CHADEMA kwanini hamjifunzi kutoka CCM?

CHADEMA kwanini hamjifunzi kutoka CCM?

Vyovyote vile lkn kuna Uongozi mpya unakuja kila baada ya miaka 5-10,
Kati ya Mwinyi, Mkapa, Kikwete ni yupi mhula wake wa kuwa Mwenyekiti ulifanana na unaotajwa kwenye katiba ya chama chenu. Katiba ya Chama chenu inasema kwamba Mwenyekiti huchaguliwa kila baada ya miaka mingapi na lini ilifanyika hivyo?
 
Labda kwa sababu hsujapata nafasi ya kujua uwezo wa wengine, sasa utaujuaje kama hutoi nafasi?
kwakweli chadema kwa kipindi hiki tunapitia wakati mgumu sana kwahiyo sio vema kufanya majaribio kindi hiki ili tusije pata watu kama katambi, nawengine wa namna hiyo
 
Kati ya Mwinyi, Mkapa, Kikwete ni yupi mhula wake wa kuwa Mwenyekiti ulifanana na unaotajwa kwenye katiba ya chama chenu. Katiba ya Chama chenu inasema kwamba Mwenyekiti huchaguliwa kila baada ya miaka mingapi na lini ilifanyika hivyo?


Nimeshalielezea hilo, na wala sijasema kwamba CCM haina mapungufu, lkn angalau wanajitahidi kuyashuughulikia, CCM huwa kuna mijadala mingi, Watu wanahoji mambo mbali mbali lkn chadema ni mwiko!
 
Hata wakina Nyerere walikaa zaidi ya miaka 20 kabla ya kuachia madaraka.
Chama mwanzo wake nimgumu lazima.iwe namizizi safi kwanza.ka la ya kumwachia mwingine.
 
Kwa hiyo unataka tujifunze kuuwa na kiteka watu? Au kuteuwa vichaa wanao jitekenya na kucheka wenyewe?au uwizi wa kutaifisha mali ya watu na kuandika msajili wa majumba?nimesahau kuwa na akili ya kimaskini na kudhani matajiri ni adui zetu?
Rudia kusoma taratibu huu uzi na uutafakari kabla hujajibu utapata kitu, weka mahaba pembeni uruhusu ubongo kufanya kazi
 
Fikiria chadema nayo ingekuwa na Mwenyekiti mpya kila baada ya Miaka 5-10 hamuoni kwamba ingewasaidia kutatua matatizo yenu kwa kuleta mawazo mapya yawe mabaya au hata kama siyo bora kulinganisha na ya uongozi uliopita lkn hii inasaidia Chama kukua na kukomaa!

Sasa hivi ni zamu ya Magufuli na yeye ana timu yake na wana mawazo yao ya jinsi ya kuongoza CCM na haijalishi kama ni mazuri au la lkn moja linabakia baada ya wao kuondoka 2025 CCM itazidi kukomaa!

Sasa chadema Uongozi ule ule kwa zaidi ya miaka 20 mnawezaje kupata Viongozi wazuri kama hamtoi nafasi kwa wengine kuja na mawazo mapya?

I mean msitafute mchawi, ninyi ndiyo tatizo, mnaendekeza Umungu mtu, ...
Unatetea ugali wako
 
Kama ccm inajadili basimnajadili tu yale unayotaka mkuu ayasikie. Siyo kusahihisha maovu kamavile kuua au kupoteza watu.nk
 
Hata wakina Nyerere walikaa zaidi ya miaka 20 kabla ya kuachia madaraka.
Chama mwanzo wake nimgumu lazima.iwe namizizi safi kwanza.ka la ya kumwachia mwingine.


Ok labda uko sawa, lkn Nyerere hakukaa miaka 20 sababu ya ukomavu wa Chama bali mfumo wa wakati huo uliruhusu hilo yaani udikteta,ä!
 
Chadema au vyama vyote vya upinzani wangekua na utaratibu wa kubadilisha viongozi naamini wangekua mbali kuliko walipo sasa tatizo umangi mwingi, vijana wanakuja tena wazuri ila wanazikwa na wahafidhina kama Mbowe na Lipumba, kuna wakati unawaza kwa Mfano pale CUF kijana mwenye maono ya kileo kama Mtatiro kwanini asikabidhiwe chama na wazee wakawa washauri, kwanini kwa Mfano Chadema pale watu kama kina Lissu au hata enzi zile Zitto au hata Mnyika wasingechukua mikoba ya Uongozi, Kama internal dynamism haitapata nafasi tutarajie upinzania dhaifu kila mwaka
 
Vyovyote vile lkn kuna Uongozi mpya unakuja kila baada ya miaka 5-10, na hii ni muhimu kwa ustawi wa Chama kwani kinakaribisha mawazo mapya na pia kutoa fursa ya kujifunza ktkana na Uingozi uliopita na kujaribu kuboresha, sasa chadema hakuna kubadilisha Uongozi mawazo hayo hayo ya watu hao hao kwa miaka zaidi ya 20, mnategemea mabadiliko hapo?

