Baada ya uchaguzi 2010 chama cha DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) hawakukubaliana na matokeo yaliyompa ushindi ndugu KIKWETE. Wakakataa kumtambua kama RAIS wa JMT. Hawakuishia hapo tu bali hata alipotinga bungeni wote walitoka nje ili kudhihirisha kutokumkubali JK kama kiongozi na rais wa JMT.
Wakiongozwa na kauli mbiu ya PEOPLES POWER, Chadema walijipambanua kuwa maamuzi na maswala muhimu yote yataamuliwa na wananchi wenyewe na wananchi ndo watakuwa mahakama kwa kila jambo la serikali.
Mpaka sasa naandika mada hii, sijawahi sikia CHADEMA wakiutangazia uma kuwa wamemtambua Jakaya Mrisho Kikwete kama rais ya Jamuhuri hii na wanautambua ushindi wake wa mwaka 2009/2010
Kwa msingi huu najiuliza yafuatayo/ na wanajavi mnisaidie.
- Chadema wameenda IKULU mara mbili kutafuta eti BUSARA ya raisi katika maamuzi mabovu yaliyotolewa na bunge kuhusu muswaada wa KATIBA mpya.Je walienda kuonana na nani?? na Kama ni RAIS je ni yuleyule wasiyemtambua?
- Kama walivyotoka katika ile hotuba ya kwanza nini kiliwazuia jana kuto toka tena?? au huyu kikwete si yule wa wakati ule
- Je CHADEMA kwa matendo yao yanayopingana na kauli walizotoa hawaoni wanatuchanganya sisi wanachama?
- Je chadema wanapokuwa majukwaani na kusema RAIS inchi imemshinda huwa wanamaanisha RAIS yupi??
Kwa misingi hii napenda kuwashauri viongozi wa chadema kuwa ni muda muafaka sasa waitishe KIKAO na waandishi wa habari na kuutangazia uma wa watanzania kuwa wanaifuta kauli yao waliyoitoa 2010 na wanamtambua JK kama RAIS halali wa JMT, na wataendelea kumtambua mpaka muda wake utapoisha. Or else waache unafiki wa maneno wakati matendo ni kinyume.Mimi ka mwanachama nasikitishwa na misimamo isiyotekelezeka ambayo hutolewa mara kwa mara na VIONGOZI. Hii ni kama kulamba matapishi yako mwenyewe