Ni chama kikubwa kwa sasa tena kilichokua kwa viwango vya kukua.Ni chama kulichosaidiwa na CCM kuwa imara kwa ujinga tu wa CCM. CCM ilifanikiwa kutumia mbinu za kishenzi kuviua au kuvidhoofisha vyama vingine vilivyokua na nguvu na ikafanikiwa.
Lakini CCM kwa mbinu hizohizo za hovyo imegonga mwamba kwa Chama makini CHADEMA. Matokeo yake sasa CCM baada ya kushindwa kuiua CHADEMA sasa inajiua,imejnyonga yenyewe.
Nilikua nasubiri kwa hofu kifo cha CHADEMA 2013, 2014 CHADEMA iko hai. Kizuri zaidi kwangu na wengi wetu CHADEMA imeimarika na kukua mara dufu na hii ndio ikiwa ni mbaya kwa CCM. Sasa hivi CHADEMA ilipofikia hata Mbowe na Slaa waking'atuka CHADEMA itasonga mbele.Na jambo la kushangaza CHADEMA inapiganiwa, inatetewa na kujengwa na watu isiowafahamu na wala sio waajiliwa wala sio viongozi wake.
Mimi binafsi ni mmoja wa voluntier ninaeipigania kwa akili na nguvu zangu zote pia nimegundua kuna watu wengi wanaipigania CHADEMA kwa hiari zao na kwa siri kubwa. Mbinu chafu zimeshindwa sasa CHADEMA jipangeni kwa hila za kuandiiisha wapiga oura na kuzuia wizi wa kura 2015 ndo hii.