CHADEMA na Zitto watafuta suluhu

hugochavez

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2013
Posts
1,907
Reaction score
1,009
imeripotiwa katika magazeti ya leo kwamba chadema imemwangukia mbunge wa kigoma kaskazini zitto kabwe na kutaka kusuluhishana na kumaliza tofauti zao na hatimaye kurudi kukijenga chadema kuelekea uchaguzi mkuu wa dola 2015.

Nini tafsiri na mantiki ya hatua hiyo muhimu ya chadema baada ya kukamisha uchaguzi wa ndani ya chama bila Zitto kisha kumwangukia?? Je, ni dhamira ya dhati au ni kumhadaa na kumkejeli kumpima kama yuko imara??

 
propaganda tu nani atake maiti irudi duniani si atakuwa msukule hata azikili ameshapoteza tena nafasi yake ya kitaifa kisiasa na kuaminika na wananchi wewe uliyemdanganya kwa milioni mia mbili na vidola vya ujerumani upo wizarani unatamba naibu waziri mpuuzi shetani uliyesimama
 

Hujaekeweka jitahidi kudadavua,jiongeze ueleweke
 

mku umeifanya siku yangu leo iwe ya kipekee sana. Hakika zitto ni m@iti!
 
Ni kituko na kichekesho Zitto kutumia magazeti ya washirika zake CCM kujaribu kuomba msamaha Chadema.Hiki ni kituko cha mwaka.

Kama Zitto anataka kuomba msamaha asimame mbele ya Watanzania atubu madhambi yake na hila zake za kutaka kuua upinzani Tanzania.

Ni mwendawazimu pekee atakayeamini uchafu huu wa Zitto alioupenyeza kwenye gazeti la CCM eti tunataka suluhu naye! Ebo..Tutake suluhu na mhujumu mageuzi Tanzania?

Mkutano mkuu wa Chadema uliofanyika wiki iliyopita na kumrudisha kwa kishindo madarakani Freeman Mbowe umewaumbua makuwadi wote wa kisiasa Tanzania na kuwaacha wameficha nyuso zao kwa aibu.

Just Imagine mkutano mkuu uliohudhiriwa na mabalozi wa mataifa ya kigeni zaidi ya 19!

Namshauri Zitto aende akauze dagaa kama biashara ya siasa imemshinda kuliko kutapatapa na vijarida vya CCM.
 
Last edited by a moderator:
Waandishi wa 10 milion kuweka picha kuelekea 2015
 
Kiukweli kama Chadema inataka kuporomoka na kupotea kisiasa basi imrudishe Zitto, Kila Aliye mwanachama anajua Habari za Usaliti wa Zitto kwa ushahidi wa Chama cha ACT kinachosimamiwa na watu wa Karibu wa Zitto, Mwagamba, Mkumbo, Mchange nk

Njia pekee ya Zitto Kurudi Chadema ni yeye Zitto Kuomba Radhi kwa Wana Chadema kuwa alitereza, lakini sio kwa viongozi kwenda kumbembeleza.
 
Asante kwa kuthibitisha kile kilichoandikwa kwenye gazeti, kwamba mnataka ZITTO AFANYE KAMA INAVYOONEKANA KWENYE RED
 
huyu ambaye siku hizi anaitwa mfalme mbowe??
 
Unapaswa kujua Chadema sio mtu, ni taasisi. Na kwa jinsi suala lenyewe lilivyo aliyetakiwa kuangukiwa ni chama sio Zitto kwani yeye ndiye mkosaji, kasaliti chama.
Pengine Zitto ameanza mipango ya kutaka kuomba radhi kwa hiyo anazusha haya ili ikitokea akaomba radhi ili arudishwe kwenye chama ionekane aliangukiwa.
Chadema kama taasisi haiko tayari kumwangukia yoyote zaidi ya kutekeleza majukumu yake ya kikatiba likiwemo suala la kuwatimua wanaoenda kinyume.
Kwa kifupi, labda uwe na ubongo wa mende ndo utaamini uzushi huu wa habari Za kubumba ili kujaribu kuiondoa Chadema katika harakati Za kupambana na uhuni unaofanywa kwenye mchakato wa Katiba Mpya.
Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…