CHADEMA mtumieni Jenerali Ulimwengu

CHADEMA mtumieni Jenerali Ulimwengu

akelu kungisi

Senior Member
Joined
Apr 2, 2012
Posts
115
Reaction score
20
Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikiujiuliza swali hili " Hivi serikali ya ccm kwa nini imeshindwa kumtumia huyu gwiji wa habari na mambo mengi ya kiutawala, uchumi, siasa na uongozi? "
Kwa hakika Jenerali Ulimwengu ni mtu wa aina yake! Ukisoma CV yake na mambo yake unaweza kugundua kuwa is a gifted person. Na hata anapotoa ushauri wake, maranyingi unakuwa mzito mno, wenye maono ya mbali yaliyojaa hekima na busara.
Kinachonishangaza ni pale serikali inapomuona kuwa ni "threat"! Hii inanishangaza sana! ( Rejea sakata la kunyang'anywa uraia na Mr Clean). Maranyingi amekuwa akitoa ushauri kwa maandiko yake katika vitabu, magazeti, vijarida , midahalo ya wazi na kwenye vituo mbalimbali vya runinga! Ninafahamu wazi kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa akiandika sana makala zake katika gazeti la RAI enzi hizo likimilikiwa Jenerali Ulimwengu.
Ninadhani kwamba huu ni wakati muafaka kwa CHADEMA kuitumia hii hazina ambayo jioni yake inakaribia mno! CCM siku zote hawapendi mtu anayesema ukweli na kuwakosoa kwa makosa ya waziwazi mfano wa ujambazi wa KAGODA, MEREMETA, RICHMOND, na ushenzi mwingi amabao hausemeki.
Jenerali Ulimwengu ni muwazi daima, anaitumia elimu yake kuyaainisha matatizo yaliyopo na kuyatolea majawabu pamoja na kuielimisha jamii ya Watanzania kuhusu elimu ya uraia.
Ninadhani CHADEMA huu ungekuwa wakati muafaka kumuomba huyu mzee awe mmoja wa washauri wenu katika chama.
Nafahamu pia ninyi wakuu wa CHADEMA huwa mnachungulia humu JF, naomba yachukueni mawazo yangu kwa uzito unaostahili!
 
Mkuu hiki ni kibaraza cha ma "great thinkers", ukiwa hauna hoja nyamaza! Habari za supu na chai ni utoto usiopimika!
 
Mkuu hiki ni kibaraza cha ma "great thinkers", ukiwa hauna hoja nyamaza! Habari za supu na chai ni utoto usiopimika!

kwani hapo kosa lake nini? kwanza kakujulia hali akaenda mbali zaidi kufaham afya yako kwa kuuliza kama umepata kifungua kinywa.. sasa wewe povu limekutoka kweli
 
Nilishawahi kusema kuwa kuwa kuna watu wanavamia jukwaa la siasa wakati siyo saizi yao hata kidogo. Pelekeni masihara yenu ya UMEKUNYWA SUPU huko jukwaa yenu la MMU,acha kuvamia majukwaa ya watu wenye akili
 
Jenerali Ulimwengu ana kadi ya CCM ni mwanaCCM asilia ingawa ni mkosoaji mzuri wa sera za chama chake.

Kununua mapandikizi kwa maneno matamu ya mdomoni kunaweza kuingiza mamluki chadema.

Kama anaona CCM hakufai pamoja na sera zake anang'ang'ania nini huko?
 
hili ni wazo na ushauri mzuri.kama chadema wana nia ya dhati ya kumkomboa mtazania na 'uhuni' wa ccm na serikali yake hawana budi kutumia hekima na busara za wazee kama ulimwengu.umeelezea vema huyu mtu ni hazina kubwa ambayo inaelekea ukingoni bila kuwa utilized vizuri kwa manufaa ya taifa kwa sasa na for the coming generations.ni mkweli asiye na chembe ya unafiki si mchumia tumbo ana uwezo mkubwa sana wa kufikiri na kuchambua mambo,ana maono ya mbali.tuna bahati kuwa na mtu kama huyu lakini tunakuwa 'wapumbavu' kwa kutotumia busara zake kwenye mambo mengi yanayolisumbua taifa hili
 
Naamini ukosahihi mimi namheshimusana huyujamaa anahekima na akiwamshauli wa chadema vemasana.TATIZO LA WATANZANIA HATUPENDI KUSHAULIWA SISI HUJIFANYA TUNAJUA KILAKITU.WAULIZE WATUMAALUFU KAMA AKINA ZITTO,MNYIKA MBOWE,LISSU,JANUARI,NK. KAMAWANAWASHAURI
 
Naamini ukosahihi mimi namheshimusana huyujamaa anahekima na akiwamshauli wa chadema vemasana.TATIZO LA WATANZANIA HATUPENDI KUSHAULIWA SISI HUJIFANYA TUNAJUA KILAKITU.WAULIZE WATUMAALUFU KAMA AKINA ZITTO,MNYIKA MBOWE,LISSU,JANUARI,NK. KAMAWANAWASHAURI
Naona unamwongerea Jenelari Urimwengu wa Lai, Mtumaalufu kweri kweri!
 
