CHADEMA Mara yasitisha ziara mkoa mzima

CHADEMA Mara yasitisha ziara mkoa mzima

Lai Otieno

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2013
Posts
311
Reaction score
90
Chadema mkoa wa mara!! Wamesitisha rasmi kwa muda mkutano zote pamoja na harakati zote. Hii nikutokana na msiba mkubwa uliotukumba kama mkoa siku ya leo kutokana na ajali mbaya ya mabasi mawili na zaidi ya abiri 39 kufariki papo hapo pia wamewaomba wadau wao wote wajitokeza kuchangia damu pamoja na mahitaji mbali mbali kwa wale majeruhi waliopo hospitali ya mkoa wa Mara..
 
Pole nyingi ziwafikie hapo mlipo kwakweli niko mbali ningejitokeza kuchangia damu..Mungu awape wafiwa nguvu ktk kipindi hiki kigumu

Raha ya milele uwape eebwana...

Namwanga wa milele uwaangazie..

Wapumzike kwa amani....Amina

BACK TANGANYIKA
 
Poleni sana mliofiwa na ndugu katika ajali hii mbaya mno. Naomba Mungu awape nguvu katika kuupokea msiba mkubwa huu. Uwape Ee Bwana Raha ya milele na mwanga wa milele uwaangazie na tunaomba uwasamehe makosa yao pia uwalipe kwa yale machache mema waliyoyafanya wakati wa uhai wao kadiri ya mapenzi yako Bwana. Amina.
 
poleni sana wafiwa wote pamoja majeruhi Mungu awajarie mpone mapema
 
Chadema ni chama kinachojali wananchi wote bola kujali itikadi za vyama.

Big up 😛eace:chadema:israel:
 
Kamanda poleni sana Tuwakumbuke marehemu kwa sala..
Ofisi ya mnikulu inampango gani,dhidi ya ajali hizi?,au ndo lugha za kila siku,madereva wawe waangalifu?, tulishuhudia ajali ya mv bukoba,mrli za zamzibar,treni ya kati,mabasi mengi kugongana,Lakini serikali hii haina tafiti,haina suluhu ni serikali inayolalamika tu!.
Hivi anajua kuwa raslimali watu imepotea?
 
Pole nyingi ziwafikie hapo mlipo kwakweli niko mbali ningejitokeza kuchangia damu..Mungu awape wafiwa nguvu ktk kipindi hiki kigumu

Raha ya milele uwape eebwana...

Namwanga wa milele uwaangazie..

Wapumzike kwa amani....Amina

BACK TANGANYIKA

Poleni wafiwa,Bwana Yesu awatie nguvu,hiyo ni ajali mbaya kabisa,ajali kama hizo utakuta watu 3au2 wa familia 1,wamefariki,inauma sana, shetani yuko kazini,tunanguvu ya kumzuia kwa maombi,hakikisha unaposafiri vunja roho ya mauti kwa jina la yesu,pangua mitego yao,nia zao,roho za ajali, baada ya hapo funika hicho chombo kwa damu ya Yesu,uwe na imani na utakatifu,yote kwa yote hao wametangulia,atujui walijiandaa vipi mungu anajua,jinsi walivyojiandaa ndivyo watakapokelewa,huwezi badilisha chochote kwa kuwaombea,
 
Ofisi ya mnikulu inampango gani,dhidi ya ajali hizi?,au ndo lugha za kila siku,madereva wawe waangalifu?, tulishuhudia ajali ya mv bukoba,mrli za zamzibar,treni ya kati,mabasi mengi kugongana,Lakini serikali hii haina tafiti,haina suluhu ni serikali inayolalamika tu!.
Hivi anajua kuwa raslimali watu imepotea?

ukoo wa panya wameshasema niuzembe wa drivers
 
Awajarie=Awajalie FaizaFoxy, watu8

Hii ni sredi spesho kwa watu wa Mara mkuu, hivyo tegemea sana kukutana na lugha kama hiyo...

Ila ile ajali ya jana ilikuwa mbaya sana, zimeona footage na baadhi ya picha aisee inatisha...

Pole kwa wafiwa wote na Mungu awape afya tena waliojeruhiwa...
 
poleni sana wana-Mara na makamanda kwa ujumla,Mungu awajalie na majeruhi wapone salama
 
Chadema wanatafuta cheap popularity kwnye roho za watu
 
Chadema mnajifanya kuwa ninyi ni wasamaris kiliko ccm, ongeeni sasa mbona harsoni mwakiembe kafika hadi hospitalini na kutoa maamuzi hapo hapo ya kufungiwa kwa kampuni mbili za mabasi yaliyosababisha ajali hiyo.
 
Chadema mnajifanya kuwa ninyi ni wasamaris kiliko ccm, ongeeni sasa mbona harsoni mwakiembe kafika hadi hospitalini na kutoa maamuzi hapo hapo ya kufungiwa kwa kampuni mbili za mabasi yaliyosababisha ajali hiyo.

Huo ni wajibu wake yeye kama kiongozi wa serikali,pia bado haijasaidia yeye kuyafungia mabasi wakati tayari yameshaua raslimali watu,kwanini asingechukua hatua kabla ya?na kusimamishwa mabasi yote ambayo hayafanyiwi service mara kwa mara na madereva wasiyo wa uhakika?
 
Back
Top Bottom