Chadema nao kufanya mkutano arusha sambamba na cuf

mpinga shetani

JF-Expert Member
Nov 22, 2010
3,236
954
Naona leo hapa Arusha hapatatosha.
Gari la matangazo ya Chadema linasikika likiwaita watu kwenye mkutano huku lile la CUf likifanya vivyo hivyo. Mh!
 
sijui kwa nini Chadema wanawahofia Cuf, ni vema wangewaacha ili wananchi wajue upi mchele na zipi pumba.!
 
lema anajua watu wamechoka na siasa za maandamano na mabomu watu wakifa wanatoa ubani laki 5
 
Hili jukwaa lina Mazuzu wengi sana, watu mnaibuka kuchangia bila kutafakari, Nipo Arusha hakuna Kitu Kama hicho CHADEMA hawana mkutano wowote Arusha Mjini, ila Cha ajabu naona watu wamekazana Kupondea tu kwa habari wasio kuwa na uhakika nayo,
 
Una Uhakika kuna mkutano wa CDM? Au unafikilia tu kwa kutumia Masaburi yako

Mpendwa lugha njema ndiyo utu wako, tutakupima kwa maneno yako, inawezekana amekosea lkn matusi si maugwana, hili ni jamvi la kuelezana kiungwana ili watu waelimike, tutumie vema midomo yetu na fikra zetu kwani Mungu atauhukumu kwa hizo.
Na pia uongo katika kuchangia hauna maana km huna uhakika acha lipite siyo lazma kila topic uchange, jamani kuna watu wenye hikma zao wanaliangalia jamvi hili kama dira ya elimu kwa wote.
Regards.
 
Cuf bwana! Niko barabara kuu arusha to moshi naona turbo toyata limejaza wanachama wa cuf kutoka nje ya arusha hili kupamba mkutano wao,jaman mkutano wa cuf arusha ni kwaajili ya wananchi wa arusha au ni mkutano wa kitaifa kupitia wananchi wa arusha?
 
Hebu ongeeni kitu cha kueleweka!!kuna mkutano wa chadema?au hakuna?sio mnaanza kushambuliana kama wanawake wambea.
 
Na kama chadema wanamkutano utafanyka wap na ni saa ngapi?.Watu mlioko arusha embu tupeni ukweli halisi!
 
Mmhh!! kama ni kweli basi kazi ipo!!! Tuombe iwe kheri, lakini pamoja na kuwa sipo huko, bado napata wasiwasi.
 
Na kama chadema wanamkutano utafanyka wap na ni saa ngapi?.Watu mlioko arusha embu tupeni ukweli halisi!

Mkutano wa Chadema ulifanyika jana maeneo ya Mwanama kata ya Olorien. Mida ya saa 11:43 msafara wa Lema Godbless ndo uliingia.
 
mkutano wa chadema arusha upo unafanyika sombetini. atakuwepo lema, lissu na nassari
 
Mtu kama hujui kinachoendelea yanini kujionyesha unajua tena mpaka unatukana jiangalieni vijana
 
Hili jukwaa lina Mazuzu wengi sana, watu mnaibuka kuchangia bila kutafakari, Nipo Arusha hakuna Kitu Kama hicho CHADEMA hawana mkutano wowote Arusha Mjini, ila Cha ajabu naona watu wamekazana Kupondea tu kwa habari wasio kuwa na uhakika nayo,

Ulikua na wajibu wa kueleza ukweli kama mkazi wa arusha, sio kuwaita wanabodi mazuzu. Umeonyesha jinsi ulivyo zuzu kwa kushindwa kutambua wajibu wako kama mwanajf.!
 
Back
Top Bottom