Chadema tahadhari

Kisendi

JF-Expert Member
Jan 29, 2009
699
178
Ndugu wana JF
Naomba niwasihi chadema kuwa Mh Shibuda atakivuruga chama ni heri kumuondoa mapema na walifanya kosa kumchukua sasa.

Upande mwingine swali kwa chadema je hizi posho mlikubaliana wote au iliibuka tu. Mwisho Mkae mkao wa kula maana hii hali ya taharuki na mabishano yanaua chama na kupunguza uaminifu ndani ya chama. Wananchi huku pembeni wanajiuliza kwa watu wananunuliwa maana Watz wengi hatuwezi kuridhika. Hili suala la Arusha na hili suala la Shibuda liangaliwe uzuri. Namuomba Dr Slaa, Zitto na Mbowe wakae vizuri. Waongee na Shibuda ili kama hakubaliani na makubaliano ya chamani heri akae pembeni.

Nchi itajengwa na wachache maana watz wengi kwa sasa tamaa na kutoridhika ndio hapa tulipo mpaka sasa maana kila idara, kila mtu, kila mtz, kila mwanachama, kila raia anatamani atajilike kuliko kufanya kazi kwa kutumia ubongo wake na ubunifu bila kufoji, bila kutumia chama, bila kutumia taasisi,bila kutumia serikali bila kutumia chochote ambacho yeye atapata pesa nyingi kwa siku.

MFANO umeme kwa nini tusiandamane kumshinikiza ngeleja aachie ngazi na wenzake. MBONA NCHI ZA WENZETU WANAFANYA NA MATOKEO YAKE nchi na watz ambao hatuna uwezo wa kununua generator, Solar panel tutaishi je bila kuuza juice, bila photocopy, bila kuuza bar, bila kutengeneza magari, kuuza maji, kuuza bite etc


NAOMBA NIWAKILISHE CHADEMA LIANGALIENI HILI NA MKAE KWA MAKINI NA HASA WALE WANAOHAMA CHAMA KUTOKA CHAMA KINGINE KUJA CHADEMA. WATAUA CHAMA HATA 2015 HAIJAFIKA.
 
Shibuda anatumika na kundi fulani!, maana si mara yake ya kwanza kufanya anayofanya sasa!
Sheria ya kumwondoa Mbunge inasemaje?
 
Wamfute uanachama na ubunge atausikia kwenye radio.Ana tuabisha wasukuma huyu ndumila kuwili.
 
Wamfute uanachama na ubunge atausikia kwenye radio.Ana tuabisha wasukuma huyu ndumila kuwili.

Shibuda anachotaka kufanya ni kwamba akifukuzwa ubunge atakimbilia mahakamani kuomba COURT INJUCTION,kwa hiyo atakuwa na uhakika wa kuendelea kuwa mbunge kwa kulindwa na mahakama huku akichafua chadema.
 
Shibuda anachotaka kufanya ni kwamba akifukuzwa ubunge atakimbilia mahakamani kuomba COURT INJUCTION,kwa hiyo atakuwa na uhakika wa kuendelea kuwa mbunge kwa kulindwa na mahakama huku akichafua chadema.

Injuction kivipi please explain mkuu
 
Ni kumuacha aendelee na upuuzi wake lakini awekewe watu makini kumchunguza nyendo zake.Kumvumilia mjinga nayo ni credit kwa umma, maana shibuda ni mmmoja kati ya kenge walio katika msafara.Shibuda hana madhara kwa sasa kwani mbinu anazotumia ni za kizamani hawezi kudhoofisha chama.CDM wamfuatilie sana hasa kule jimboni kwake na kisha wafanye assessment to determine the probabilty of his riskness within CDM, WHETHER low range, medium range high range.Kisha wafanye maamuzi
 
Shibuda anachotaka kufanya ni kwamba akifukuzwa ubunge atakimbilia mahakamani kuomba COURT INJUCTION,kwa hiyo atakuwa na uhakika wa kuendelea kuwa mbunge kwa kulindwa na mahakama huku akichafua chadema.

Kweli mkuu nimekumbuka mbunge mmoja wa CUF alitumia staili hii na hatimaye kipindi cha ubunge kilipokwisha akarudi kwa waliomtuma akapokelewa kama shujaa. Kosa lilifanyika tangu mwanzo kupokea hiki kirusi toka CCM. CDM wajifunze kutokana na kosa, hili si kila mtu ana sifa ya kuwa mwanachama wa CDM kwani alikimbilia huko kuitumia CDM kama daraja la kupatia Ubunge alipokwisha upata hana sababu tena ya kuipenda CDM
 
Kweli mkuu nimekumbuka mbunge mmoja wa CUF alitumia staili hii na hatimaye kipindi cha ubunge kilipokwisha akarudi kwa waliomtuma akapokelewa kama shujaa. Kosa lilifanyika tangu mwanzo kupokea hiki kirusi toka CCM. CDM wajifunze kutokana na kosa, hili si kila mtu ana sifa ya kuwa mwanachama wa CDM kwani alikimbilia huko kuitumia CDM kama daraja la kupatia Ubunge alipokwisha upata hana sababu tena ya kuipenda CDM

Ni kweli,katika shamra shamra za kuwapokea wahamiaji ni lzm mtu aonyeshe utayari wa kwenda pamoaja katika yale ambayo yana maslahi kwa taifa,ikiwezekana wapewe mda wa kuwatazama,hatukatai fikra mbadala lakini tabia kama ya Shibuda ni lazima ikomeshwe,atakuwa kama Lyatonga huyo
 
Back
Top Bottom