CHADEMA ni NGO INAYONUFAISHA WACHACHE

CHADEMA ni NGO INAYONUFAISHA WACHACHE

Wasifu mzito na historia za kutukuka za baadhi ya wateule wanaounda
timu ‘mpya' ya viongozi watendaji wa CCM kwa kiwango kikubwa ndicho
kitu kikubwa pekee kinachosababisha mtu yeyote makini ajikute akipata
shida kuyabeza yale yaliyofanywa na chama hicho tawala mwishoni mwa
wiki kule Dodoma.................absalom kibanda critical thinking

Msuko mpya wa safu ya wakuu wa idara za CCM uliotangazwa na Rais
Jakaya Kikwete ukiwajumuisha wanasiasa wasiojua mizaha wawapo kazini
kama alivyo Philip Mangula, au makada wa muda mrefu wa chama hicho wa
kariba ya Muhammad Seif Khatib na Zakia Meghji una kila sababu ya
kutafutiwa dawa mahususi na makamanda wa kambi ya upinzani ambao kwa
muda mrefu wamekuwa wakipambana kuing'oa CCM madarakani.

Ni mtu asiyejali au mpuuzi asiyezijua vyema siasa za Tanzania
anayeweza akasimama na kuudharau uteuzi uliofanywa na Rais Kikwete
ambaye baada ya kushindwa mara kadhaa hatimaye amefanikiwa
kumshawishi, mmoja wa wanasiasa makini na wakongwe, mtumishi wa umma
wa muda mrefu, mwanadiplomasia na Kanali Mstaafu wa Jeshi,
Abdulrahaman Kinana kuwa Katibu Mkuu wa CCM.
 
kwa namna nnavyoona cdm inavyowanufaisha viongozi wake, ambao wengi sasa wanatembelea magari ya kifahari na kujenga majumba ya kifahari nnaona cdm ni kama ngo au pressure group ambayo inatisha ili ile...

chadema inawanyima usingizi,mnatia huruma sana ndugu zanguni
mnatapatapa sasa,mkisubiri kuwa chama cha upinzani muda si mrefu lol!
 
Utakuwa siyo mtu kama hulifahamu hili.

Unajua kuna vitu vingine huitaji akili ya ziada kuvitambua. Mbaya zaidi hii NGO inaangalia sana watu wa ukanda fulani na wa imani fulani.
Ni bora kuficha ujinga wako,kuliko kuficha hekima
Elimu uliyonayo na comment zako haviendani,ni kitu gani hasa kinalufanya uwe
so conservative na ccm,not in this era mkuu!!
 
By golii: CHADEMA wana plan za maendeleo sio NG'Os kama unavyodai, huoni Taifa halina hata ndege zaidi ya kukodi, wakati ccmfuu wanadai wanamiliki ndege ya Rais ya kupigia misele
 
Baada ya kumaliza uchaguzi umekuja na ajenda hii ,hoja yako haina mantiki .........kesho utakuja na agenda ipi .
 
Nadhani umeshindwa kucontrol hisia kiasi ambapo hukuweza kuruhusu fikra kupata nafasi.
 
Kwa namna nnavyoona CDM inavyowanufaisha viongozi wake, ambao wengi sasa wanatembelea magari ya kifahari na kujenga majumba ya kifahari nnaona CDM ni kama NGO au pressure group ambayo inatisha ili ile...


CCM inamnufaisha nani kwani????????????????/
 
Back
Top Bottom