CHADEMA & M4C: Kuelekea 2015 yakemeeni haya Kagera!.

CHADEMA & M4C: Kuelekea 2015 yakemeeni haya Kagera!.

SCHRUMBEGER

Member
Joined
Jan 29, 2013
Posts
12
Reaction score
2
Kumeanza kutokea tabia isiyokuwa ya kuridhisha kwa baadhi ya watu hasa wale wenye nia ya kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu 2015 kupitia CHADEMA. Wamekuwa kama CCM, maana wameanza kugombania majimbo, wameanza kutengeneza fitini mara huyu ni pandikizi n.k. Ni vema tukaiacha demokrasia ichukue nafasi yake ili tuweze kujitofautisha na wale wa upande wa pili.

Niwakumbushe wenzangu kuwa kazi ya ujenzi wa chama ni kubwa, haiwezi kufanywa na mtu mmoja katika jimbo/wilaya na CHADEMA ikaweza kupata ushindi 2015. Kwa mawazo yangu naona ni vizuri wakati wa M4C mkoani Kagera tukayazungumzia haya yafuatayo:

a) Hakuna mwenye jimbo/wilaya, jimbo/wilaya ni mali ya wananchi/wapiga kura.

b) Ni vema tukajua kuwa “kura ya maoni” ndiyo itakayotumika kutupatia mgombea wa nafasi yoyote kwa mujibu wa taratibu za chama.

c) Tusidhani kuwa mtu kuwahi kujiunga CHADEMA ni kigezo tosha cha kuaminiwa. Aliyeingia CHADEMA leo kwa nia ya kweli ya kimabadiriko ni bora kuliko aliyeingia CHADEMA miaka kumi iliyopita lakini bado hajaamini katika mabadiliko ya kweli!.

d) Mtu kuwa karibu na viongozi wakuu wa chama na makao makuu siyo hoja ya kuhalarisha mtu kuvunja taratibu za chama kwa maslahi yake.

e) Tabia ya kuchafuana kwa meseji, fitina, majungu na mizengwe ni tabia ya CCM ambayo haiwezi kumsaidia mtu kukubalika katika jamii yake, kwani kwa mbinu hii hata CCM wameshindwa. Turudi kwenye falsafa ya chama i.e “Nguvu ya Umma” ndiyo pekee itakayomsaidia mtu.

f) Kurubuni viongozi wa jimbo/wilaya kwa namna yoyote ile ili wavunje taratibu za chama kwa makusudi kabisa kwa ajiri ya kumpendelea mtu ni “Rushwa”. Mtu huyo hawezi kupata situ ridhaa ya chama bali pia ridhaa ya wananchi kuwaongoza.

g) Kutumia uhusiano wa kimapenzi na viongozi wa chama kwa kutaka kupewa kipaumbele na upendeleo katika shughuli za chama pia ni “Rushwa”. Mtu huyo hawezi kupata situ ridhaa ya chama bali pia ridhaa ya wananchi kuwaongoza. Pia ni kukidharirisha chama na wewe wenyewe.

h) “Watu wote wenye nia ya kugombea wajitokeze mapema ili watu wawajue” waraka no.2 wa katibu mkuu wa 2011. Watu watawajua kwa kushiriki katika shughuli za kijamii, kimaendeleo n.k huku tukikijenga na kukiimarisha chama. Hili haliwezi kufanywa kwa kuitisha tu vikao vya kamati tendaji ya jimbo na kutoa posho tukadhani eti watu wametujua. Twende kwa wananchi maana wao ndo wenye maamuzi lakini pia ni wengi (nguvu ya umma) kuliko kamati tendaji!.

i) Tujitofautishe na CCM ambayo watu hasa wazee vijijini walishaichukulia ni kama dini/imani fulani katika mioyo yao. Kwa hiyo mbinu zao za kukijenga na kukiimarisha chama chao lazima zitofautiane kabisa na zile za CHADEMA.

Ikumbuke kuwa “It is very difficult to exercise freedom in poverty”
 
Mkuu, (id ngumu-kama kijerumani hivi)

Nakubaliana na wewe 100%. Nakusudia kutangaza nia na sikwa mtindo wa kuchafuana. Niliongea na jamaa yangu kijijini na anishauri ni sigombee kwa sababu siasa imejaa uongo na unafiki na swali langu kwake lilikuwa kwa hiyo? siasa tuwaachie wanafiki na waogo? of course ndicho wanasiasa wengi nchini wamejitahidi kufanya. Lakini je tuwaachie awajamaa...waendelee hivyo? No!
 
Mi Naona hata mtoa post naye yupo kinafiki pia,Mimi nadhani muda huu ni nyie muimalishe chama kwanza si muda wa kutangaza nia hata kidogo,nia zenu zionekane kwenye kutangaza chama,kamwe msijidanganye kuwa cdm ipo imara kihivyo,wenzenu ccm hawalali mpaka wamewasambaratisha,mtapambana na kutangaza nia mwisho wa siku mtakuta hakuna kitu kinaitwa cdm,kuweni makini tafadhali.
 
