Wakati umefika tuache UNAFIKI.
Ebu fikiri, Tundu Lissu alipigwa risasi kwa sababu tu alikuwa anatetea haki. Leo yupo mahabusu kwa kubambikwa kesi ya uhaini kwa sababu tu ya kutetea Haki.
Ikiwa Tundu Lissu alimwaga damu yake kwa kutetea Haki, kwa nini sisi tunaogopa kujitoa sadaka damu zetu zimwagike ili kutetea Haki ya Lissu na ya Watanzania kwa ujumla?
Mimi niombe sana, kama kweli tupo serious, na kwamba tunatakiwa kudai Haki, tujitoe sadaka. Sina maana tuchukue silaha kupambana na dola ili kudai Haki, namaanisha kwamba tukae mstari wa mbele kabisa kudai Haki kwa vitendo. Kama vyombo vya dola vitataka kutupiga au kutuumiza hilo ni lao lakini sisi tusiogope kuumizwa.
Inashangaza sana, mtu amepigwa risasi na amemwaga damu, sisi tunaogopa nini?
Damu zetu ni za thamani kubwa zaidi damu ya Lissu?
Ebu tuchukue hatua madhubuti zinazoumiza, siyo kupiga kelele tu.
Ebu fikiri, Tundu Lissu alipigwa risasi kwa sababu tu alikuwa anatetea haki. Leo yupo mahabusu kwa kubambikwa kesi ya uhaini kwa sababu tu ya kutetea Haki.
Ikiwa Tundu Lissu alimwaga damu yake kwa kutetea Haki, kwa nini sisi tunaogopa kujitoa sadaka damu zetu zimwagike ili kutetea Haki ya Lissu na ya Watanzania kwa ujumla?
Mimi niombe sana, kama kweli tupo serious, na kwamba tunatakiwa kudai Haki, tujitoe sadaka. Sina maana tuchukue silaha kupambana na dola ili kudai Haki, namaanisha kwamba tukae mstari wa mbele kabisa kudai Haki kwa vitendo. Kama vyombo vya dola vitataka kutupiga au kutuumiza hilo ni lao lakini sisi tusiogope kuumizwa.
Inashangaza sana, mtu amepigwa risasi na amemwaga damu, sisi tunaogopa nini?
Damu zetu ni za thamani kubwa zaidi damu ya Lissu?
Ebu tuchukue hatua madhubuti zinazoumiza, siyo kupiga kelele tu.