CHADEMA Makao Makuu, wekeni utaratibu wa kuwatambua madiwani wanaogoma kupokea hongo ili wakisaliti chama na wapiga kura wao

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,033
144,386
Hili jambo kama sikosei leo naliongea kwa mara ya pili hapa JF.

Viongozi wa CHADEMA, mtu kukataa rushwa ya milioni 200 na hapo hapo akatoa tuhuma hizo hadharani kupitia vyomba vya habari kama huyu Meya wa Iringa, si jambo dogo ambalo linapaswa kuacha lipite hivi hivi.

Mtu kama huyu bila shaka ana ushahidi vinginevyo wamshitaki na wakishindwa kufanya hivyo, nyinyi kama chama chukueni hatua ya kumpongeza kwa kumpa ama tuzo au nishani maalumu itakayotolewa na chama na hili lifanyike kwa kila diwani atakaewza kufanya jambo kama hili la kizalendo na tuzo au nishani hiyo akabidhiwe mbele ya waandishi wa habari.

Vile vile nashauri mbunge Joshua Nassari na mwenzake Godbless Lema nao chama kiwaandalie nishani ya uzalendo na ushujaa kwa kutoa hadharani ushahidi wa tuhuma za kununua madiwani mkoani Arusha na kukabidhi ushahidi huo katika mamlaka husika (TAKUKURU).

Maadamu wameshindwa kuwashitaki kwa kuwachafua, basi huu kwetu ni ushahidi kuwa tuhuma walizotoa zilikuwa za kweli maana wazungu wanasema, "silence means yes."

Na Ili kuokoa gharama, hawa wote niliowataja na wengine ambao wamekuwa wakieleza hujuma hizi kupitia vyombo mbalimbali vya habari, wote kwa pamoja; wapewe nishani au tuzo hizo katika tukio moja kubwa la pamoja litakaloandaliwa na chama huku mkitoa mialiko kwa viongozi wa vyama vingine na wa taasisi zingine watakao kuwa tayari kushiriki katika tukio hilo wakiwemo na watu binafsi.

Ifike mahali tutambue uzalendo wa watu wa aina hii katika chama kwa kuwapa heshima wanayostahili kama ilivyofanyika kwa Lissu kukabidhiwa sera mpya za chama akiwa nje ya nchi bila shaka ikiwa ni heshima aliyopewa na chama chake.

Ni ushauri tu na hii si mara ya kwanza.

CHADEMA Makao Makuu,mpeni tuzo diwani Eliaf Michael - JamiiForums
 
Naunga mkono hoja, lakini mtu kama Nassari sio wa kumuamini sana kwa maoni yangu. Huyu meya wa Iringa bora 2020 cjama kimpe upendeleo kwa nafasi ya ubunge maana Msigwa siku hizi amekua tiamaji tiamaji hana tofauti na Riyoba wa serengeti.
 
Wazo zuri.... Ila hiyo hafla ya kukabidhi nishani/tuzo itafanyikia vipi, maana wataisambaratisha kabla haijaanza
Sio ndio watauthibitishia ulimwengu kuwa yasema ni ya kweli.

Wacheni wahangaike maana hawana namna.
 
Hili jambo kama sikosei leo naliongea kwa mara ya pili hapa JF.

Viongozi wa CHADEMA, mtu kukataa rushwa ya milioni 200 na hapo hapo akatoa tuhuma hizo hadharani kupitia vyomba vya habari kama huyu Meya wa Iringa, si jambo dogo ambalo linapaswa kuacha lipite hivi hivi.

Mtu kama huyu bila shaka ana ushahidi vinginevyo wamshitaki na wakishindwa kufanya hivyo, nyinyi kama chama chukueni hatua ya kumpongeza kwa kumpa ama tuzo au nishani maalumu itakayotolewa na chama na hili lifanyike kwa kila diwani atakaewza kufanya jambo kama hili la kizalendo na tuzo au nishani hiyo akabidhiwe mbele ya waandishi wa habari.

