MAFILILI
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 2,377
- 1,200
[h=2] Meya ampongeza Mgeja kwa kuiponda Chadema [/h] umanne, Aprili 30, 2013 06:30 Na Mwandishi Wetu, Mwanza
MEYA wa Manispaa ya Ilemela, Henry Matata, ameibuka na kumpongeza Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, kwa kuponda Baraza la Mawaziri litakaloundwa na Serikali ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Aidha, baadhi ya wanachama na wafuasi wa chama hicho wameonyesha kukerwa na uteuzi huo na wameeleza hiyo ni dharau kwa watu wengine na inaonyesha nje ya wabunge hao hakuna mtu wa kushika wadhifa huo kama ambavyo Mbunge wa Nyagamana, Ezekia Wenje, anatavyotaka umma uamini hivyo.
Akizungumza na MTANZANIA jana kuhusu baraza hilo, Matata, alisema huo ni ubakaji wa demokrasia ndani ya chama.
Alisema Wenje hana uwezo wa kutangaza baraza la mawaziri, bali mwenye dhamana hiyo ni rais pekee anayeweza kufanya hivyo.
Mimi ni mwanachama wa Chadema, kuwa Meya nimepelekwa na katibu wa wilaya kwa barua iliyonitambulisha kuwa ni mgombea wa chama. Siwezi kusema siko Chadema ukiachana na mambo ya Mahakama. Namshangaa Wenje, katangaza baraza la mawaziri wa Mwanza au wa Tanzania. Anawezaje kutangaza baraza la mawaziri wakati mwenye dhamana hiyo ni rais. Anawavika kilemba cha ukoka wabunge hao, alisema Matata.
Alisema watu wenye busara wanamwona mbunge huyo hana akili kwa madai kuwa Chadema inaweza kushika dola, endapo tu itaachana na mtindo wa kufukuza wanachama wake kwa kisingizio cha usaliti na fitina zinazofanywa na baadhi ya watu kwa chuki binafsi.
Alisema fitina zao za kuwachukia wanachama kuwa wasaliti na kuvurugana, itawawia vigumu kushika dola kama anavyodhani Wenje kwamba hawawezi kushika dola hadi washikamane na akatoa pongezi kwa Mgeja kuwa anaona mbali kutokana na ujasiri wake wa kuponda baraza hilo.
Huwezi kupata dola kama hamna mshikamano, Chadema wanapaswa kujenga hoja ili wananchi wenye busara wawaelewe, si kwa maandamano, vurugu ama kufitiniana na kuvurugana. Lazima viongozi wawe na busara ya kushawishi wananchi na hao wachache walionao wasiwafukuze ili washinde na kupata dola, alisema Matata.
Mwanachama mwingnie wa Chadema aliyejitambulisha kwa jina moja la Lucy, alisema kitendo cha Wenje kutaja majina ya wabunge wa kuunda baraza la mawaziri ni kupora uhuru wa wanachama na kubaka demokrasia na madaraka.
Tunalalamika CCM wanabebana na kulindana, wanapeana vyeo kumbe hata sisi viongozi wetu wanataka tuamini wabunge waliotajwa ndiyo wanafaa kuwa mawaziri, nje ya hao hakuna mwanachama anayefaa kuwa rais ama waziri. Huko ni kubaka na kuminya demokrasia, alisema Lucy.
Mwingine alijitambulisha kwa jina moja la Lutaigulwa, alisema kuna udikteta ndani ya Chadema na ndiyo maana Wenje kwa udikteta huo alimua kupanga safu hata kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015.
Alisema kupangwa kwa safu hiyo ya mawaziri, kumeonyesha dhamira ya wazi na ya dhati kuwa viongozi nia yao ni madaraka na si kuwatetea Watanzania.
Baraza hilo la Wenje limewachefua na kuwagawa Chadema na kusababisha baadhi ya wafuasi na wanachama wake kumpongeza Mgeja kuwa ni jasiri, baada ya kuliponda hadharani kuwa halina mashiko na viongozi wake wanabaka na kuminya demokrasia.
