CHADEMA ni kiboko ya CCM

CHADEMA ni kiboko ya CCM

Hakikwanza

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2010
Posts
4,043
Reaction score
1,012
Chadema inawanyima usingizi ccm kila wakilala na kuamka wanaiwaza chadema kuliko chama chao.
Kwa miaka kadhaa sasa, nimezidi kuamini zaidi kwamba CHADEMA ni chama ambacho kimelenga kuleta mabadiliko katika nyanja ya kiutawala, kijamii, kiuchumi na kisiasa. Kifupi kimedhamiria kwa dhati bila shaka kukiangusha chama tawala cha CCM.

CCM ambayo ilizaliwa mwaka 1977, ilirithi utawala kutoka kwa kilichokuwa Chama cha TANU. Uhuru wa nchi yetu tuliupata wakati TANU kikiwa ni chama cha siasa kilichokuwa kikiongozwa na Baba wa Taifa, hayati Mwalimu Julius Nyerere.

Alipokuwa akitangaza dhamira yake ya kutaka kujiuzulu wadhifa wa urais, Nyerere ambaye ndiye Waziri Mkuu wa kwanza wa nchi yetu hii, aliwahi kusema: "Mimi nang'atuka, lakini bila CCM madhubuti nchi itayumba."

Usemi na utabiri huu wa Baba wa Taifa umeanza kujionyesha dhahiri sasa. Sote tunashuhudia jinsi nchi inavyoyumba kwa utawala tulionao huu wa CCM. Hili halina kificho wala hapaswi mtu kuvimbisha mishipa ya shingo yake kubisha ukweli wa jambo hili.

Enzi za Mwalimu hakukuwepo na utitiri wa viongozi kujilimbikiza mali. Enzi hizo ulikuwepo uwajibikaji wa dhati baina ya viongozi kwa wananchi wake. Dhuluma na uporaji wa haki za wanyonge ulikuwa mwiko. Lakini leo hii tunashuhudia maajabu.

CCM ya Mwalimu Nyerere si sawa na hii ya leo ya akina Rais Jakaya Kikwete, Nape Nnauye, Abdulrahman Kinana, Philip Mangula, Mwigulu Nchemba, Juma Nkamia anayetukana wabunge wenzake bungeni, imekosa mwelekeo. Ndivyo ilivyo.

Ndani ya CCM kumeibuka mambo mazito ya kudharauliana na kupuuziana wao kwa wao. Imeonekana hawaaminiani tena. Huyu akisema hiki, mwingine anasema hivi. Yaani ni vurugu tupu.
Chadema mwendo mdundo .
 
Chadema inawanyima usingizi ccm kila wakilala na kuamka wanaiwaza chadema kuliko chama chao. Chadema mwendo mdundo .
Ilitakiwa uandike ACT inawanyima usingizi chadema, kila wakilala wanaiwaza ACT kuliko saccos yao. ACT mwendo mdundo
 
Kamanda unaweza kunipa matokea ya Kelenga na Chalinze kuna mtu kaniomba mimi sina.
 
Narudia tena, asubuhi tuwe tunakunywa chai au uji!! Haya ndio madhara ya viroba na gongo.
 
Ilitakiwa uandike ACT inawanyima usingizi chadema, kila wakilala wanaiwaza ACT kuliko saccos yao. ACT mwendo mdundo

ACT NININI? Chama chenye umaarufu mitandaoni. Nenda kwa watu wakawaida uliza ACT ninini upate jibu, wengi watakurekebisha watakuambia ni AICT (Africa Inland Church of Tanzania). Kaa na ACT yako chama ambacho hata makao makuu yake hayajulikani ni wapi kigoma au Dar
 
Ilitakiwa uandike ACT inawanyima usingizi chadema, kila wakilala wanaiwaza ACT kuliko saccos yao. ACT mwendo mdundo

ACT ni branch ya CCM iliyoundwa kwa makusudi ya kishetani ili kuidhoofisha cdm, ila chadema ni kisiki cha mpingo na itazidi kusonga mbele
 
Kamanda unaweza kunipa matokea ya Kelenga na Chalinze kuna mtu kaniomba mimi sina.

CCM ilishinda kwa kuwanunua wananchi kwa kutumia pesa inazoziiba serikalini.
 
Narudia tena, asubuhi tuwe tunakunywa chai au uji!! Haya ndio madhara ya viroba na gongo.

CCM asubuhi na mapema mna bwia unga na kuvuta bhangi ndio maana ni wezi wa fedha za umma. Yaani ni mateja.
 
Ilitakiwa uandike ACT inawanyima usingizi chadema, kila wakilala wanaiwaza ACT kuliko saccos yao. ACT mwendo mdundo

wewe mwizi wa simu bungeni...hapa unataka kutuaminisha kuwa na wewe ni ACT? au unaunga mkono tawi lenu....
 
CCM ni chama kilichokosa dira hapa duniani hata Marehemu Kolimba aliona hilo. CCM ipo kwa sababu ya usalama wa taifa na majeshi ndio wanaoibeba
 
Ilitakiwa uandike ACT inawanyima usingizi chadema, kila wakilala wanaiwaza ACT kuliko saccos yao. ACT mwendo mdundo

CCM imekosa mbinu hadi imeamua kuanzisha tawi liitwalo act lakini nalo linaelekea kufa,wananchi hawalitaki kwani linaonekana ni kusanyiko la wahuni wasio na dira wala mwelekeo.Hivi ccm wamekosa akili kiasi cha kuwaamini Mchange na wapuuzi wenzake na kuwapa mafweza kwa imani ya kuua cdm? CDM kwa sasa ni chama cha watz wote na kimeenea kila kona ya taifa hili,watu wanakipenda,wamekiamini na ndilo tumaini lao pekee katka kukabiliana na dhuruma,uonevu na kila aina ya uovu wa ccm.
 
Kamanda unaweza kunipa matokea ya Kelenga na Chalinze kuna mtu kaniomba mimi sina.

Unaweza kuniambia kwa nini wapiga kura wanakuwa chini ya nusu ya watu walioandikishwa kwenye daftari? Unajisifu kwa huu ushindi wa hujuma? Ushindi katika tume hii ya uchaguzi? Ushindi katika mazingira yasiyotoa fursa ya watu wenye sifa ya kupiga kura kuandikishwa katika daftari? Kwa nini huongelei matokeo ya chaguzi za mitaa na vijiji yaliyotoa fursa za watu kuandikishwa kama sheria ya chaguzi za serikali za mitaa inavyosema? Tulifanya chaguzi za marudio za serikali za mitaa huku kwetu,je unajua aibu iliyoipata ccm?
 
Back
Top Bottom