Vile vile nashauri mbunge Joshua Nassari na mwenzake Godbless Lema nao chama kiwaandalie nishani ya uzalendo na ushujaa kwa kutoa hadharani ushahidi wa tuhuma za kununua madiwani mkoani Arusha na kukabidhi ushahidi huo katika mamlaka husika (TAKUKURU).

Maadamu wameshindwa kuwashitaki kwa kuwachafua, basi huu kwetu ni ushahidi kuwa tuhuma walizotoa zilikuwa za kweli maana wazungu wanasema, "silence means yes."

Na Ili kuokoa gharama, hawa wote niliowataja na wengine ambao wamekuwa wakieleza hujuma hizi kupitia vyombo mbalimbali vya habari, wote kwa pamoja; wapewe nishani au tuzo hizo katika tukio moja kubwa la pamoja litakaloandaliwa na chama huku mkitoa mialiko kwa viongozi wa vyama vingine na wa taasisi zingine watakao kuwa tayari kushiriki katika tukio hilo wakiwemo na watu binafsi.

Ifike mahali tutambue uzalendo wa watu wa aina hii katika chama kwa kuwapa heshima wanayostahili kama ilivyofanyika kwa Lissu kukabidhiwa sera mpya za chama akiwa nje ya nchi bila shaka ikiwa ni heshima aliyopewa na chama chake.

Ni ushauri tu na hii si mara ya kwanza.

CHADEMA Makao Makuu,mpeni tuzo diwani Eliaf Michael - JamiiForums
Wanapandisha dau hao.
Zikifika mia tano kama ni kweli nawashauri waende kimwili lakini kiroho wabaki Chadema.

Harakati zote hizo za kujiuza na kununua mwisho wake ni 2025,hivyo wote waliojiuza kimaslahi watarudi upinzani mana upinzani wa wakati huo utakua ni imara sana na naamini wabunge watakaribia watafikia 50/50.
Na pia hawa wenyeviti feki wa upinzani watakua wameshasambaratika na vyama vyao vitakua vinaongozwa na wapinzani wa kweli kama akina Tundu ,Kubenea,Mnyika,Bonifasi ,Zito, Heche, Esther Matiku ,Kambaya na wengine. CCM nayo itakua imemeguka mmeguko wa awamu ya Tatu na ya Mwisho. Patakua na Vyama kuungana kwa nia ya dhati ya kuiondoa Sisiem madarakani.

Juhudi na woga wote wa Polepole ni kuhakikisaha 2020 Mwenyekiti wao anapita kwa kishindo na bunge lisiwe na wapinzani wa kuiumbua serikali.
 
Farijianeni chadema mtakuja kushtuka 2020 hamtaamini kitakachotokea.mfano usikie magufuli kashinda kwa 90% hivi kwani mtafanyaje maana wa kuandamana kwa Sasa simuoni.kwa kweli jiandaeni kisaikolojia
 
Farijianeni chadema mtakuja kushtuka 2020 hamtaamini kitakachotokea.mfano usikie magufuli kashinda kwa 90% hivi kwani mtafanyaje maana wa kuandamana kwa Sasa simuoni.kwa kweli jiandaeni kisaikolojia
Hata Mimi naona dalili ya Upinzani kupotea Bungeni.
Siupendi sana upinzani hasa ule unaoongozwa na waongo na watu wabinafsi na madikteta kama Mbowe.
Hata hivyo naamini Kufikia 2019 ACT itakua kwenye nafasi nzuri sana na pia CUF Lipumba( japo Mwenyekiti wake ni wakala wa CCM ) itakua na mwamko mkubwa kwa Bara hasa maeneo ya Tanga,Lindi,Mtwara na Pwani.
Pia Mamluki wengi akiwemo Mbowe watakua wamepigwa chini. Vyama vingi vitakua vinaongozwa na wapinzani wa kweli kwa hiyo CCM inaweza ikajitangazia ushindi wa kufuru lakini ikaliacha Taifa pabaya sana. Tusiombee uhuni wa chaguzi ndogo uendelee Kuna watu watakuja kuzeekea kwenye kesi au gerezani na kulitia taifa doa.Nchi yetu inapoteza sifa ya watanzania kuwa watu wakarimu na wenye upendo na mshikamano. Kwa sasa watu wamegawanyika makundi mawili kundi la wanaojiona kuwa wao watatawala milele na kuwa wao ni miungu wenye kushusha adhabu kwa wenzao bila kuulizwa na wale waliokata tamaa kwa hofu kuu.
Kundi la watu wachache sana limetufikisha hapa ,hasa wateule. Na wale wanaotafuta nafasi za kuteuliwa,wanawaza madaraka na maslahi tu bila kujali mustakabali wa nchi. Kuna watu ukiwasikiliza unajiuliza maswali mpaka unakosa majibu mana ni watu waliojisahau kabisa kuwa wao ni binadamu na hawataishi milele,wamelewa madaraka na kulewa sifa.