Jenerali Twaha Ulimwengu ni ccm asilia [ccm ya Kambarage sio ya hawa mafisadi] ambaye pia ni mzalendo ambae maandiko yake yanaonesha kuwa anaweka Utaifa mbele kuliko chama!!! Kumshauri mtu sio lazima muwe chama kimoja; bila shaka pale British Legion wanapokuwa wanapata kinywaji huwa wanashauriana na wakina Mbowe informally katika mazungumzo!!
 
kwani hapo kosa lake nini? kwanza kakujulia hali akaenda mbali zaidi kufaham afya yako kwa kuuliza kama umepata kifungua kinywa.. sasa wewe povu limekutoka kweli

Kwa hiyo wewe ulikuwa unaona kulikuwa na haja ya kujua kama amepata kifungua kinywa? Ili itusaidie nn? Halafu bila aibu unaunga mkono upuuzi!!
It was an act of total absurdity kuleta mizaha kwenye mijadala ya msingi,kuchangia sio lazima unaweza kukaa kimya au nenda Facebook!!
 
mtu yeyote safi hawezi kuwa ccm.
ukiona yupo ccm bado ni kwaajili ya kutoa siri za uchafu unaotendeka ndani au anataka kuwa wa mwisho baada ya katiba mpya.
 
Kumbuka alishawahi kuwa katika system huko nyuma na kuna maamuzi ya hovyo aliwahi kuyafanya akiwa kiongozi wa serikali. Ndiyo wale wale tu wakipewa ulaji... kidumu sana tu... lakini wakinyang'anywa wanajifanya wakosoaji ha ha ha!
 
hili ni wazo na ushauri mzuri.kama chadema wana nia ya dhati ya kumkomboa mtazania na 'uhuni' wa ccm na serikali yake hawana budi kutumia hekima na busara za wazee kama ulimwengu.umeelezea vema huyu mtu ni hazina kubwa ambayo inaelekea ukingoni bila kuwa utilized vizuri kwa manufaa ya taifa kwa sasa na for the coming generations.ni mkweli asiye na chembe ya unafiki si mchumia tumbo ana uwezo mkubwa sana wa kufikiri na kuchambua mambo,ana maono ya mbali.tuna bahati kuwa na mtu kama huyu lakini tunakuwa 'wapumbavu' kwa kutotumia busara zake kwenye mambo mengi yanayolisumbua taifa hili

Kwenye M4C Mheshimiwa Mbowe aliwaeleza watu sampuli ya kama Jenerali kuwa..Sie tunatangulia mtatukuta mbele ya safari
 
Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikiujiuliza swali hili " Hivi serikali ya ccm kwa nini imeshindwa kumtumia huyu gwiji wa habari na mambo mengi ya kiutawala, uchumi, siasa na uongozi? "
Kwa hakika Jenerali Ulimwengu ni mtu wa aina yake! Ukisoma CV yake na mambo yake unaweza kugundua kuwa is a gifted person. Na hata anapotoa ushauri wake, maranyingi unakuwa mzito mno, wenye maono ya mbali yaliyojaa hekima na busara.
Kinachonishangaza ni pale serikali inapomuona kuwa ni "threat"! Hii inanishangaza sana! ( Rejea sakata la kunyang'anywa uraia na Mr Clean). Maranyingi amekuwa akitoa ushauri kwa maandiko yake katika vitabu, magazeti, vijarida , midahalo ya wazi na kwenye vituo mbalimbali vya runinga! Ninafahamu wazi kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa akiandika sana makala zake katika gazeti la RAI enzi hizo likimilikiwa Jenerali Ulimwengu.
Ninadhani kwamba huu ni wakati muafaka kwa CHADEMA kuitumia hii hazina ambayo jioni yake inakaribia mno! CCM siku zote hawapendi mtu anayesema ukweli na kuwakosoa kwa makosa ya waziwazi mfano wa ujambazi wa KAGODA, MEREMETA, RICHMOND, na ushenzi mwingi amabao hausemeki.
Jenerali Ulimwengu ni muwazi daima, anaitumia elimu yake kuyaainisha matatizo yaliyopo na kuyatolea majawabu pamoja na kuielimisha jamii ya Watanzania kuhusu elimu ya uraia.
Ninadhani CHADEMA huu ungekuwa wakati muafaka kumuomba huyu mzee awe mmoja wa washauri wenu katika chama.
Nafahamu pia ninyi wakuu wa CHADEMA huwa mnachungulia humu JF, naomba yachukueni mawazo yangu kwa uzito unaostahili!

