Jenerali Ulimwengu ana kadi ya CCM ni mwanaCCM asilia ingawa ni mkosoaji mzuri wa sera za chama chake.
Kununua mapandikizi kwa maneno matamu ya mdomoni kunaweza kuingiza mamluki chadema.
Kama anaona CCM hakufai pamoja na sera zake anang'ang'ania nini huko?
Nani kakwambia CCM haifai kisera au kiitikadi? CCM ina itikadi nzuri na sera nzuri tu ila utekelezaji ni taabu kwa sababu ya maslahi binafsi kushika usukani kwenye kuendesha CCM. ndiyo maana watu kama Ulimwengu wapo wanakosoa ndani kwa ndani huku wakiwa na moyo kwamba CCM haina mbadala na mapambano yao ya kuielimisha CCM na kuuelimisha umma yataifanya CCM ifuate tena misingi yake.. Kazi ya ulimwengu haitaji kuwa kiongozi au mshauri wa chama chochote yeye kama mwanandishi na mwanaharakati anasema anachokiona na jamii inajifunza na kuamua mustakabali wa nchi..kadi yake ya kijani haikuhusu.