Nadhani Mabadiliko hua yanaletwa na wapinzani wa Kweli na jasiri.
Mungu siku zote hafanyi kazi na watu,waongo , wanafiki na waoga. Ukiona upinzani unapota ujue Mungu hayupo upande huo mana umejaa uongo na unafiki na ubinafsi.
 
Wazo zuri.... Ila hiyo hafla ya kukabidhi nishani/tuzo itafanyikia vipi, maana wataisambaratisha kabla haijaanza
Hata mimi naunga mkono hoja hii; ila siamini kama serikali (CCM & polisi) watakuwa tayari kuvumilia maumivu ya impact ya shughuli kama hiyo. Wataisambaratisha kabla haijaanza.
 
Hili jambo kama sikosei leo naliongea kwa mara ya pili hapa JF.

Viongozi wa CHADEMA, mtu kukataa rushwa ya milioni 200 na hapo hapo akatoa tuhuma hizo hadharani kupitia vyomba vya habari kama huyu Meya wa Iringa, si jambo dogo ambalo linapaswa kuacha lipite hivi hivi.

Mtu kama huyu bila shaka ana ushahidi vinginevyo wamshitaki na wakishindwa kufanya hivyo, nyinyi kama chama chukueni hatua ya kumpongeza kwa kumpa ama tuzo au nishani maalumu itakayotolewa na chama na hili lifanyike kwa kila diwani atakaewza kufanya jambo kama hili la kizalendo na tuzo au nishani hiyo akabidhiwe mbele ya waandishi wa habari.

Vile vile nashauri mbunge Joshua Nassari na mwenzake Godbless Lema nao chama kiwaandalie nishani ya uzalendo na ushujaa kwa kutoa hadharani ushahidi wa tuhuma za kununua madiwani mkoani Arusha na kukabidhi ushahidi huo katika mamlaka husika (TAKUKURU).

Maadamu wameshindwa kuwashitaki kwa kuwachafua, basi huu kwetu ni ushahidi kuwa tuhuma walizotoa zilikuwa za kweli maana wazungu wanasema, "silence means yes."

Na Ili kuokoa gharama, hawa wote niliowataja na wengine ambao wamekuwa wakieleza hujuma hizi kupitia vyombo mbalimbali vya habari, wote kwa pamoja; wapewe nishani au tuzo hizo katika tukio moja kubwa la pamoja litakaloandaliwa na chama huku mkitoa mialiko kwa viongozi wa vyama vingine na wa taasisi zingine watakao kuwa tayari kushiriki katika tukio hilo wakiwemo na watu binafsi.

Ifike mahali tutambue uzalendo wa watu wa aina hii katika chama kwa kuwapa heshima wanayostahili kama ilivyofanyika kwa Lissu kukabidhiwa sera mpya za chama akiwa nje ya nchi bila shaka ikiwa ni heshima aliyopewa na chama chake.

Ni ushauri tu na hii si mara ya kwanza.

CHADEMA Makao Makuu,mpeni tuzo diwani Eliaf Michael - JamiiForums
Wazo zuri sana hili tena ningependekeza hata viongozi wa serikali waalikwe, japo wakijua maudhui ya shughuli yenyewe wanaweza wasije na badala yake waisambaratishe kwa sababu ambazo in obvious!
 
Back
Top Bottom