CHADEMA mmevuna mlichopanda

CHADEMA mmevuna mlichopanda

Mzalendo_Mwandamizi

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2007
Posts
1,116
Reaction score
4,773
Kabla ya Julai 2015, nilikuwa miongoni mwa Watanzania waliokuwa wakiiunga mkono Chadema. Sio kama mwanachama bali nilikuwa naafikiana nao katika harakati zao za kisiasa hususan vita dhidi ya ufisadi.

Lakini ghafla wakampokea Lowassa, mwanasiasa ambaye Chadema hao hao walimwandama kwa takriban miaka tisa mfululizo (tangu mwaka 2006 hadi 2015) wakimuita fisadi.

Na wala sikutafakari mara mbili, nikaamua kuacha kuiunga mkono Chadema. Bahati nzuri Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt Slaa ambaye pia alikuwa mgombea urais mwaka 2010, nae aliamua kuachana na chama hicho. Niliandika haya kumpongeza

Sidhani kama Chadema wanahitaji kupewa pole kwa sababu kila aliyejaribu kuwatahadharisha kuhusu Lowassa aliishia kutukanwa.

Uamuzi wa Lowassa kurejea CCM si jambo la kushangaza kwa sababu (a) alihama CCM kwa ajili tu ya kusaka urais huko Chadema (b) kwa kugombea urais kupitia Chadema, Lowassa aliweza kukihenyesha chama hicho kilichomuita fisadi huko nyuma, lakini kikalazimika kuzunguka nchi nzima kumsafisha Waziri Mkuu huyo wa zamani.

Kwa kifupi, Chadema mmevuna mlichopanda. Hatma ya chama hiki sasa itategemea sana jinsi kitakavyoweza kuhimili kipigo hiki kikubwa kabisa kwao. As it stands, kuna uwezekano mkubwa kabisa kwa chama hicho kutoambulia japo jimbo moja katika uchaguzi mkuu ujao, sio kwa kushindwa bali sio siri kuwa kuna wabunge kadhaa wa chama hicho wapo njiani kwenda CCM.

Na liwalo na liwe, wabunge wawili wasiotarajiwa kabisa kuwa ipo siku wataikimbia Chadema ni Kubenea na Bulaya wapo njiani kwenda CCM.

Tujikumbushe #FutureTweet hii ya Januari 9 mwaka jana


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kabla ya Julai 2015, nilikuwa miongoni mwa Watanzania waliokuwa wakiiunga mkono Chadema. Sio kama mwanachama bali nilikuwa naafikiana nao katika harakati zao za kisiasa hususan vita dhidi ya ufisadi.

Lakini ghafla wakampokea Lowassa, mwanasiasa ambaye Chadema hao hao walimwandama kwa takriban miaka tisa mfululizo (tangu mwaka 2006 hadi 2015) wakimuita fisadi.

Na wala sikutafakari mara mbili, nikaamua kuacha kuiunga mkono Chadema. Bahati nzuri Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt Slaa ambaye pia alikuwa mgombea urais mwaka 2010, nae aliamua kuachana na chama hicho. Niliandika haya kumpongeza

Dear Dkt Slaa,asante kwa kufanya maamuzi magumu kwa kujiuzulu. Tutakuenzi milele ~ Kulikoni Ughaibuni

Na niliwananga Chadema na makala hii

Siasa mchezo mchafu au baadhi ya wanasiasa ndo wachafu? USALITI: Chadema/Ukawa na Lowassa ~ Kulikoni Ughaibuni

Na baada ya Chadema kulamba matapishi yao na kumkumbatia Lowassa, chama hicho kiligeuka kuwa "chama cha mtu mmoja" kama nilivyotanabaisha katika makala hii

Makala yangu RAIA MWEMA la 05/08/15: "Chama kimoja Vyama Vingi Chama cha Mtu Mmoja" ~ Kulikoni Ughaibuni

Na the latest ni tahadhari niliyotoa baada ya Lowassa kukutana na Magufuli Ikulu mwaka jana

Uchambuzi Wa Kina Lowassa Kukutana Na JPM Na Kumpongeza: Mkakati Au Anarudi CCM?: ~ Kulikoni Ughaibuni

Sidhani kama Chadema wanahitaji kupewa pole kwa sababu kila aliyejaribu kuwatahadharisha kuhusu Lowassa aliishia kutukanwa.