Jitahidini kuondoa tofauti zenu mapema kabla hamjawaangusha wananchi, kuna kila dalili mna mivutano kati yenu na hasa huko muleba, 2015 tunataka jimbo sio mapambano ya wagombea vyeo
 
Nakubaliana 100% na mtoa post. Pia ni kweli Muleba hasa Muleba Kaskazini kuna mgogoro mkubwa, nafikiri mtoa post anaelewa vizuri. Chadema ni ya Watanzania Wote wanaotaka mabadiliko yakweli kutoka kwenye minyororo ya ukiritiba wa kifisadi tuliyonayo sasa. Tatizo kubwa huku kuna vijifisadi dagaa ambavyo vinaanza kuchomoka, kupitia ukaribu wao kwa viongozi wa Kitaifa, Mkoa, Jimbo mpaka sasa wanashukuka kwenye Kata ili kughiribu wapigakura. Tunaomba sana ratiba ya M4C itangazwe hata kwenye vyombo vya habari maana huku Muleba hao viongozi waliojiweka hawawezi kufikisha ujumbe kwa wanachama maana kuna kata zingine hazina hata uongozi lakini jimbo linadanganya kuwa viongozi wapo. Sasa M4C itakapochakaza kila kitongoji ndipo Wakombozi wa kweli watajionea uozo tulionao na kujua ni kwanini tumechelewa kushika Dola. Maana CDM inavyoonekana kwenye Mikutano ya Kamanda toka sehemu ambazo zimekwisha funguka inafikirika ndivyo ilivyo sio. Hii inatokana na walijipa nafasi bila kuchaguliwa na wapiga kura na wamebaki na dhana kuwa sie ndio wenye Chama na wanaoingia leo ni Mamluki wa CCM. Dr. wa ukweli ukisaidiwa na Makamanda wa ukweli ondoeni hawa watu kungali mapema ili tujipange kwani ukombozi wa kweli uko mlangoni.
 
Hoja ni nzuri sana ya kutoa angalizo,ingawa naona msisitizo huko Muleba,sijui wilaya nyingine huko mambo yao yako vipi?.Labda namimi nitoa mawazo yangu kidogo,kwa CDM,kazi kubwa mnayo mbele ya safari,kwasababu gani machampion wa M4C,Muleba wengi wao ndo masuporter wa UFISADI.
 
Kumeanza kutokea tabia isiyokuwa ya kuridhisha kwa baadhi ya watu hasa wale wenye nia ya kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi mkuu 2015 kupitia CHADEMA. Wamekuwa kama CCM, maana wameanza kugombania majimbo, wameanza kutengeneza fitini mara huyu ni pandikizi n.k. Ni vema tukaiacha demokrasia ichukue nafasi yake ili tuweze kujitofautisha na wale wa upande wa pili.

Niwakumbushe wenzangu kuwa kazi ya ujenzi wa chama ni kubwa, haiwezi kufanywa na mtu mmoja katika jimbo/wilaya na CHADEMA ikaweza kupata ushindi 2015. Kwa mawazo yangu naona ni vizuri wakati wa M4C mkoani Kagera tukayazungumzia haya yafuatayo:

a) Hakuna mwenye jimbo/wilaya, jimbo/wilaya ni mali ya wananchi/wapiga kura.

b) Ni vema tukajua kuwa "kura ya maoni" ndiyo itakayotumika kutupatia mgombea wa nafasi yoyote kwa mujibu wa taratibu za chama.

c) Tusidhani kuwa mtu kuwahi kujiunga CHADEMA ni kigezo tosha cha kuaminiwa. Aliyeingia CHADEMA leo kwa nia ya kweli ya kimabadiriko ni bora kuliko aliyeingia CHADEMA miaka kumi iliyopita lakini bado hajaamini katika mabadiliko ya kweli!.

d) Mtu kuwa karibu na viongozi wakuu wa chama na makao makuu siyo hoja ya kuhalarisha mtu kuvunja taratibu za chama kwa maslahi yake.

e) Tabia ya kuchafuana kwa meseji, fitina, majungu na mizengwe ni tabia ya CCM ambayo haiwezi kumsaidia mtu kukubalika katika jamii yake, kwani kwa mbinu hii hata CCM wameshindwa. Turudi kwenye falsafa ya chama i.e "Nguvu ya Umma" ndiyo pekee itakayomsaidia mtu.

f) Kurubuni viongozi wa jimbo/wilaya kwa namna yoyote ile ili wavunje taratibu za chama kwa makusudi kabisa kwa ajiri ya kumpendelea mtu ni "Rushwa". Mtu huyo hawezi kupata situ ridhaa ya chama bali pia ridhaa ya wananchi kuwaongoza.

g) Kutumia uhusiano wa kimapenzi na viongozi wa chama kwa kutaka kupewa kipaumbele na upendeleo katika shughuli za chama pia ni "Rushwa". Mtu huyo hawezi kupata situ ridhaa ya chama bali pia ridhaa ya wananchi kuwaongoza. Pia ni kukidharirisha chama na wewe wenyewe.

