Kabisa mkuu CUF yatosha, ninani asiejua kuwa kusini tokea mfumo Wa vyama vingi uasisiwe kuwa hiyo ni ngome imara ya CUF!!!!??
Ni hujuma za CCM na tume yake ya uchaguzi tu ndio inayoifanya CUF isifanye vizuri lakini kama tungekuwa na chaguzi huru na haki basi hakuna ubishi kusini ingekuwa Pemba ya Tanzania bara!!! Sasa kwa chadema kulazimisha lazima wagombee kusini ni moja wapo iliyoufanya UKAWA isifanye vizuri sana.
Kwisha kwa uchaguzi ndio mwanzo wa uchaguzi ni wakati mzuri Wa UKAWA kukaa chini na kujitathmini na kujua wapi walikosea na wapi walipatia!! Halafu wapange mkakati wa mambo yaliyotokea segerea kwa mtatiro hayajirudii tena kwa kila chama kuheshimu makubaliano yaliyofikiwa na UKAWA.
Si busara kutoyaheshimu maamuzi mliojiwekea ya ujumla kwa baadhi ya vyama kujiona bora zaidi ya wengine, hili limetugharimu sana uchaguzi huu uliopita.