Mkwawa
JF-Expert Member
- Jun 8, 2011
- 1,334
- 1,464
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CDM) kimekuwa kikitoa kilio chake cha kupinga posho mbali mbali zinazolipwa na serikali au mashirika ya umma pamoja na wanasiasa kwa ajili ya vikao vya kikazi. CDM wanaona kuwa ni wajibu wa mfanyakazi kufanya kazi aliyoajiriwa nayo bila kulipwa posho ya kufanya kazi hiyo. CDM wamejikita kwenye hoja kwamba kama inaonekana kazi haendani na kipato ni wakati wa kuangalia mishahara ili iendane na kazi husika badala ya kakundi kadogo kujilipa fedha nyingi kwa kisingizio cha posho na kusahau kundi kubwa la wavuja jasho bila posho za kujikimu kama waalimu, madaktari, polisi, wanajeshi, manesi, wakulima, wafanyakazi nk.
Je kilio hiki ni cha CDM pekee, je kilio hiki ni cha wanasiasa? yako wapi makundi yanayoathirika? wako wapi waalimu? wako wapi wanajeshi na polisi? wako wapi wakulima na wanafunzi?
Wabunge wa CDM wakiwa wanauwezo wa kukaa kimya na kula posho zao ambazo zinapanda kila kukicha na vikao vingi vinavyopangwa na bunge kwa ajili ya kulipana posho, wao walau wameamua kutuonyesha jinsi watetezi wetu walivyoamua kutusahau na kugawana keki ya nchi wenyewe.
Imefika wakati kwa kila mpiga kura kutathimini kama hii ndio kazi ya mbunge wake na bunge kwa ujumla. Kazi kubwa ya Mbunge ni kuonisha mahitaji ya wananchi wa sehemu husika na kuyapeleka bungeni na kutetea maslahi yakinifu kutokana na uchumi uliopo na vyanzo vyake. Je kujilipa miposho bila uwiano hilo ndilo lengo? kweli wanatukumbuka? Kwa nini hatusikii wakisema inabidi mwalimu alipwe posho ya kujikimu anapoingia darasani? Kwa nini daktari asilipwe posho ya kujikimu anapotibu mgonjwa. Kweli bado tunahitaji bunge na hawa wabunge tulionao??
Hii vita isiwe ni vita ya wabunge 48 wa CDM na viongozi wao dhidi ya uongozi mbovu wa serikali na bunge isiwe vita ya wachahe ni vita yangu ni vita yako ni vita yetu. Tuamke tupiganie haki zetu, kodi zetu ni mali zetu sote tunawajibu nazo sio kajikundi ka wapumbavu wachache wanaofikiri wao ndio wanahitaji pumzi kuliko sisi.
Watanzania hakuna mwanasiasa anayetupenda wala kutujali kama sisi wenyewe hatujijui, wakati umefika kujua majukumu ya serikali na bunge kwetu. Tunaweza kuwawajibisha tukiungana. Hakuna sababu ya kutengana kwa hili, tuache uvyama hautusadii wote tunaibiwa bila kujali itikadi zetu. Wote tunanyanyaswa na kadi za vyama vyetu mifukoni. Wote tunauwawa na umasikini wetu huku tukiwapeperushia bendera.
Lets say No to POSHO.
Je kilio hiki ni cha CDM pekee, je kilio hiki ni cha wanasiasa? yako wapi makundi yanayoathirika? wako wapi waalimu? wako wapi wanajeshi na polisi? wako wapi wakulima na wanafunzi?
Wabunge wa CDM wakiwa wanauwezo wa kukaa kimya na kula posho zao ambazo zinapanda kila kukicha na vikao vingi vinavyopangwa na bunge kwa ajili ya kulipana posho, wao walau wameamua kutuonyesha jinsi watetezi wetu walivyoamua kutusahau na kugawana keki ya nchi wenyewe.
Imefika wakati kwa kila mpiga kura kutathimini kama hii ndio kazi ya mbunge wake na bunge kwa ujumla. Kazi kubwa ya Mbunge ni kuonisha mahitaji ya wananchi wa sehemu husika na kuyapeleka bungeni na kutetea maslahi yakinifu kutokana na uchumi uliopo na vyanzo vyake. Je kujilipa miposho bila uwiano hilo ndilo lengo? kweli wanatukumbuka? Kwa nini hatusikii wakisema inabidi mwalimu alipwe posho ya kujikimu anapoingia darasani? Kwa nini daktari asilipwe posho ya kujikimu anapotibu mgonjwa. Kweli bado tunahitaji bunge na hawa wabunge tulionao??
Hii vita isiwe ni vita ya wabunge 48 wa CDM na viongozi wao dhidi ya uongozi mbovu wa serikali na bunge isiwe vita ya wachahe ni vita yangu ni vita yako ni vita yetu. Tuamke tupiganie haki zetu, kodi zetu ni mali zetu sote tunawajibu nazo sio kajikundi ka wapumbavu wachache wanaofikiri wao ndio wanahitaji pumzi kuliko sisi.
Watanzania hakuna mwanasiasa anayetupenda wala kutujali kama sisi wenyewe hatujijui, wakati umefika kujua majukumu ya serikali na bunge kwetu. Tunaweza kuwawajibisha tukiungana. Hakuna sababu ya kutengana kwa hili, tuache uvyama hautusadii wote tunaibiwa bila kujali itikadi zetu. Wote tunanyanyaswa na kadi za vyama vyetu mifukoni. Wote tunauwawa na umasikini wetu huku tukiwapeperushia bendera.
Lets say No to POSHO.