Inawezekana unamuelewa vizuri na kumkubali jenerali ulimwengu, lakini mfano mdogo tu, uliona wapi mtu akapewa uimam akiwa mkristo au kupewa uaskofu huku akiwa muislam, fikiri vizuri wapi unapotakiwa kupeleka ushauri, ilitakiwa uanze kumshauri jenerali kujiunga na chadema
 
Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikiujiuliza swali hili " Hivi serikali ya ccm kwa nini imeshindwa kumtumia huyu gwiji wa habari na mambo mengi ya kiutawala, uchumi, siasa na uongozi? "
Kwa hakika Jenerali Ulimwengu ni mtu wa aina yake! Ukisoma CV yake na mambo yake unaweza kugundua kuwa is a gifted person. Na hata anapotoa ushauri wake, maranyingi unakuwa mzito mno, wenye maono ya mbali yaliyojaa hekima na busara.
Kinachonishangaza ni pale serikali inapomuona kuwa ni "threat"! Hii inanishangaza sana! ( Rejea sakata la kunyang'anywa uraia na Mr Clean). Maranyingi amekuwa akitoa ushauri kwa maandiko yake katika vitabu, magazeti, vijarida , midahalo ya wazi na kwenye vituo mbalimbali vya runinga! Ninafahamu wazi kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa akiandika sana makala zake katika gazeti la RAI enzi hizo likimilikiwa Jenerali Ulimwengu.
Ninadhani kwamba huu ni wakati muafaka kwa CHADEMA kuitumia hii hazina ambayo jioni yake inakaribia mno! CCM siku zote hawapendi mtu anayesema ukweli na kuwakosoa kwa makosa ya waziwazi mfano wa ujambazi wa KAGODA, MEREMETA, RICHMOND, na ushenzi mwingi amabao hausemeki.
Jenerali Ulimwengu ni muwazi daima, anaitumia elimu yake kuyaainisha matatizo yaliyopo na kuyatolea majawabu pamoja na kuielimisha jamii ya Watanzania kuhusu elimu ya uraia.
Ninadhani CHADEMA huu ungekuwa wakati muafaka kumuomba huyu mzee awe mmoja wa washauri wenu katika chama.
Nafahamu pia ninyi wakuu wa CHADEMA huwa mnachungulia humu JF, naomba yachukueni mawazo yangu kwa uzito unaostahili!

Alikwambia anataka kwenda Chadema??? au anatafuta chama??? Kweli JF imevamiwa siku hizi.
 
Naona ujumbe umefika, na chadema ukiwa na akili ni sifa tofauti na CCM ambapo ujuaji umewaponza wengi badala ya kuwapaisha
 
Mkuu Ndinani,
Habari za kupeana mawazo ya kuhusu namna kuendesha chama makini huwez uzifanya kwenye klabu za pombe ama kwenye vilinge vya soga( kahawa ). Mantiki ya uzi wangu ni kuwashauri CHADEMA wamuombe mzee Jenerali Ulimwengu awe mmoja wa washauri wa chama FORMAL not INFORMAL. Hata mimi huwa naonana na Mnyika kwenye canteen tunapokunywa chai na huwa ninamshauri mambo ya chama chao, lakini maudhui yake yatakuwa less concerned ukilinganisha na ushauri ambao ningetoa iwapo ningetambuliwa katika mfumo wa chama chao.
Jenerali Ulimwengu si mtu wa aina hiyo, ana uzito wa kipekee sana katika taifa letu Tanzania. Kwamba alikuwa knye system akaboronga si kweli, ninachofahamu ni kwamba the man was so strong kuwaambia ukweli majambazi na wanaotafuna Tanzania yetu bila huruma kwa kalamu yake na maneno yake amabayo yamemfanya awe mhanga hadi leo.
Ndiyo maana ninawashauri wakuu wa CHADEMA kulifikiria hili suala ikiwezakana wamuajiri kabsa kwa kazi hiyo kama walivyomuita Profesa Baregu, Jenerali deserves also!
 
Kwanini yeye asiitumie CDM?

Any way ,ia namjua JU ana vimambo fulani vya kichinichini hatari sana!....sema tu kuna muda huwa anazinduka na kukumbuka wajibu wake.
 
Back
Top Bottom