Kwa mfano kwa maoni yangu Mbowe hakupaswa kuwa KUB tena alishakalia hiyo nafasi angetoa fursa kwa wengine pia ili kupima uwezo waona pia kuwapa imani Wanachama wengine kwamba wana nafasi ya kufika juu!
Mkuu umekuja na wazo zuri sema wafu wa ubongo kazi yao ni kupambana na wewe badala ya kujibu hoja
Boss Barbarosa Ukiona hivyo ujue, Mh. Mbowe kawashika pabaya. Kila mnalopanga kuiua Chadema mnashindwa. Kuna mmoja alisema kabla ya Uchaguzi Chadema itakuwa ishakufa kabisa. Mkashindwa na Akashindwa. Sasa hivi mnanunua Wapinzani, Chadema bado ipo.

Ukishaona mpinzani wako anakushauri, tafakari mara mbili mbili.

Ila la kubadilisha Uongozi kwa awamu, nakuunga mkono hoja.

Ila ushauri wangu kwako na kwenu, msiue Upinzani. Upinzani ni mzuri kwa Afya na Ustawi wa Taifa, Taasisi, Kundi, Ndoa, Familia. Bila Upinzani Imara hakuna maendeleo. Na zama za Ndio Mzee zimepitwa na wakati.

Hamasisheni wananchi kufuata Katiba na Sheria za Nchi.
 
Fikiria chadema nayo ingekuwa na Mwenyekiti mpya kila baada ya Miaka 5-10 hamuoni kwamba ingewasaidia kutatua matatizo yenu kwa kuleta mawazo mapya yawe mabaya au hata kama siyo bora kulinganisha na ya uongozi uliopita lkn hii inasaidia Chama kukua na kukomaa!

Sasa hivi ni zamu ya Magufuli na yeye ana timu yake na wana mawazo yao ya jinsi ya kuongoza CCM na haijalishi kama ni mazuri au la lkn moja linabakia baada ya wao kuondoka 2025 CCM itazidi kukomaa!

Sasa chadema Uongozi ule ule kwa zaidi ya miaka 20 mnawezaje kupata Viongozi wazuri kama hamtoi nafasi kwa wengine kuja na mawazo mapya?

I mean msitafute mchawi, ninyi ndiyo tatizo, mnaendekeza Umungu mtu, ...
Acha kufananisha CCM na vitu vya ajabu
 
Mleta uzi kaja na wazo jema sana sema wengi naona wamesoma kama kitini cha hadithi na kuanza kumshambulia, ukweli ni kwamba vyama vyote vya upinzani vingekua vinaruhusu mawazo mbadala wangekua mbali sana, Vijana kama Mtatiro pale CUF wangefaa sana wapewe nafasi mazee kina Lipumba wawe washauri, Chadema huko nako waapo watu wanaowaza kileo lkn hawapati nafasi, wahafidhina wanadumaza siasa yetu kabisa
 
mnanunua wapigakura kwa tishetina kanga mtashindwa nini kununua viongozi-njaa?
Kwa uzumbukuku wako wewe umeona upande mmoja tu wa wanaonunua hujaona kua na wanaokubali kununuliwa ni tatizo...ukitaka kufikiri vyema punguza mahaba upofu na misisimko
 
Lkn tofauti Mungu mtu wa CCM ana ukomo, lkn chadema hakuna na wala hakuna anayejua lini Mbowe utawala wake utafikia ukomo, sasa hilo siyo jambo jema kwa ustawi wa Chama!
Kaka unapoteza muda kuwaelimisha wasiotaka kuelimisha,hawa wamelishwa kasumba,hawaoni wala kusikia juu ya Dj watakuja shtuka kumekucha na hili ndio kosa la hawa madikteta uchwara hawashauriki kisa Dj wao ambaye ni mwenyekiti wa maisha kwenye SACCOS ya mkwewe
 
Lkn tofauti Mungu mtu wa CCM ana ukomo, lkn chadema hakuna na wala hakuna anayejua lini Mbowe utawala wake utafikia ukomo, sasa hilo siyo jambo jema kwa ustawi wa Chama!
Kumbe mwamgwaya Mbowe. Sasa hilo ni janga lenu wenyewe na Mungumtu wenu wa kukurupuka ambae hashauriki.
 
Back
Top Bottom