Uamuzi wa Lowassa kurejea CCM si jambo la kushangaza kwa sababu (a) alihama CCM kwa ajili tu ya kusaka urais huko Chadema (b) kwa kugombea urais kupitia Chadema, Lowassa aliweza kukihenyesha chama hicho kilichomuita fisadi huko nyuma, lakini kikalazimika kuzunguka nchi nzima kumsafisha Waziri Mkuu huyo wa zamani.

Kwa kifupi, Chadema mmevuna mlichopanda. Hatma ya chama hiki sasa itategemea sana jinsi kitakavyoweza kuhimili kipigo hiki kikubwa kabisa kwao. As it stands, kuna uwezekano mkubwa kabisa kwa chama hicho kutoambulia japo jimbo moja katika uchaguzi mkuu ujao, sio kwa kushindwa bali sio siri kuwa kuna wabunge kadhaa wa chama hicho wapo njiani kwenda CCM.

Na liwalo na liwe, wabunge wawili wasiotarajiwa kabisa kuwa ipo siku wataikimbia Chadema ni Kubenea na Bulaya.




Sent using Jamii Forums mobile app
Viongozi na wafuasi wa Chadema hujiadai wanajitambua na wenye uelewa sana kumbe kinyume chake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Binafsi naona CHADEMA wamelamba dume kwa Lowassa kuondoka kuliko angeendelea kukaa na kusababisha power struggle 2020 hasa baada ya Lissu kumpiku kwa ushawishi.
Sioni CHADEMA wataathirika vipi kwa kitendo hicho.

Hakuna mbunge atakayeachia jimbo sasa ilhali uchaguzi haurudiwi tena kisheria.
 
usiache mbachao kwa msaala upitao
majuto ni mjukuu
asiye sikia la mkuu huvunjika guu

Mbowe amekisaidia sana chama lakini nadhani ni wakati sasa wa CHADEMA kuzaliwa upya kwa maslahi mapana ya demokrasia ya nchi yetu
 
wewe 2015 lowassa angegombea urais ndani ya CCM kwa sifa mbaya alizokuwa nazo CCM ingepata tabu sana pengine vurugu zingezuka inakuaje mtu mchafu namna ile anashinda urais wakati watanzania wanajua ni mchafu,kilichofanyika pale ni kuokoa CCM na maslahi yao kwani urais upo tu,kama hivi sio miaka mingi lowassa na kundi lake wanaweza ongoza nchi....

Huu ndio upambavu wangu,weka hekima yako wewe!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
usiache mbachao kwa msaala upitao
majuto ni mjukuu
asiye sikia la mkuu huvunjika guu

Mbowe amekisaidia sana chama lakini nadhani ni wakati sasa wa CHADEMA kuzaliwa upya kwa maslahi mapana ya demokrasia ya ncho yetu
Na hii ndio tafsiri ya CDM kuzaliwa upya Mkuu........
 
Hahahaha vipi sasa kwa ndugu yetu SLAA atamkimbia tena mamvi huko? Huyu jamaa hajawahi kuwa mtu sahihi chadema
 
Njia ya Lissu kuingia kwenye ligi kuu inazidi kung'olewa visiki....
Binafsi naona CHADEMA wamelamba dume kwa Lowassa kuondoka kuliko angeendelea kukaa na kusababisha power struggle 2020 hasa baada ya Lissu kumpiku kwa ushawishi.
Sioni CHADEMA wataathirika vipi kwa kitendo hicho.

Hakuna mbunge atakayeachia jimbo sasa ilhali uchaguzi haurudiwi tena kisheria.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TL njia nyeupeeeeeee 2020 patachimbika, watu hawataki tena pombe.
 
Binafsi naona CHADEMA wamelamba dume kwa Lowassa kuondoka kuliko angeendelea kukaa na kusababisha power struggle 2020 hasa baada ya Lissu kumpiku kwa ushawishi.
Sioni CHADEMA wataathirika vipi kwa kitendo hicho.

Hakuna mbunge atakayeachia jimbo sasa ilhali uchaguzi haurudiwi tena kisheria.
Lowassa kafanya vizuri kuondoka muda muafaka.Na hajataka kusubiri dakika za majeruhi kaondoka mapema CDM wana muda mzuri wa kujipanga

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom