PreGE2025 CHADEMA kuijadili barua ya Msajili Juni 3.2025

PreGE2025 CHADEMA kuijadili barua ya Msajili Juni 3.2025

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,481
Reaction score
14,841
Kamati Kuu ya CHADEMA imepanga kukutana tena June 03, 2025 kujadili barua ya Msajili wa Vyama vya siasa kisha itatoa mwelekeo

Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche akiongea Jijini Arusha leo July 28,2025 amesema "Mmemsikia Msajili wa Vyama ameifutia CHADEMA ruzuku, ametishia kukifuta Chama cha CHADEMA, maamuzi tuliyotoa May 23 na May 24 ni maamuzi ya Kamati Kuu sio ya kwangu, tumeitisha Kamati Kuu ya Chama June 03,2025 tunarudi Mkutano Mkuu kujadili barua ya Msajili na tutatoa mwelekeo"

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Itakumbukwa jana May 27,2025 Msajili wa Vyama vya siasa nchini Tanzania alitangaza kusitisha kutoa ruzuku kwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hadi pale watakapotekeleza maelekezo ya Ofisi ya Msajili kutokana na Msajili kusema Chama hicho hakina Viongozi wanaoweza kusimamia mapato, matumizi na marejesho ya fedha hizo za Umma ambapo hatua hii ilikuja siku mbili tangu Kamati Kuu ya CHADEMA iazimie kuwa haitofuata uamuzi wa Msajili wa kutengua uteuzi wa Wajumbe wanane wa Sekretarieti na Kamati Kuu ya Chama hicho waliothibitishwa na Baraza Kuu la Chama hicho January 22,2025.

 
Huyu Msajili katumwa epukeni shari yake kwa kumpandisha kizimbani.
 
Mabenki na kampuni zote za simu zisitishe miamala ya fesha kwenda chadema kwa kuwa sasa hivi haina uongozi. Vinginevyo Heche atakula anabapula tu hela za chama
 
Back
Top Bottom