VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Mkae mtulie kwa upendo na heshima. Muongee kwa staha na kwa kujenga hoja.Mheshimiane nyinyi kwa nyinyi.Tumieni Katiba yenu kumaliza hoja yoyote itakayoletwa mezani. Msikubali kupambanishwa na watamani madaraka kama wafanyavyo wenzenu wa 'jembe na nyundo'.
Mwenyekiti Mbowe na timu yako ya uongozi wa kitaifa,shughulikia matatizo ya chamani mwako kikatiba.Wananchi wa Tanzania wameshawaelewa hoja zenu.Wanasubiri 2015 wawape nchi muiendeshe.Bungeni,onesheni kuwa mnaweza.Majukwaani,jengeni hoja za kiukombozi. Magazetini,andikweni kwa wema.Runingani,tangazweni mnavyojisambaza kwa hoja mujarabu na umati wa Watanzania walio na matumaini nanyi.
Mwaka 2015,simamisheni mgombea ambaye hata uchakachuzi hautampora ushindi wake. Iwe wa Urais,ubunge au udiwani.Watanzania wanawangoja.Msiwaangushe. Mkae mtulie na hatari zote zisiwafikie.
Nangoja ukombozi...
Mwenyekiti Mbowe na timu yako ya uongozi wa kitaifa,shughulikia matatizo ya chamani mwako kikatiba.Wananchi wa Tanzania wameshawaelewa hoja zenu.Wanasubiri 2015 wawape nchi muiendeshe.Bungeni,onesheni kuwa mnaweza.Majukwaani,jengeni hoja za kiukombozi. Magazetini,andikweni kwa wema.Runingani,tangazweni mnavyojisambaza kwa hoja mujarabu na umati wa Watanzania walio na matumaini nanyi.
Mwaka 2015,simamisheni mgombea ambaye hata uchakachuzi hautampora ushindi wake. Iwe wa Urais,ubunge au udiwani.Watanzania wanawangoja.Msiwaangushe. Mkae mtulie na hatari zote zisiwafikie.
Nangoja ukombozi...