Mgeja alisema Dk. Slaa kutajwa kwake kuwa mgombea urais, ni kuminya demokrasia na uhuru wa wanachama.
MEYA wa Manispaa ya Ilemela, Henry Matata, ameibuka na kumpongeza Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, kwa kuponda Baraza la Mawaziri litakaloundwa na Serikali ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Aidha, baadhi ya wanachama na wafuasi wa chama hicho wameonyesha kukerwa na uteuzi huo na wameeleza hiyo ni dharau kwa watu wengine na inaonyesha nje ya wabunge hao hakuna mtu wa kushika wadhifa huo kama ambavyo Mbunge wa Nyagamana, Ezekia Wenje, anatavyotaka umma uamini hivyo.
Akizungumza na MTANZANIA jana kuhusu baraza hilo, Matata, alisema huo ni ubakaji wa demokrasia ndani ya chama.
Alisema Wenje hana uwezo wa kutangaza baraza la mawaziri, bali mwenye dhamana hiyo ni rais pekee anayeweza kufanya hivyo.
Mimi ni mwanachama wa Chadema, kuwa Meya nimepelekwa na katibu wa wilaya kwa barua iliyonitambulisha kuwa ni mgombea wa chama. Siwezi kusema siko Chadema ukiachana na mambo ya Mahakama. Namshangaa Wenje, katangaza baraza la mawaziri wa Mwanza au wa Tanzania. Anawezaje kutangaza baraza la mawaziri wakati mwenye dhamana hiyo ni rais. Anawavika kilemba cha ukoka wabunge hao, alisema Matata.
Alisema watu wenye busara wanamwona mbunge huyo hana akili kwa madai kuwa Chadema inaweza kushika dola, endapo tu itaachana na mtindo wa kufukuza wanachama wake kwa kisingizio cha usaliti na fitina zinazofanywa na baadhi ya watu kwa chuki binafsi.
Alisema fitina zao za kuwachukia wanachama kuwa wasaliti na kuvurugana, itawawia vigumu kushika dola kama anavyodhani Wenje kwamba hawawezi kushika dola hadi washikamane na akatoa pongezi kwa Mgeja kuwa anaona mbali kutokana na ujasiri wake wa kuponda baraza hilo.
Huwezi kupata dola kama hamna mshikamano, Chadema wanapaswa kujenga hoja ili wananchi wenye busara wawaelewe, si kwa maandamano, vurugu ama kufitiniana na kuvurugana. Lazima viongozi wawe na busara ya kushawishi wananchi na hao wachache walionao wasiwafukuze ili washinde na kupata dola, alisema Matata.
Mwanachama mwingnie wa Chadema aliyejitambulisha kwa jina moja la Lucy, alisema kitendo cha Wenje kutaja majina ya wabunge wa kuunda baraza la mawaziri ni kupora uhuru wa wanachama na kubaka demokrasia na madaraka.
Tunalalamika CCM wanabebana na kulindana, wanapeana vyeo kumbe hata sisi viongozi wetu wanataka tuamini wabunge waliotajwa ndiyo wanafaa kuwa mawaziri, nje ya hao hakuna mwanachama anayefaa kuwa rais ama waziri. Huko ni kubaka na kuminya demokrasia, alisema Lucy.
Mwingine alijitambulisha kwa jina moja la Lutaigulwa, alisema kuna udikteta ndani ya Chadema na ndiyo maana Wenje kwa udikteta huo alimua kupanga safu hata kabla ya uchaguzi wa mwaka 2015.
Alisema kupangwa kwa safu hiyo ya mawaziri, kumeonyesha dhamira ya wazi na ya dhati kuwa viongozi nia yao ni madaraka na si kuwatetea Watanzania.
Baraza hilo la Wenje limewachefua na kuwagawa Chadema na kusababisha baadhi ya wafuasi na wanachama wake kumpongeza Mgeja kuwa ni jasiri, baada ya kuliponda hadharani kuwa halina mashiko na viongozi wake wanabaka na kuminya demokrasia.
Mgeja alisema Dk. Slaa kutajwa kwake kuwa mgombea urais, ni kuminya demokrasia na uhuru wa wanachama.