CHADEMA Kunani?

CHADEMA Kunani?

MAFILILI

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2011
Posts
2,377
Reaction score
1,200
CHADEMA ni muhimili wa upinzani nchini Tanzania hatahivyo wameshindwa kuleta mabadiliko kutokana na mwenendo wao wa kuendesha shughuli za kisiasa kimazoea.

Nachukua fursa hii adimu kuwaasa CHADEMA kupitia kwa Dr Kitila Mkumbo kuwa huu ni wakati muafaka kwa chama chao kuonyesha siasa za dhati kuelekea mabadiliko nchini mwetu ili kuleta maisha bora kwa watanzania. Ili wafikie pahala pa kuwa kielelezo cha mabadiliko nchini yapaswa chama kivae taswiraya chama cha siasa kutoka kwenye taasisi y watu wateule wanaopiga debe la mageuzi ya kisiasa pasipo kuwa na dhamira ya dhati kuwaongoza watanzania. Badala yake CHADEMA kimebaki ni chama kinachoongoza kwa malumbanoi na taasis za kidola kama vile Polisi hivyo ina athari kwa ustawi wa chama kwani watanzania wanaunganisha CHADEMA na maandamano.

Dr. Kitila huu ni wakati muafaka kwa kutoa ushauri kwa Mtendaji Mkuu wa Chama,Dr, Slaa aache dhana ya kutumia maandamano kuwa ni silaha pekee ya kuitoa CCM madarakani. CCM inatakiwa irudi kwa vijana ili CHADEMA wazidi kupotea katika ramani ya kisiasa mkoani Mtwara.
 
siku ccm wakipata kura hata 100 tu MASASI, MTWARA MJINI, NA RUANGWA watakuwa wamejitahidi sana.
 
Kwani maandamano hayaruhusiwi kikatiba???
Ni mara ngapi ccm na jk huandamana sehemu mbalimbali na kuyaita maandamano husika kwa jina la matembezi ya mshikamano???
Nakushauri ukae utulie ujisomee sheria za nchi na kanuni alafu ndo uje kuongea na watu wenye akili timamu.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Magamba yanahofu ya hali ya juu, propaganda zao za kudai CDM ni chama cha kidini, wachaga na kinataka kuleta umwagaji damu nchini zimegonga ukuta, sasa wameamua kupandikiza video ili kuwabambikia kesi Viongozi wa juu wa CDM.

Kweli chadema tishio la magamba ya mamba
 
CHADEMA ni muhimili wa upinzani nchini Tanzania hatahivyo wameshindwa kuleta mabadiliko kutokana na mwenendo wao wa kuendesha shughuli za kisiasa kimazoea.

Nachukua fursa hii adimu kuwaasa CHADEMA kupitia kwa Dr Kitila Mkumbo kuwa huu ni wakati muafaka kwa chama chao kuonyesha siasa za dhati kuelekea mabadiliko nchini mwetu ili kuleta maisha bora kwa watanzania. Ili wafikie pahala pa kuwa kielelezo cha mabadiliko nchini yapaswa chama kivae taswiraya chama cha siasa kutoka kwenye taasisi y watu wateule wanaopiga debe la mageuzi ya kisiasa pasipo kuwa na dhamira ya dhati kuwaongoza watanzania. Badala yake CHADEMA kimebaki ni chama kinachoongoza kwa malumbanoi na taasis za kidola kama vile Polisi hivyo ina athari kwa ustawi wa chama kwani watanzania wanaunganisha CHADEMA na maandamano.

Dr. Kitila huu ni wakati muafaka kwa kutoa ushauri kwa Mtendaji Mkuu wa Chama,Dr, Slaa aache dhana ya kutumia maandamano kuwa ni silaha pekee ya kuitoa CCM madarakani. CCM inatakiwa irudi kwa vijana ili CHADEMA wazidi kupotea katika ramani ya kisiasa mkoani Mtwara.
Unaandika Chadema walete maisha bora kwa kila mtanzania wakati Ccm walioko madarakani wameshindwa kuleta hayo maisha bora kwa kila mtanzania hivi wakati mnaandika humu huwa mnatumia ------ kuandika?

Unasema ccm warudi kwa vijana chama cha wezi kijana gani atarudi huko labda wenye akili zilizooza kama nyie na weeengi ni waganga njaa tu wametoka shule ajira hamna mnabaki kutoa matusi jf imekula kwenu
 
Kidole cha mwisho. Juuuuuu!!!!!!! Piga ua chadema madarakani lazima ccm jipangeni xna 2015 2mepania ile mbaya
 
.Badala yake CHADEMA kimebaki ni chama kinachoongoza kwa malumbanoi na taasis za kidola kama vile Polisi hivyo ina athari kwa ustawi wa chama kwani watanzania wanaunganisha CHADEMA na maandamano.
mkuu hebu tufafanulie juu ya kauli yako hii with the key point:
a) CDM ndiyo waanzilishi wa malumbano hayo na vyombo vya dola? toa mifano hai
b) Dhana ya kuandamana ni nini hasa kwa chama cha siasa?

katika majumuisho yako, ainisha wajibu mkuu wa chama cha upinzani - na kama kinaonewa / kupokwa haki na dola je ni wapi mahala pa kupeleka malalamiko yao mbali na mahakani? kwa njia ipi?

Majibu ya point hizi yatasaidia hoja yako iwe na uzito.(ijadilike)
 
CHADEMA ni muhimili wa upinzani nchini Tanzania hatahivyo wameshindwa kuleta mabadiliko kutokana na mwenendo wao wa kuendesha shughuli za kisiasa kimazoea.

Nachukua fursa hii adimu kuwaasa CHADEMA kupitia kwa Dr Kitila Mkumbo kuwa huu ni wakati muafaka kwa chama chao kuonyesha siasa za dhati kuelekea mabadiliko nchini mwetu ili kuleta maisha bora kwa watanzania. Ili wafikie pahala pa kuwa kielelezo cha mabadiliko nchini yapaswa chama kivae taswiraya chama cha siasa kutoka kwenye taasisi y watu wateule wanaopiga debe la mageuzi ya kisiasa pasipo kuwa na dhamira ya dhati kuwaongoza watanzania. Badala yake CHADEMA kimebaki ni chama kinachoongoza kwa malumbanoi na taasis za kidola kama vile Polisi hivyo ina athari kwa ustawi wa chama kwani watanzania wanaunganisha CHADEMA na maandamano.

Dr. Kitila huu ni wakati muafaka kwa kutoa ushauri kwa Mtendaji Mkuu wa Chama,Dr, Slaa aache dhana ya kutumia maandamano kuwa ni silaha pekee ya kuitoa CCM madarakani. CCM inatakiwa irudi kwa vijana ili CHADEMA wazidi kupotea katika ramani ya kisiasa mkoani Mtwara.

Taratibu magamba mnaamka...........
 
Back
Top Bottom