h) "Watu wote wenye nia ya kugombea wajitokeze mapema ili watu wawajue" waraka no.2 wa katibu mkuu wa 2011. Watu watawajua kwa kushiriki katika shughuli za kijamii, kimaendeleo n.k huku tukikijenga na kukiimarisha chama. Hili haliwezi kufanywa kwa kuitisha tu vikao vya kamati tendaji ya jimbo na kutoa posho tukadhani eti watu wametujua. Twende kwa wananchi maana wao ndo wenye maamuzi lakini pia ni wengi (nguvu ya umma) kuliko kamati tendaji!.

i) Tujitofautishe na CCM ambayo watu hasa wazee vijijini walishaichukulia ni kama dini/imani fulani katika mioyo yao. Kwa hiyo mbinu zao za kukijenga na kukiimarisha chama chao lazima zitofautiane kabisa na zile za CHADEMA.

Ikumbuke kuwa "It is very difficult to exercise freedom in poverty"

Ndani ya CDM kwenye maandishi mekundu hapo juu huwezi kukwepa, ndivyo wanavyoishi. Subiri mkuu ujionee 2015 hasa katika majimbo ya kawe, moshi mjini ambako Ndesamburo hatagombea tena na maeneo mengine. Usisahau wakati baadhi ya makada ya CDM wanafukuzwa chama walisema kuna mbunge wa viti maalum ana ujauzito wa mmoja wa viongozi wa juu kabisa wa CDM.
 
Hoja ni nzuri sana ya kutoa angalizo,ingawa naona msisitizo huko Muleba,sijui wilaya nyingine huko mambo yao yako vipi?.Labda namimi nitoa mawazo yangu kidogo,kwa CDM,kazi kubwa mnayo mbele ya safari,kwasababu gani machampion wa M4C,Muleba wengi wao ndo masuporter wa UFISADI.

afadhali sasa wameanza kuona nao wameoza. Kwa nini wanakwenda Muleba wakati mfano mzuri tu ni katika safu nzima ya uongozi wa juu ambako kuna ukiritimba mkubwa. Ni vema wakaanza na huko juu kwanza kama kweli wana nia ya dhati ya kukuza demokrasia ndani ya chama.
 
Nakubaliana 100% na mtoa post. Pia ni kweli Muleba hasa Muleba Kaskazini kuna mgogoro mkubwa, nafikiri mtoa post anaelewa vizuri. Chadema ni ya Watanzania Wote wanaotaka mabadiliko yakweli kutoka kwenye minyororo ya ukiritiba wa kifisadi tuliyonayo sasa. Tatizo kubwa huku kuna vijifisadi dagaa ambavyo vinaanza kuchomoka, kupitia ukaribu wao kwa viongozi wa Kitaifa, Mkoa, Jimbo mpaka sasa wanashukuka kwenye Kata ili kughiribu wapigakura. Tunaomba sana ratiba ya M4C itangazwe hata kwenye vyombo vya habari maana huku Muleba hao viongozi waliojiweka hawawezi kufikisha ujumbe kwa wanachama maana kuna kata zingine hazina hata uongozi lakini jimbo linadanganya kuwa viongozi wapo. Sasa M4C itakapochakaza kila kitongoji ndipo Wakombozi wa kweli watajionea uozo tulionao na kujua ni kwanini tumechelewa kushika Dola. Maana CDM inavyoonekana kwenye Mikutano ya Kamanda toka sehemu ambazo zimekwisha funguka inafikirika ndivyo ilivyo sio. Hii inatokana na walijipa nafasi bila kuchaguliwa na wapiga kura na wamebaki na dhana kuwa sie ndio wenye Chama na wanaoingia leo ni Mamluki wa CCM. Dr. wa ukweli ukisaidiwa na Makamanda wa ukweli ondoeni hawa watu kungali mapema ili tujipange kwani ukombozi wa kweli uko mlangoni.

Huyu yalimshinda kwake kule Karatu, Muleba ndo ataweza? yeye mwenyewe ni source ya upendeleo.
 
Hoja ni nzuri sana ya kutoa angalizo,ingawa naona msisitizo huko Muleba,sijui wilaya nyingine huko mambo yao yako vipi?.Labda namimi nitoa mawazo yangu kidogo,kwa CDM,kazi kubwa mnayo mbele ya safari,kwasababu gani machampion wa M4C,Muleba wengi wao ndo masuporter wa UFISADI.

Mtoa mada hajataja Jimbo lolote zaidi ya kutaja mkoa wa Kagera akimaanisha wilaya na majimbo yote. Labda kuna jambo unalijua katika jimbo la Muleba ambalo mtoa post kaligusa moja kwa moja. Yote ya yote ni vema kuyakemea mambo hayo hapo juu ili tuweze kupata ushindi 2015.
 
Hapa tatzo ni watu kuanza kujiunga CDM ili kupata vyeo,lakini wangoje tu mbivu na mbichi zitafahamika.. mtajichuja tu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom