletea maendeleo wananchi kwenye majimbo yao waache porojo.Chukulia MTU kama Lisu hajawahi ongelea kero za jimbo lake hata siku moja kutwa yuko anapiga umbeya usiohusiana na jimbo lake.Wananchi walimchagua ahangaikie kero zao za maji,elimu ,afya nk za jimboni kwake .Kuchagua wabunge wa upinzani ni kupoteza muda
 
Mie nadhani hata huu uamuzi wa Chadema kususia uchaguzi utakuwa ni ushauri wa Lowassa huu huku yeye akiendelea kufanya mambo ndani ya chama kwa siri.
naona sasa unaanza kukua ingawa unakua hovyo
 
Back
Top Bottom